Mashindano ya ubora wa bangi

Mashindano ya ubora wa bangi

Natamani kupeleka sample toka shambani kwetu kule Bunchari, tuna ekari kadhaa. Ila nahisi nikipeleka nitakuwa nimejipeleka selo mwenyewe bila kushurutishwa na mtu.

Et mura omweito Excel nifanyeje?

Hakukamati mtu.......si unaonyesha tiketi kwamba unaenda kutangaza nchi.........mpaka bendera utapewa............hii ni Tanzania bana.........
 
utamu wa ngoma ucheze kwa step utapenda ila ukiwa na papara hufaidi kitu......kama una mtu wako wa karibu au ndugu kama anasumbuliwa na pumu mpe dozi ya mmea kutwa moja mara mbiliiii.....😛😛😛😛

Midomo yao imepauka kama mmoja wa maraisi wa nchi za east Africa.
 
Aisee....nini kimeingizwa kwenye 'msuba', kiasi cha watu kuwa tayari kungoana kucha...!? Au mnafidika na biashara hii haraamu?

BlackBold: Yawezekana zisipatikane tafiti zilizoko kwenye maandishi kwa muda, lakini kwa watumiaji wa kilevi hiki amadhara yanayowapata kitaa...sisi tulioko huko tunashuhudia wanavyoharibikiwa.

Msimamo wangu uko pale pale:


UVUTAJI WA BANGI NA UTUMIAJI WA AINA NYINGINE YA MADAWA YA KULEVYA NI HATARI KWA AFYA YAKO YA MWILI NA KIAKILI; PIA NI HATARI KWA NDUGU ZAKO JAMAA ZAKO, KIZAZI CHA SASA NA VIZAZI VIJAVYO.

KOMESHA KWA NGUVU ZOTE MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA

Hakuna anayepigania biashara, tunapigania matumizi salama kwa afya na imani yetu. Bangi sio biashara haramu ya mamilioni, walimaji wa jani ni wakulima masikini wa kawaida, wauzaji, wasambazaji ni watu wa kawaida kabisa... Hakuna cha ajabu katika jani, zaidi ni baraka.

Inashangaza kuona watu wamehalalisha sumu, madhambi na upuuzi mwingine wenye nasaba na shetani lakini majani wanayaona tatizo sana.

Amkeni watu wa mungu, jiungeni kwenye harakati!
 
bangi inatibu nini? mods hebu futa hii thread ya wahalifu

Uhalifu ni settings tu, kuna wakati wapiganaji wa uhuru walikuwa wahalifu kwa Serikali za kikoloni, lakini leo ndio mashujaa wa kukumbukwa.

Bangi inatibu vingi, tukianza kuchunguza inabidi tuwe na uzi mwingine maalumu. Kwa sasa tufanye meditation... PUFF PUFF!
 
have you ever heard someone overdose on marijuana??sasa kanywe chloroquine arobaini uje utuambie kipi kibaya
 
Karibuni Jamaika camp uone balaa supu ya utumbo wa ng"ombe wenye mavimavi kidogo jumlisha kitu kutoka tarime yaani unajiona upo mbinguni mwenye kichwa cha panzi lazima uzimike au unye hapohapo
 
Mtu alievuta bangi na kuchanganyikiwa basi lazima alichangantiwa na madawa ya kulevya.
Wahuni wanafanya hivyo ili kuongeza ile HIT. Lakini original mmea wenyewe, uvunwe ukiwa tayari, na ukaushwe taratibu ila sio chini ya direct sunlight, kwa kweli huleta ufunuo wa maisha kwa ninavyosikia.
 
Cha Moro lazima kichwa kigonge na cha tabora lazima usikie njaa.
Arusha wamejitahidi unakuwa uko HIGH ila twende mbele turud nyuma kitu cha Malawi ni kwere.
Nashkuru sasa hivi nimeacha kula Mmea nimeelekea kwa Yesu

Umenikumbusha miaka hiyo ya 90's, usiku tunakaa kilinge maeneo ya Igogo/Igoni aka Umafiani, Mwanza. Huyu katoka Bugarika, huyu Bugando nkali, yule Bugando mishen, huyu, mabatini, mwingine katoka Igoma, mwingine Kirumba, mwingine Nera, Ghana na Mkuyuni.
Huyu anakuja na cha Tarime, huyu cha Arusha, yule cha Tabora, cha Bukoba, cha Musoma, cha Uganda alafu tunamalizia na cha Somalia, yani ilikuwa ni full kujilipua na mastori meeeeengi mpaka kunakucha, asubuhi watu wote macho mekunduuuu vichwa viko HIGHER yani burudaaaani watu kula ujana.

Kwa kweli asante Yesu kwa wokovu, haya makitu yangetupeleka shimoni wengine.
 
ImageUploadedByJamiiForums1416095506.104156.jpg
 
Wewe laki si pesa utakuwa na matatizo makubwa, wahalifu ni wewe na genge lako mnaouza na kulamba unga kama nyoka:evil:
 
Last edited by a moderator:
Ngoja nipeleke cha Tarime yaani unakitoa shambani kibichi na cha kijani halafu unachimba shimo unaweka matawi ya migomba chini unaweka kitu unamalizia na matawi unafukia siku saba baada ya hapo unakitoa kinakuwa kimeiva kimeiva kimekuwa cha njano unakitoa unakipeleka unakiweka

kwenye choo shimo ndani mpaka kinanyauka na kukauka ukikitoa hapo mtu akavuta lazima avue nguo Asante bhangi umetusomesha wengi na hauna madhara mengi kama sigara.

Kitu cha msumbiji kinavyo andaliwa mi hoi halafu ni kikali niaje ukivuta kichwa kichwa bila kula unaweza ukachukua jembe ukaanza kulima mtaa wa kongo kariakoo.

Una kuta shamba kubwa limestawi ganja balaa,then siku ya kuvuna wanachukua mbuzi wana washindisha na njaa kutwa nzima,siku inayo fuata wanaenda kuwa fungia kwenye shamba la bangi,wakisha shiba jioni wanaenda kufungiwa kwenye chumba chenye sakafu wakinya kile kinyesi chote kinakua cha bangi tupu kazi hapo ni kusaga tu na kuvuta kudadeki unaweza ukaomba poo.
 
'Jani likulie milimani kwenye baridi na maeneo ya mawe mawe....au miamba....' pafu moja tu kama unaanza uvutaji, unafyatuka palepale nakuanza kutembea umeina ukiulizwa kwa nini unatembea umeinama unawajibu...nyie hamuoni hiyo mbingu ilivyo karibu nikitembea wima wima sitanigonga kichwa.!!

UVUTAJI WA BANGI NA UTUMIAJI WA AINA NYINGINE YA MADAWA YA KULEVYA NI HATARI KWA AFYA YAKO YA MWILI NA KIAKILI; PIA NI HATARI KWA NDUGU ZAKO JAMAA ZAKO, KIZAZI CHA SASA NA VIZAZI VIJAVYO.

KOMESHA KWA NGUVU ZOTE MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA

Kitu cha malawi ukibahatika ambacho hakijachakachuliwa kinakuwa kama nta.halafu kinafuata kitu cha R chuga hiyo stiki hatari.MMEA ULETAO MAARIFA
 
Back
Top Bottom