Mashangingi ya CHADEMA!!

Mashangingi ya CHADEMA!!

kwa kweli mimi ni mwanachadema damu lakini kuna mahali hata nyie wachangiaji wenzangu tuwe tunaongea ukweli,KUHUSU KUTUMIA MAGARI YA KIFAHARI VIONGOZI CHADEMA HIYO TABIA WANAYO,kwa wale wanaofuatilia siasa za ndani kumbukeni siku ujumbe wa chadema ulioenda ikulu kuwasiliana na rais,haraka haraka niliona vx kali sio tu vx ili ina ubora wa kipekee wa wale viongozi,VX aliyokuwa kapanda mbowe sio ya kitoto hata mil 80 sidhani kama utaweza kuipata ,pili wabunge wengi wa chadema wana magari ya kifahari ingawa kuna wachache sana wanayakawaida,ANGALIA GARI YA REGIA MTEMA ALIYOPATANAYO AJALI,mtoto ana miezi kadhaa bungeni anatembelea vx tena viti maalum ,wakati baba yake hapo tabata tunamjua,KWELI KWA HILI VIONGOZI WA CHADEMA BADILIKIE TUMIENI RAV 4 NI GARI NZURI ,NGUMU,INAENDA BARABARA ZOTE MIL 20 TU INATOSHA BADALA LA HAYO YA MIL 80

Chungu lakini ndo dawa.....mimi napata ugumu kulewa kwamba hayo yao ya binafsi tusijadili n so tuamini kwamba wakiwa madarakani wanaweza kusimamia yale ya jukwaani

Kizunguzungu cha siasa ni hatari kuliko kichefuchefu cha malaria
 
Kigarama...
Naomba nitumie maneno haya kukufumbua macho. Unapoishi jirani kuna mtu ana VX na mwingine ana Suzuki Nomade. Mwenye VX akilala na njaa akaenda kumwomba mwenye Suzuki chakula kesho yake, nadhani mwenye Suzuki atamwambia mwenye VX kuuza gari lake la gharama kubwa na fedha atakayopata atanunua Suzuki (ili aweze kusafiri) na inayobaki atanunua chakula na nyingine atafanya mtaji wa biashara...hakika hata patwa na njaa tena.
Sasa Kigarama...
CCM ikiambiwa masuala ya msingi kama afya na elimu inasema hakuna fedha nchi yetu bado maskini. hakika lazima tuende nje kuhemea ili tuweze kupata chochote cha kula. kama haya ni ya kweli, basi tumia mfano wangu wa awali wa hao watu wawili yaani mwenye VX na mwenye Suzuki.
kwa hiyo Kigarama...
CDM ina maisha yake, ili kusaidia Taifa hili Tajiri linaloitwa maskini na magamba ilikuja na mpango mzima wa kuwakwamua watanzania...waunge mkono!
 
Kinachogombewa hapa si mtu bali ni mfumo...
Angalia Rwanda...
Angalia wakati wa Nyerere...
Angalia na wakati wa Mwinyi, viongozi walipotoka Zanzibar...
Kwa hiyo ....ni.... MFUMO!!! ...........ndo tatizo letu kuu.............
 
Kigarama...
Naomba nitumie maneno haya kukufumbua macho. Unapoishi jirani kuna mtu ana VX na mwingine ana Suzuki Nomade. Mwenye VX akilala na njaa akaenda kumwomba mwenye Suzuki chakula kesho yake, nadhani mwenye Suzuki atamwambia mwenye VX kuuza gari lake la gharama kubwa na fedha atakayopata atanunua Suzuki (ili aweze kusafiri) na inayobaki atanunua chakula na nyingine atafanya mtaji wa biashara...hakika hata patwa na njaa tena.
Sasa Kigarama...
CCM ikiambiwa masuala ya msingi kama afya na elimu inasema hakuna fedha nchi yetu bado maskini. hakika lazima tuende nje kuhemea ili tuweze kupata chochote cha kula. kama haya ni ya kweli, basi tumia mfano wangu wa awali wa hao watu wawili yaani mwenye VX na mwenye Suzuki.
kwa hiyo Kigarama...
CDM ina maisha yake, ili kusaidia Taifa hili Tajiri linaloitwa maskini na magamba ilikuja na mpango mzima wa kuwakwamua watanzania...waunge mkono!

Mkuu kama Chadema ina maisha yake na ina jitosheleza kwa nini inaendelea kupokea ruzuku inayo toka serikalini na ambayo ni kodi ya wananchi? Jamani watu hamjui swala la ruzuku?
 
