Nani kawapa leseni ya kufanya biashara?
Ni wajibu wa nani kukusanya kodi?
Kodi zenu indeed!
Nani kawapeleka bungeni?
Hizo kodi zenu wanazokula, wanaiba au wanapewa?
masopakyindi, ihurumie nchi yako na wahurumie Watanzania...yawezekana huna habari kuwa Chadema hawajawahi kukamata dola! Haijawahi kutokea popote duniani eti bajeti ya Upinzani ikajadiliwa bungeni, ni hapa Tanzania tu ambapo hata kwa akili ya kawaida, ujinga unaofanywa na Wabunge wa CCM unaweza kuvumilika na masopakyindi akashangilia...kweli, the country has gone to the dogs!
Baada ya bajeti hii kupita kwa kishindo, CDM itakuwa imevunja rekodi ya kuwa Chama kinachosimamia mambo hewa yasiyokuwa kila kukicha, itabidi sasa wabadili jina!!! Napendekeza kiitwe CHAMA HEWA!!... bahati mbaya sana cdm kimeshindwa kukwepa hatima hii mbaya na mbovu..
Una roho ngumu mdogo wangu, lakini nafikiri kuna mambo ya msingi huwezi kuyatilia maanani kwa sababu huyajui kwani huyaoni na hata ukiyaona hutayatambua. Haya yote ni matokeo ya athari ya tume iliyoundwa tarehe 28 Januari, 1964 na kutoa ripoti yake tarehe 22 Machi, 1965. Tupo wengine wetu tuliokuwepo wakati huo ambao pamoja na nia nzuri ya Mwalimu ya kujenga taifa lenye umoja, tuliona athari ambazo hadi leo zinaendelea kuwatafuna Watanzania wenzetu kama wewe.
Mwalimu alipotaka kung'atuka mwaka 1975, hofu kubwa ilitanda nchini swali kubwa likiwa je, Tanzania bila Mwalimu inawezekana? Miaka kumi baadaye iliwezekana na Ali Hasan Mwinyi akawa Raisi wa pili Tanzania! Mwalimu huyo huyo kwa kutambua kwamba ili dunia iendelee kuwapo mabadiliko hayazuiliki, hakusita kuunga mkono upepo wa mageuzi. masopakyindi, kwa kipindi kirefu Watanzania walio wengi walikuwa wameathirika kiasi cha kutokuwa tayari kupokea mfumo nje ya ule waliouzoea.
Watawala wakatumia kikamilifu uoga wa ujinga wa wananchi walio wengi kuwaaminisha kuwa Tanzania bila CCM haiwezekani. CCM ndiye baba, ndiye mama na ndiye mlinzi wa amani na utulivu. Kwa leo naacha hapa masopakyindi, ila ukae ukijua kuwa moto wa mabadiliko hauzimwi kwa ubabe, hauzimwi kwa ulaghai na hauzimwi kwa kubeza mwamko wa wananchi. CCM inaelekea kubaya na kadri siku zinavyosonga ndivyo hali inazidi kuwa mbaya...watanyanyasa na hata kuua lakini yote ni kama kumwaga petroli motoni!
Wewe kweli mzalendo k... sasa sijui kirefu cha hyo K nini??
Kumbe ndio sababu. Kumbe hujaenda shule ndio maana mawazo yako ni duni kiasi hiki!!!!! Kweli CCM imetuangusha, miaka 50 ya uhuru bado adui ujinga anasumbua watu!!!! Afadhali umetujulisha hilo ili tusikulaumu bure. Watu kama wewe ndio mtaji wa CCM. Lakini wasomi na wajanja ni mwiba mkali kwa hao magamba. Pole sana ndugu yangu. Lakini zama za ujinga zinahesabika. Zitakoma siku Chadema itakapoingia madarakani.
Hiyo "K" kwenye jina lako inasadifu uliyoyaandika bz unawaza kwa kutumia masaburi
"K"~~masaburi
masopakyindi, mbona hakuna hata kimoja nilichosema ambacho unakipinga? UnasemaIs that so!
Mkuu Mag3, unarudia kosa lile lile la watu wanaojaribu kudistort historia ya nchi hii ili ku achiieve their own narrow goals.
Achana na mambo ya 1963 hadi 1965, na 1975-hapo tutawapoteza wengi tu humu JF.
Usijidai kuwa ulikuwepo peke yako , tulikuwepo wengi tu!
Turudi hapa karibuni, 1991.
Ever heard of Tume ya Nyalali?
Tume ya Rais ya kukusanya maoni juu ya kuanzisha vyama vingi nchini?
Tume ya Nyalali ilibaini kuwa asilimia 80 ya maoni ya Watanzania yalionyesha wangependa kuendelea na mfumo wa chama kimoja, na asilimia 20 tu ndio waliotaka yafanyike mabadiliko ya kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi.
Hata hivyo, kwa kuzingatia ukuaji wa demokrasia duniani, pamoja na maoni ya wengi (80%) kutaka tuendelee na mfumo wa chama kimoja, Tume ya Nyalali, kwa busara zake, ikapendekeza kwamba ni vema nchi yetu ibadilike na kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi.
Tume hiyo iliwasilisha Taarifa yake kwa Rais mnamo tarehe 17 Februari,15 ,1992 na kusababisha nchi kubadili rasmi mfumo wake wa siasa kutoka chama kimoja na kuwa na mfumo wa vyama vingi mnamo tarehe 1 Julai, 1992.
Na ni baada ya hapo ndio kukazaliwa vyama kama NCCR, TADEA, CUF CHADEMA etc na utitiri mwingi tu!
