KakaJambazi
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 18,711
- 12,067
Tushafanya maamuzi.
Dada huyu unayemwita katibu wa chadema alihamia ACT Wazalendo muda mrefuNi kweli chombo chenu kinaweza kwenda bila hata nahodha..,ndio maana hamuoni tofauti baina ya nahodha kipofu na kutokuwa na nahodha kabisa.
watakao bakia chadema ni wenye mihemko ya kisiasa na si vinginevyo, kwa sababu ukweli wanaujua lakini wana kumbatia uchafu, wenye akili timamu wanazidi kuondoka.hongereni mnaotoka huko si mahala salama
Huyu jamaa alishahamia ACT wazalendo zamani sana. Imekuaje aseme katoka CHADEMA na asiseme ACT?
CHADEMA yazidi kudhoofika,viongozi Urambo wajivua magwanda
Hakika BUNDI ametua na kujenga kiota katika nyumba ya jirani, kama ni mkosi basi huu ni Babu kubwa..Katibu Mwingine wa Wilaya akihama CHADEMA na kujiunga na CCM wilayani Urambo.
Katika hali isiyo ya kawaida Katibu wa Wilaya ya Urambo wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Ndugu Obedi Malola amekihama Chama hicho na kujiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM) huku akisema "UKWELI" mchungu juu ya kile kinachoendelea ndani ya Chadema.
Katibu huyo wa Wilaya - CDM (aliyehama) ameeleza sababu zilizomuhamisha CHADEMA kuwa;
1. CHADEMA imeacha misingi yake ya kutetea wanyonge na masikini wa nchi hii, na badala yake imeanza kutetea na kusafisha wezi, wanyonyaji na walanguzi wa nchi hii.
2. Amesema ameshindwa kumvumilia MBOWE aliyeamua kuiuza CHADEMA kwa mafisadi, yeye si sehemu ya wizi wa nchi hii, hayuko tayari kusafisha na kutetea wezi na wala rushwa.
3. Amesema CHADEMA inapokea ruzuku milioni 334, lakini ofisi ya CHADEMA ya wilaya hiyo inadaiwa pango na kwamba wametupiwa vifaa vya ofisi nje.
4. Pia, amesema CHADEMA wapo watu wema, lakini kwa woga wameamua kukaa kimya wakati MBOWE akikipoteza chama hicho, yeye haogopi na kwamba anajua kwa HAKI na UKWELI kuwa MAGUFULI atakuwa Rais bora wa nchi hii..ameiona kazi yake na anaamini ni CHAGUO SAHIHI.
Amtaka MAGUFULI akishaapishwa, baada ya kumaliza Hotuba yake bungeni apitishe na muswada wa kuanzisha mahakama ya wezi na mafisadi ili kabla mwaka huu haujaisha Wezi na mafisadi wawe wameshapelekwa jela;
NB:
Hii hapa VIDEO kamili ya alichokiongea Katibu Huyo mbele ya Umati wa wananchi wa Urambo.
Mtaji wa wana siasa ni umaskini wa watz ... hivi kweli urambo mnakubali muongozwe na familia moja miaka nenda rudi na hali umaskini ukizidi? duuuu
Hakika BUNDI ametua na kujenga kiota katika nyumba ya jirani, kama ni mkosi basi huu ni Babu kubwa..Katibu Mwingine wa Wilaya akihama CHADEMA na kujiunga na CCM wilayani Urambo.
Katika hali isiyo ya kawaida Katibu wa Wilaya ya Urambo wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Ndugu Obedi Malola amekihama Chama hicho na kujiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM) huku akisema "UKWELI" mchungu juu ya kile kinachoendelea ndani ya Chadema.
Katibu huyo wa Wilaya - CDM (aliyehama) ameeleza sababu zilizomuhamisha CHADEMA kuwa;
1. CHADEMA imeacha misingi yake ya kutetea wanyonge na masikini wa nchi hii, na badala yake imeanza kutetea na kusafisha wezi, wanyonyaji na walanguzi wa nchi hii.
2. Amesema ameshindwa kumvumilia MBOWE aliyeamua kuiuza CHADEMA kwa mafisadi, yeye si sehemu ya wizi wa nchi hii, hayuko tayari kusafisha na kutetea wezi na wala rushwa.
3. Amesema CHADEMA inapokea ruzuku milioni 334, lakini ofisi ya CHADEMA ya wilaya hiyo inadaiwa pango na kwamba wametupiwa vifaa vya ofisi nje.
4. Pia, amesema CHADEMA wapo watu wema, lakini kwa woga wameamua kukaa kimya wakati MBOWE akikipoteza chama hicho, yeye haogopi na kwamba anajua kwa HAKI na UKWELI kuwa MAGUFULI atakuwa Rais bora wa nchi hii..ameiona kazi yake na anaamini ni CHAGUO SAHIHI.
Amtaka MAGUFULI akishaapishwa, baada ya kumaliza Hotuba yake bungeni apitishe na muswada wa kuanzisha mahakama ya wezi na mafisadi ili kabla mwaka huu haujaisha Wezi na mafisadi wawe wameshapelekwa jela;
NB:
Hii hapa VIDEO kamili ya alichokiongea Katibu Huyo mbele ya Umati wa wananchi wa Urambo.