Mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,502
Reaction score
911,254
Yakiwa mekundu umeumizwa mno!
Yakiwa manene kwisha khabari kabisa!
Yakiwa yamepasuka katikati miguno!
Yakiwa zambarau wahoji waficha nini!
Yakiwa ndani ya
"lip-bum" maswali kibao!
Hivi mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Shavu la mdomo wa chini sasa gumzo!
Eti mpingo tii yawaje awe nalo jekundu?
Ati hiyo ni dalili maini na figo zimeliwa!
Sijui huyo tabibu mahiri wamemtoa wapi?
Bado napekuwa vitabu kujua ukweli wake!
Hivi mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Kwa mustakabali huu, kunyanyapaana sera!
kwa mustakabali huu, chuki kuongezeka sana!
Kwa mustakabali huu, nani ni mzima basi?
Kwa mustakabali huu, maambukizi kudumishwa!
Kwa mustakabali huu, usalama sasa uko wapi?
Hivi mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Uso utasuguliwa kuficha majeraha.
Meno yatatakaswa kulinda fizi zote.
Ulimi utakwanguliwa kufukuza harufu.
Kigele cheupe kuchochewa na jiwe kali!
Mkorogo kufunika mengi bila zengwe!
Hivi mashavu ya mdomo yaashiria nini?
 
Yakiwa mekundu umeumizwa mno!
Yakiwa manene kwisha khabari kabisa!
Yakiwa yamepasuka katikati miguno!
Yakiwa zambarau wahoji waficha nini!
Yakiwa ndani ya
"lip-bum" maswali kibao!
Hivi mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Shavu la mdomo wa chini sasa gumzo!
Eti mpingo tii yawaje awe nalo jekundu?
Ati hiyo ni dalili maini na figo zimeliwa!
Sijui huyo tabibu mahiri wamemtoa wapi?
Bado napekuwa vitabu kujua ukweli wake!
Hivi mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Kwa mustakabali huu, kunyanyapaana sera!
kwa mustakabali huu, chuki kuongezeka sana!
Kwa mustakabali huu, nani ni mzima basi?
Kwa mustakabali huu, maambukizi kudumishwa!
Kwa mustakabali huu, usalama sasa uko wapi?
Hivi mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Uso utasuguliwa kuficha majeraha.
Meno yatatakaswa kulinda fizi zote.
Ulimi utakwanguliwa kufukuza harufu.
Kigele cheupe kuchochewa na jiwe kali!
Mkorogo kufunika mengi bila zengwe!
Hivi mashavu ya mdomo yaashiria nini?

Mmmh hii mada ina MIVURUGO!
 
mashavu mdomo wa chini....................... kwani mtu ana midomo mingapi............... chaka mbaya msaada plz
 
tungo tata sana ndo maana wachangiaji wanakula kona
 
Lingekuwa shavu ningejua ni la usoni,
umeyasemea "mashavu" una lako jambo,
kwa kuwa sii kila wingu hubeba maji ya mvua,
basi sii kila "mashavu" yana maelezo uliyoyapambanua.

kwa nia ya kueleweka naamini hata mimi umenielewa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom