Masikini watumishi Serikalin!!!!

Mvaa Tai

JF-Expert Member
Aug 11, 2009
6,159
4,443
Kuna nyepesi zinasema Serikali ilitenga katika bajeti yake karibu Tshs Billion48 kwa ajili ya mikopo kwa watumishi wa Serikali ili waweze kununua vitu kama Magari, Samani za ndani na Matengenezo ya magari. Inasemekana katika kiasi hicho ni zaidi ya Billion32 karibu 70% zimekopeshwa kwa wabunge tuu, kiasi kinacho baki yaani chini ya 30% ndicho kitakachokopeshwa kwa watumishi woote serikalini nchi nzima. na mbaya zaidi inasemekana kiasi cha 90,000,000 alichokopeswa kila mbunge kwa wabunge karibu 360, yaani 360x90,000,000=32.4Bn ni nusu tuu ndo mbunge anatakiwa kuirudisha kama mkopo, inayobaki atalipiwa na serikali.

Swali linakuja, kama haya ni ya kweli ni kwanini wabunge wamepewa kipaumbele kiasi hiki?
 
Kama kiasi hicho ni kweli basi watumishi tume kwisha. Maana, kiasi kilicho baki hakitoshi chochote.
 
Kama kiasi hicho ni kweli basi watumishi tume kwisha. Maana, kiasi kilicho baki hakitoshi chochote.

Hizo tetesi hata mimi nilizipata siku nimepita pale hazina upande wa Advances, nadhani zitakuwa na ukweli ndani yake lakini tuiachie serikali maana ndo inajua mipango yake juu ya maslahi ya watumishi wake
 
hizo pesa wabunge wanapewa zanini?ukisema magari mbona wanayo kwanini uwape pesa inamaana mbunge kila baada ya miaka 5 ananunua gari?kwanini wasipewe wale wabunge wapya tu?huku ni kuchezea pesa kwa nchi kama tanzania yaani kila baada ya miaka 5 serikali inawapa wabunge magari mapya kweli hapo umaskini utaisha kweli?
 
kwa staili hii ndo maana tunarudi enzi hizooo! Ubinafsi na ufisadi ndo ulowajaa viongozi wetu... Uozo mtupu!
 
Kipaumbele kilitakiwa kiwe kwa walimu,madaktari,mahakimu na maafisa ugani sio wabunge.
 
Kwa nini kila kitu wanapendelewa wabunge tu!
asante kwa swali zuri lenye jibu wazi......wanalipa fadhila kwa wana CCM wao, umeshahu kuwa wana wabunge kibao huko mjengoni?? wanaendekeza utabaka...yaani ili ikija suala la kuchangia chama wawe kataka good position..na sio kujenga nchi
 
hizo pesa wabunge wanapewa zanini?ukisema magari mbona wanayo kwanini uwape pesa inamaana mbunge kila baada ya miaka 5 ananunua gari?kwanini wasipewe wale wabunge wapya tu?huku ni kuchezea pesa kwa nchi kama tanzania yaani kila baada ya miaka 5 serikali inawapa wabunge magari mapya kweli hapo umaskini utaisha kweli?

Nani angetoa hiyo proposal maana hata Waziri wa fedha naye ni mbunge wa zamani, kwahiyo unamaanisha angependekeza kwamba wabunge wa zamani wasipewe ili na yeye asipate? au waziri mkuu anaweza akapendekeza mbunge wa zamani asipate ili nayeye asipate?
 
hivi kwani wabunge wana thamani kuliko walim, madaktari, manjinia, wa sosiolojia n.k???
Hivi kwa hali hii kwa ninitusipate hasira na kusapot CHADEMA??
Kwa nini tusikate tamaa kiasi cha kuwachukia viongozi wetu toka mkuu wao hadi yule wa mwisho anaewasapo, hata tukatamai kua na uwezo wa kuwatoa duniani kabisa??
Hivi wabunge 360, watachukuaje 70% af watumish wanaokadiriwa kua 300,000 wachukue 30%??
Hivi haya ni mahesabu gani?? hivi huu sio uungu utu?? hivi sisi kuendelea kukubali hal hii sio kukosa utimamu jamani!!

OOOshhh!! i hate this system.Hivi zile serikali za kijasusi si zitusaidie kuwaondoa hawa mapapa wanaotumaliza viperege humu baharini jamani??
 
Huo ndio ukweli kwani hata mie nimeongea na Mhe. mmoja akasema wao wanastahili kulipa 9m/= kwa mwaka kwa miaka 5 ni 45m/=. Kwa hiyo ni kweli wanalipa nusu ya deni wale wafanyakazinwengine ndio imekula kwao. hii ndio serikali yetu
 
Jamani wana JF mnaambiwa mwenye nacho huongezewa na asiyekuwanacho hunyang'anywa na hata kile kidogo alichonacho, pia wanaangalia kibanzi kilichopo kwenye jicho lao kwanza ndio waangalie katika jicho la watumishi. Ila haya yoote yana mwisho
 
hizo mbona nying sana, tushazoea watumishi ni jalala, lakin nina iman kuna cku watajua umuhimu wetu tu, tukiingia rroad watajua tu
 
Back
Top Bottom