Phew! I almost made the greatest mistake of my life. I almost thought you were for real
masopakyindi kumbee... ni wale wale! Unaweza kusemaje kuwa, kama kuna viongozi-tena wazito, walilipinga hilo, hizo zaweza kuwa sababu za
kibinafsi zaidi kuliko matakwa ya umma...! Wakati huo huo unasema asilimia 80% ya huo umma ulionyesha wangependa kuendelea na mfumo wa chama kimoja! Je unakumbuka tamko rasmi la CCM kuhusu mageuzi kabla hawajakemewa na Mwalimu? Vyoyote vile utakavyodai, ukweli ni kuwa CCM ililazimika kupokea mageuzi shingo upande na si kwa mapenzi yake, waliyaogopa na wanaendelea kuyaogopa hadi leo.
Vipengele vyote vilivyopendekezwa na tume ya Nyalali kuwa vilikuwa vina ulazima wa kufanyiwa kazi kabla ya mfumo rasmi wa vyama vingi kupitishwa vilikataliwa na serikali ya CCM, kwa nini? Misingi ya kuhakikisha kuna haki na usawa katika kuendesha siasa ya vingi haikuridhiwa na serikali ya CCM, kwa nini? Huwezi kuzaa mtoto ukamnyima lishe bora na bado ukategemea mtoto awe na afya nzuri! Lakini daima usisahau matunda ya mateso anayopata na hatari itakayokukabili kama huyo mtoto pamoja na taabu zote hizo ata"prevail" , usishangae akikukana!
Kazi ya vyama vya upinzani duniani kote ni kukosoa na kama upinzani unainyima CCM usingizi kwa hili, basi upinzani unatimiza wajibu wake ipasavyo. Hivi unaelewa sera ni nini? Sera ni maneno tu na bila matendo sera haina maana yoyote, sera ya upinzani itaonekana wakishika madaraka. Hii inanikumbusha watu wanaotaka kutoana macho eti kwa bajeti mbadala uliotolewa na Mh. Zitto halafu watu wenye mawazo kama yako eti wakaanza kuijadili na kuikosoa!
masopakyindi, huu ndio ulimbukeni at its best, unaikosoa au kuijadili ili iweje? Matokeo yake...fisadi Ngeleja kutuzwa bungeni!
Mkuu uko katika mapenzi!
Mapenzi yako kwa CHADEMA yanakufanya usiweze kufikiri critically, kama watu wengi walio katika mapenzi.
Tatizo lako kubwa , na la CHADEMA vile Vile ni chuki yao kwa CCM.
Hili haliwaongezei afya wala shibe, badala yake linawaongezea vocabulary ya matusi ambayo kwa umma wa Kitanzania inawaona kuwa wehu.
Tulitegemea kuwa baada ya kebehi, matusi na kwa ujumla vurugu za hapo Bungeni, CHADEMA ingepanda chati.
Lakini imekuwa tofauti, wananchi wengi wanataka utendaji makini wa serikali si vijembe na umahiri wa kutukna.
Tukirudi kwenye mchakato wa kuanzisha vyama vingi, inaelekea sasa wewe aidha hukuwepo au hukuwa unaelewa nini kinaendelea. Viongozi wengi kama si wote waliingia madarakani kwa kupitia mgongo moja tu wa CCM.
Katika vyombo vyote vya serikali, kulikuwepo kada msimamizi wa sera ya chama, iwe jeshini, polisi,mawizarani, mikoani na kote kwingineko.
Sasa unaposema leo(1991) tuingie vyama vingi, reaction ya hao wanao simama sera za chama wanaenda wapi?
Na hapo ndo nikakupoteza.
Wale makamisaa majeshini, mawizarani, mikoani-kwa maslahi yao wangependaje mabadiliko hayo, na ndiyo ajir yao?
Kama hukuelewa hiyo contradiction basi pengine wakati huo ulikuwa kinda!
Zaidi ya hapo, nafikiri hata maana ya sera huelewi.Sera!Policy!
Mkuu, CHADEMA bila policy inayoeleweka mtaendelea kutwanga maji kwenye kinu.
Na uelewe vizuri tu kuwa ukiwa na Policy baada ya hapo unakuwa na mikakati ya utekelezaji wa Policy hiyo.
Sasa CDM haina sera wala mikakati, na ndio maana tuna wauliza sera zenu kuondoa umasikini- mna jibu CCM ina matatizo!
SerA zenu ya viwanda-mna jibu CCM ina matatizo!
Sera zenu z mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa- mna jibu CCM ina matatizo!
Sera yenu ya ulinzi na usalam- mna jibu CCM ina matatizo!
Sera siyo siri za mwenyekiti wa CHADEMA, ziwekeni wazi wananchi wazijue na wawaelewe.
Najua mna pata matatizo maana hamna hata think tanks wa kitaifa wenye uwezo wa kutengeneza maono ya mbele kwa watanzania.
Na ndio maana hata Zitto kuachiwa kutoa ugoro ule Bungeni majuzi, ume expose serious flaws katika utendaji kichama, kwa CDM.
Endeleeni kuisahihisha CCM, ili kibaki kuwa chama pekee chenye uwezo wa kuongoza, kukosolewa na kujisahihisha.