chabuso
JF-Expert Member
- Feb 18, 2013
- 6,379
- 5,887
Kwa muda huu katika mitandao ya kijamii habari zinazozngumzwa ni vipi Maaskofu na wachungaji wa dini ya Kristo wanavyomkosoa Raisi Magufuli vipi anavyoingoza nchi ya Tanzania
Binafsi naona kama hawa watu wa Mungu wamechelewa,walikuwa wamkosoe raisi pale tu alipoanza kuwakashifu na kuwaadhiri raia anaowaongoza hadharani mbele ya halaki ya watu.
Hawa watu wa mungu walitakiwa waanze kumkaripia kumkosoa Raisi pale tu yeye na mtoto wake mkuu wa mkoa walipokuja na tabia wanayoita "Kutumbua majipu"..
Lakini sio mbaya afadhali hawa watu wa Mungu wenye imani ya kristo wameweza kusimama na kuwatetea wanyonge ambao hawana nguvu za kumwambia Raisi kuwa anachofanya sicho,ambacho haifai kumfanyia hata mtoto wako..
Sasa kuna hawa watu wa Mungu wenye imani ya Kiislam masheikh,hawa watu ndio wananishangaza mimi,Juzi nimesoma katika mtandao wa kijamii Sheikh mkuu wa Tanzania (Bakwata) anawamrisha waislam wasifanye mazoezi ya karate..
Kama mtu wa mungu unaiona nchi wapi inaelekea,unaona raisi kakata kamba,hakamatiki,wananchi wanalalamika kila kona wewe unakwenda kuwaambia watu wa imani yako wasifanye mazoezi ya karate..,Ajabu
Ningependa kumwambia Sheikh mkuu wa dini ya kiislam kuwa mazoezi ni njia moja ya kuondoa mkusanyiko wa mawazo(stress) katika akili ya binadamu,Jela zote ulaya lazima wafungwa wawekewe sehemu ya kufanya mazoezi,dakini 30 kwa siku..,sijui jela za Tanzania ziko je kwa hili,wanafanya hivyo ili kuondoa "stress" za wafungwa
Watanzania kwa sasa wanahitaji mazoezi ya nguvu ili kuondoa "stress",maisha yamekuwa maugu kila mtanzania ana mawazo yaliyomzidi uwezo...
Huyu Sheikh angeligombania mambo ya msingi wanayoyataka waislam mfano mahakama ya Kadhi ambayo imepigwa vita na wafuasi wa dini nyangine,Masheikh kutoka Zanzibar wamewekwa ndani zaidi ya miaka mitano(5) sasa bila kupewa huku yoyote...
Au angalau huyu Sheikh asimame pamoja na watu wa Mungu wenye imani tafauti na yeye ili kumkosoa raisi kwa haya anayowafanyia watanzania ambao ndio anaowaongoza
Nawapa hongera kwa watumishi wa Mungu wenye imani ya Kikiristo kwa kusimama kuitetea demokrasi na haki za msingi za watanzania wote bila ya kujali imani zao
Binafsi naona kama hawa watu wa Mungu wamechelewa,walikuwa wamkosoe raisi pale tu alipoanza kuwakashifu na kuwaadhiri raia anaowaongoza hadharani mbele ya halaki ya watu.
Hawa watu wa mungu walitakiwa waanze kumkaripia kumkosoa Raisi pale tu yeye na mtoto wake mkuu wa mkoa walipokuja na tabia wanayoita "Kutumbua majipu"..
Lakini sio mbaya afadhali hawa watu wa Mungu wenye imani ya kristo wameweza kusimama na kuwatetea wanyonge ambao hawana nguvu za kumwambia Raisi kuwa anachofanya sicho,ambacho haifai kumfanyia hata mtoto wako..
Sasa kuna hawa watu wa Mungu wenye imani ya Kiislam masheikh,hawa watu ndio wananishangaza mimi,Juzi nimesoma katika mtandao wa kijamii Sheikh mkuu wa Tanzania (Bakwata) anawamrisha waislam wasifanye mazoezi ya karate..
Kama mtu wa mungu unaiona nchi wapi inaelekea,unaona raisi kakata kamba,hakamatiki,wananchi wanalalamika kila kona wewe unakwenda kuwaambia watu wa imani yako wasifanye mazoezi ya karate..,Ajabu
Ningependa kumwambia Sheikh mkuu wa dini ya kiislam kuwa mazoezi ni njia moja ya kuondoa mkusanyiko wa mawazo(stress) katika akili ya binadamu,Jela zote ulaya lazima wafungwa wawekewe sehemu ya kufanya mazoezi,dakini 30 kwa siku..,sijui jela za Tanzania ziko je kwa hili,wanafanya hivyo ili kuondoa "stress" za wafungwa
Watanzania kwa sasa wanahitaji mazoezi ya nguvu ili kuondoa "stress",maisha yamekuwa maugu kila mtanzania ana mawazo yaliyomzidi uwezo...
Huyu Sheikh angeligombania mambo ya msingi wanayoyataka waislam mfano mahakama ya Kadhi ambayo imepigwa vita na wafuasi wa dini nyangine,Masheikh kutoka Zanzibar wamewekwa ndani zaidi ya miaka mitano(5) sasa bila kupewa huku yoyote...
Au angalau huyu Sheikh asimame pamoja na watu wa Mungu wenye imani tafauti na yeye ili kumkosoa raisi kwa haya anayowafanyia watanzania ambao ndio anaowaongoza
Nawapa hongera kwa watumishi wa Mungu wenye imani ya Kikiristo kwa kusimama kuitetea demokrasi na haki za msingi za watanzania wote bila ya kujali imani zao