CHADEMA ilitoa hoja za msingi sana wakati wa Kampeni za Mwaka 2010 na zikakubalika na wananchi wa Tanzania.

Mgombea Urais wakati huo MH: Willbroad Peter Slaa na wagombea wa nafasi za Udiwani na Ubunge walikuwa wanatoa tuhuma kwamba serikali iliyopo madarakani inafuja fedha za wananchi kwa kununua magari ya kifahari aina ya Land Cruiser VX na V8 wakati fedha hizo zingetumika vizuri zingeleta maendeleo kwa wananchi. Katika kukoleza hoja hiyo ikaaminishwa kwamba kama CHADEMA ikishika madaraka basi magari hayo ya kifahari yatauzwa na madala yake yatanunuliwa magari madogo ya bei rahisi.

Slaa alikuwa anasema aina ya magari yanayotumiwa na Wakuu wa Wilaya na Mikoa thamani yake ni sawa sawa na gari moja kujenga Zahanati Nne vijijini. Wanachi waliambiwa kwamba magari hayo yatauzwa na fedha itakayopatikana itatumika kuwekeza kwenye Elimu.

Baada ya uchaguzi wa Mwaka 2010 viongozi wa CHADEMA hawatumii VX au V8 kwa matumizi ya kichama na yao binafsi, au thamani ya magari hayo imeshuka baada ya wao kuanza kuyatumia?

UKIKEREKA SEMA UPENDAVYO!!

Naomba kuuliza hapo kwenye red, hivi vyama vya siasa vinatumia magari ya serikali ?
 
Ni kwa mujibu wa sheria......suala la usahihi ni subjective mno

Kwamantiki hiyo waeza kubaliana nami kuwa kama sheria inasema hivyo basi haiko sawa ni matumizi mabaya ya kodi za watz hivyo tunahitaji sheria hii ibadilishwe au sivyo?
 
Nazungumzia "consistency" ya chama kwenye mambo wanayoyapigania wakati wa Kampeni. Kusema akili yangu mbovu hakuondoi ukweli kwamba hata hayo mashangingi ya CHADEMA yananunuliwa na kwa kodi za wananchi. Wewe hujui kuna baadhi ya wabunge kabla ya kuwa wabunge hata Baiskeli walikuwa hawana uwezo wa kununua.

Unajisahaulisha kwamba wabunge wote walipewa mkopo wa shilingi Milioni 90 na ofisi ya Bunge kwa ajili ya kununulia magari yao?

Haya Mashangingi ya CHADEMA yamenunuliwa kwa fedha za serikali au mikopo wanayopewa wabunge?

Au ulifikiri kwa akili yako nyingi kuwa CDM walimaanisha hata ya Bakhresa na Manji nayo yauzwe?
 
CDM walichokuwa wanalalamikia ni suala la Serikali kuwa na magari ya kifahari ambayo ni ya bei kubwa na yana high fuel consumption.. Na vle vle yana gharama kubwa kwenye kuyamaintain.. Hiyvo unakuwa ni mzigo mkubwa na wa gharama kwa serikali..! Sasa mtoa uzi unaposema CDM wanayatumia magari ya aina hiyo unapaswa kutuweka wazi.. yanalipiwa na Serikali..? Kama ni mkopo ni haki yao wabunge wote kama ilivyoainishwa katika privileges za wabunge.. Na ukumbuke hata katika taasisi na mashirika mengine yana utaratibu wa kutoa mikopo ya magari kwa wafanyakazi wao ili kuwaharasishia kwenye usafiri wafanyakazi ili kuleta ufanisi.. Na mbunge ana choice ya gari gani anunue.. Mh. Mnyika yeye aliamua kununua Toyota Vitz na pick up.. Kama mwingine alinunua vx ni haki yake.. Kiwango kinachotolewa na serikali cha mafuta kwa magari ya wabunge ni kile kile uwe na Vitz au vx.. Services ya magari yao wanalipa wenyewe wabunge..

Ndo haya tunayosema inawezekana kubana matumizi mkuu.....sasa kwa case yako hii anapewa mafuta ya kutumia kwa rate ipi ya cunsumption VX, VITZ au PICK UP??? Na je ingekuwa ni kampuni yako binafsi na unataka kutoa hiyo allowance ungelipa kwa kigezo kipi??? Kati ya hayo magari ainishwa???

Jamani with all due respect haya mambo yana effect kwenye maisha yetu.......hivi kwa huyu mbunge mmoja uliyemtolea mfano hapa....Why do you think kafikia hayo maamuzi at a personal level??