Mbadailiko yote haya yalifanyika chini ya uangalizi wa kisiasa wa CCM na serikali yake.
Sasa leo, Mag3, unakuja na baseless allegations kuwa ati, I quote,
"Watawala wakatumia kikamilifu uoga wa ujinga wa wananchi walio wengi kuwaaminisha kuwa Tanzania bila CCM haiwezekani. CCM ndiye baba, ndiye mama na ndiye mlinzi wa amani na utulivu"
I am sorry , but such statements make me sick, more so when it comes from one whom I thought to be head and shoulders above small time petty thinkers.
Na mimi nilisema hivi, kwa kipindi kirefu Watanzania walio wengi walikuwa wameathirika kiasi cha kutokuwa tayari kupokea mfumo nje ya ule waliouzoea. Je ndugu yangu kama ulikuwepo, unakumbuka nguvu nyingi iliyotumika kupinga mageuzi yasitokee Tanzania? Unakumbuka kampeni iliyofanywa na CCM kuwaomba, kuwaonya na kuwatisha wanancnhi kuhusu athari ya vyama vingi?Tume ya Nyalali ilibaini kuwa asilimia 80 ya maoni ya Watanzania yalionyesha wangependa kuendelea na mfumo wa chama kimoja, na asilimia 20 tu ndio waliotaka yafanyike mabadiliko ya kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi.
Baada ya bajeti hii kupita kwa kishindo, CDM itakuwa imevunja rekodi ya kuwa Chama kinachosimamia mambo hewa yasiyokuwa kila kukicha, itabidi sasa wabadili jina!!! Napendekeza kiitwe CHAMA HEWA!!... bahati mbaya sana cdm kimeshindwa kukwepa hatima hii mbaya na mbovu..
masopakyindi, mbona hakuna hata kimoja nilichosema ambacho unakipinga? Unasema Na mimi nilisema hivi, kwa kipindi kirefu Watanzania walio wengi walikuwa wameathirika kiasi cha kutokuwa tayari kupokea mfumo nje ya ule waliouzoea. Je ndugu yangu kama ulikuwepo, unakumbuka nguvu nyingi iliyotumika kupinga mageuzi yasitokee Tanzania? Unakumbuka kampeni iliyofanywa na CCM kuwaomba, kuwaonya na kuwatisha wanancnhi kuhusu athari ya vyama vingi?
Kwa mara ya kwanza kabisa TV zikiwa zimeruhusiwa ja unakumbuka vipindi vya ITV na CTN kuhusu vurugu na mauaji ya Rwanda ili kuwaogopesha wananchi juu ya harati ya vyama vingi? masopakyindi unakumbuka ziara za Waziri Mkuu, John Cigwiyemisi Samweli Malecela chini kuwaonya, kuwatisha na kuwafananaisha wanamageuzi na sisimizi? Je, kulikuwepo na ulazima wa kuundwa kwa tume ya Nyalali kuwauliza wananchi kama wanataka uhuru zaidi? Unakumbuka kuwa kuna mwanamageuzi, Mabere Nyaucho Marando alimkatalia Mwinyi uteuzi wake kwenye tume na sababu alizotoa?
masopakyindi, unasema ninapotosha historia na kwamba ulikuwepo, naomba nikuulize swali, je Mwalimu asingewakemea viongozi na kusema kuzungumzia vyama vingi si dhambi, Mwinyi angeunda tume? Je unakumbuka juhudi za Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa mambo ya ndani, Agostino Lyatonga Mrema, kupambana na wanamageuzi? Unakumbuka FFU ilivyotumika kuzima harakati za wanamageuzi na kuwapa vilema vya maisha wengine kwa kudai uhuru wa mawazo tu? Ndugu yangu unadai napotosha historia, jibu haya halafu tuendelee!
Phew! I almost made the greatest mistake of my life. I almost thought you were for real masopakyindi kumbee... ni wale wale! Unaweza kusemaje kuwa, kama kuna viongozi-tena wazito, walilipinga hilo, hizo zaweza kuwa sababu za kibinafsi zaidi kuliko matakwa ya umma...! Wakati huo huo unasema asilimia 80% ya huo umma ulionyesha wangependa kuendelea na mfumo wa chama kimoja! Je unakumbuka tamko rasmi la CCM kuhusu mageuzi kabla hawajakemewa na Mwalimu? Vyoyote vile utakavyodai, ukweli ni kuwa CCM ililazimika kupokea mageuzi shingo upande na si kwa mapenzi yake, waliyaogopa na wanaendelea kuyaogopa hadi leo.Mkuu Mag3, siasa is never static...
Kama ilivyo mawazo ya binadamu, siasa vile vile hubadilika kutokana na mazingira yanayowasibu wananchi wake.
Kwa hiyo kama kuna viongozi-tena wazito, walilipinga hilo hizo zaweza kuwa sababu za kibinafsi zaidi kuliko matakwa ya umma...
Mara zote wapinzani wameona ni sifa kubwa KULAUMU TU bila kuwa na sera mbadala, sera ambazo hata leo hawana.
Kwa sasa hivi mimi binafsi sijaona chama chenye uwezo,umahiri, na hata utaalam wa kuendesha serikali, na wabakie kukosoa tu kwa afya yao.
Well,masaburi yako yamejaa HEWA
Wataingia madarakani siku watanzania walio wengi watakapowapitia kura za ndiyo. Hii ina maana kwamba ni lazima watanzania walio wengi wawe wameelimishwa na kuelewa umuhimu wa mabadiliko ya kisiasa kwa ajili ya maendeleo yao.Naomba kuuliza,hivi CDM wataingia lini madarakani?