Hata kama ni mikopo na watalipa.....attitude na behaviour ya binadamu si rahisi kuibadili eti tu kwa sababu leo nipo huku na kesho nipo kule.........waswahili tunasema mazoea hujenga tabia...wakiyazoea hayo madubwasha ndo nitoleeeeee
 
Nadhani hoja inajibiwa kwa hoja mimi siamini kama maneno yaliotumika hapo juu kwenye mjadala wa hoja kama kiazi,akili mbovu,mjinga,mvivu wa kufikiri,mfuasi wa kibwetere yana nafasi,cha msingi tujifunze kuvumiliana na kujibu hoja za msingi kwa hoja na wala si jaziba maana tunaamini watu wenye access ya JF walio wengi ni wasomi na wenye uelewa wa mambo.
You may agree to disagree but kwa hoja ili kwa mtu ambaye si mwanasiasa au muumini wa chama chochote apate mwelekeo

Umeongea mkuu...yaani ni kashfa na kejeli wakati kuna hoja ya kujadilika hapa............kiongozi wa umma kwa manufaa ya umma....private sphere inapungua sana na sometimes yaweza futika kabisa

Kioo huwa hakitoi image yake bali ya kilicho mbele yake......so matumizi personal yaweza kuwa indicator ya kubashiri collective expenditure as well.........though not limited to

My take;Wasiwasi huwa hauondolewi kwa lugha mbaya na kashfa bali hutoweka kirahisi sana kwa kumhakikishia huyo mwenye wasiwasi usalama wake. Mtoa hoja ana wasiwasi na aondolewe mashaka yake kwa hoja
 
kwamantiki hiyo waeza kubaliana nami kuwa kama sheria inasema hivyo basi haiko sawa ni matumizi mabaya ya kodi za watz hivyo tunahitaji sheria hii ibadilishwe au sivyo?

ziko sheria nyingi mbaya na kandamizi amabazo lazima zitolewe na katiba mpya!
 
Mtoa mada haelewi kwamba magari ya sirikali ni mapya na gharama zake ni kama zaidi milion 200 tofauti na hayo cdm
 
Kigarama...
Naomba nitumie maneno haya kukufumbua macho. Unapoishi jirani kuna mtu ana VX na mwingine ana Suzuki Nomade. Mwenye VX akilala na njaa akaenda kumwomba mwenye Suzuki chakula kesho yake, nadhani mwenye Suzuki atamwambia mwenye VX kuuza gari lake la gharama kubwa na fedha atakayopata atanunua Suzuki (ili aweze kusafiri) na inayobaki atanunua chakula na nyingine atafanya mtaji wa biashara...hakika hata patwa na njaa tena.
Sasa Kigarama...
CCM ikiambiwa masuala ya msingi kama afya na elimu inasema hakuna fedha nchi yetu bado maskini. hakika lazima tuende nje kuhemea ili tuweze kupata chochote cha kula. kama haya ni ya kweli, basi tumia mfano wangu wa awali wa hao watu wawili yaani mwenye VX na mwenye Suzuki.
kwa hiyo Kigarama...
CDM ina maisha yake, ili kusaidia Taifa hili Tajiri linaloitwa maskini na magamba ilikuja na mpango mzima wa kuwakwamua watanzania...waunge mkono!

Na wewe endelea hapa ili twende sawa; Basi baadaye mwenye suzuki biashara yake ikawa nzuri na maisha yakamnyookea watoto wake wakawa vijana na wakapata mikopo kwa kutumia influence ya baba yao na kuanza kuishi maisha ya ghali kama jirani yao aliyeuza VX lakini kila mzee wao alipoaswa juu ya vijana wake yeye alijibu ni mikopo yao wenyewe waache wafanye watakavyo bila kukumbuka ya kuwa mikopo ile ali influnce yeye mkuu wa kaya na huko nyuma aliwahi kumshauri jirani yake auze VX.....

My take;Kama mzee angekuwa na busara angewaonya vijana hawa kwa kuwapa mifano ya jirani aliyeuza VX badala ya kusema ni mikopo yao wenyewe.......
 
Akili yako mbovu,chadema iliadress yale yanayonunuliwa kwa kodi za watz.kuelewa kugumu sana ndgu yangu...kiazi

naamini wewe hukumwelewa vizuri anachozungumzia soma kwa makini thread ndipo ujibu siyo kukurupuka kama unatoka usingizini bana, ccm hapana chadema sawa kwa nini?
 
Na wewe endelea hapa ili twende sawa; Basi baadaye mwenye suzuki biashara yake ikawa nzuri na maisha yakamnyookea watoto wake wakawa vijana na wakapata mikopo kwa kutumia influence ya baba yao na kuanza kuishi maisha ya ghali kama jirani yao aliyeuza VX lakini kila mzee wao alipoaswa juu ya vijana wake yeye alijibu ni mikopo yao wenyewe waache wafanye watakavyo bila kukumbuka ya kuwa mikopo ile ali influnce yeye mkuu wa kaya na huko nyuma aliwahi kumshauri jirani yake auze VX.....

My take;Kama mzee angekuwa na busara angewaonya vijana hawa kwa kuwapa mifano ya jirani aliyeuza VX badala ya kusema ni mikopo yao wenyewe.......

Very low mentality this is.........
 
Kinachogombewa hapa si mtu bali ni mfumo...
Angalia Rwanda...
Angalia wakati wa Nyerere...
Angalia na wakati wa Mwinyi, viongozi walipotoka Zanzibar...
Kwa hiyo ....ni.... MFUMO!!! ...........ndo tatizo letu kuu.............

Hii inaitwa REIFICATION; Mfumo haunyeshi kama mvua mkuu hutengenezwa na kuhuishwa na watu ambao ndo hawa tunaowaongelea hapa in their singular and plural terms......regarding expenditures respectively.....you never expect a good system while the terms, conditions and responsible persons are somewhat contra to the basic tenets of the so expected system

Recast the example above in your quote; During the JK Nyerere times huo mfumo ulijengewa misingi na watu walioamini na kutumikia content ya mfumo husika ndo mana iliwezekana so ni watu waliweka mfumo na kuusimamia mkuu sio mfumo ulisimamia watu on its own
 
Hebu tuache ushabiki katika kila jambo. Mimi binafsi naona mtoa hoja anayo hoja. Kama ni kweli kwamba Chadema wamenunua mashangingi ama kwa matumizi ya chama ama kwa matumizi binafsi basi wamekosea, hawajamaanisha waliyoyatamka kwa vitendo, si mfano mzuri katika hili. Chadema wanapaswa kuonesha mfano kwa maneno na vitendo, hiyo ndio namna pekee ya kujitofautisha na CCM na kufundisha kwa vitendo. Natoa wito kwa viongozi wa Chadema kuliangalia hili jambo kwa umakini maana ni mambo madogomadogo ya namna hii ndio yanaondoa taratibu imani yao kwa chama. Nawasilisha.
 
Hebu tuache ushabiki katika kila jambo. Mimi binafsi naona mtoa hoja anayo hoja. Kama ni kweli kwamba Chadema wamenunua mashangingi ama kwa matumizi ya chama ama kwa matumizi binafsi basi wamekosea, hawajamaanisha waliyoyatamka kwa vitendo, si mfano mzuri katika hili. Chadema wanapaswa kuonesha mfano kwa maneno na vitendo, hiyo ndio namna pekee ya kujitofautisha na CCM na kufundisha kwa vitendo. Natoa wito kwa viongozi wa Chadema kuliangalia hili jambo kwa umakini maana ni mambo madogomadogo ya namna hii ndio yanaondoa taratibu imani yao kwa chama. Nawasilisha.

Tatizo sio aina ya gari bali ni vipi tuna prioritize matumizi ya fedha za umma......mtu binafsi akipenda kununua VX V8 rukhsa kabisa......CHADEMA walipigia kelele serikali kununua magari ya kifahari wakati nchi inamatatizo mengine ya muhimu......... na si kuwa kununua gari ya kifahari kwa level ya mtu binafsi ni tatizo........ni sawa uko msibani hamjanunua hata sanduku na michango ni finyu mtu anataka ipikwe biriani.......sasa kama kuna mfiwa na uwezo wa kupika biriani nyumbani kwake asifanye hivyo kwa kuwa alisema isipikwe msibani?
 
Very low mentality this is.........

Personal attack has never been an alternative to an expected response.......the task is still ahead of you MR VERY HIGH MENTALITY, and that regards the issue on the discrepancy that has been highlighted which exists between the preached and the lived, I accept the low degree of mental activity endowed in me as per your wishes BUT then how do you disentangle the enmashed duo existance of such personalities in a country like this?????
 
If you can't beat them ......... Si unakumbuka ile hadithi ya 'Shamba la Wanyama,' (Animal's farm) ya George Orwell?
 
Back
Top Bottom