Masasi signs ni mradi wa nani?

Masasi signs ni mradi wa nani?

Kiranja Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2010
Posts
4,464
Reaction score
5,176
Kampuni hii ambayo inatajwa kuwa inamilikiwa na mwanamama, kwa nini ipewe nafasi ya ukiritimba kwenye sekta ya kutengeneza nambari ya magari?

Kipindi hiki cha soko huria, kwanini wawekezeji wasikubaliwe kushindana na masasi sign ili mwananchi anufaike na ushindani wa kibiashara na pia awe na uwanja mpana wa kumchagua mtengeneza kibao amtakaye?

Je, Masasi Signs ni mradi wa kibopa gani?
 
haha haha ha Mzee wa Wivu wa kike kajiwekea kamradi ka kumlisha na kumneenesha miaka yote.
Zisi kantre bwana, ukipata chance ya kujilimbikizia, wafikirie na wenzako ambao kamwe hawatoweza kuyafikia mafanikio yako.
 
Ni kweli Masasi ni mradi wa mwana mama mmoja ambaye mara nyingi anapatikana Arusha.
Ila kusema kweli kazi anaifanya ipasavyo.

Lbda kama mtu aw'disqualify kwa vigezo vingine eg. jinsi alivyopata tenda, muda wa kuendesha tenda n.k
Lakini kwa kufanya kazi waliyopewa, jamaa wanajitahidi.
 
Hata mimi nawakubali ni wazuri na sasa hivi unapata plate baada ya siku tatu. swali la kujiuliza ni Je, Tenda hii ni ya Kudumu?
 
Hawa si walishinda tenda?

Amandla....

Kuna kampuni ya wahindi sikumbuki jina lake ilikwenda mahakama kuu kupinga Masasi signs kupewa zabuni ya kutengeneza namba za magari lakini walishindwa.
Pia MS hawana mkataba wa kudumu kutengeneza number plates
 
tatizo tunapoingia kwenye soko huria, maana yake serikali inatakiwa kusimamia viwango vya bidhaa/huduma kwa wateja na sio kusimamia ukiritimba kama huo wa masasi. Tunge kuwa na ajira karibu kila mkoa hata wilayani.
 
Kwa sasa kuna kampuni nyingine imepewa kazi ya kutengeneza plate, lakini cha ajabu ni kuwa Standard zake si sawa na zile za masasi. Namba zake ni pana zaidi.

Swali la kujiuliza, hata kama mtu mwingine akipewa fursa za kutengeneza namba. Je, kila mmoja atakuwa na standard (patent) zake?

Maana hizi namba za hawa jamaa wa SI ni tofauti kimuonekano na za masasi, standard ya plates ni ipi?
 
Hata mimi nawakubali ni wazuri na sasa hivi unapata plate baada ya siku tatu. swali la kujiuliza ni Je, Tenda hii ni ya Kudumu?

Mimi niliomba nililipa saa nane dkt 45 , nikapata kibao baada ya saa kama moja baadaye hivi.

Masasi vibao vyao ni vizuri na real professional.

Kuna kampuni nyingine ipo nayo yatengeneza vibao, lakini sivipendi, maandishi yake makubwa yameacha nafasi , kama mtoto anajifunza kuandika darasa la kwanza.

Masasi- safi......
 
Huyo masasi amemonopolize soko na anafanya vizuri kazi zake. TANESCO amaemonopolize soko kazi ovyooo. Na bado wote hao tunaona kuna tatizo. wakati mwingine wateja wa hao wadau tunakuwa ni tatizo. vibaya hatupendi na vizuri hatupendi.
 
THE former GV wa benki kuu,the late B,played a crucial role in the masasi,s acquisation of this tender,his younger brother N,used to go out with sara masasi
 
Kwani tenda inatoka baada ya muda gani? Tayari kuna hiyo nyingine manavyosema, sasa shida iko wapi? Cha msingi sisi wateja tuwe na uchaguzi wa kati ya Masasi na hao wengine!! Halafu serikali itoe standards ambazo zitafuatwa na wote! Labda hizo kubwa zinaumuhimu wake katika ku-note namba kutokea mbali!!!!
 
Mimi niliomba nililipa saa nane dkt 45 , nikapata kibao baada ya saa kama moja baadaye hivi.

Masasi vibao vyao ni vizuri na real professional.

Kuna kampuni nyingine ipo nayo yatengeneza vibao, lakini sivipendi, maandishi yake makubwa yameacha nafasi , kama mtoto anajifunza kuandika darasa la kwanza.

Masasi- safi......


Masasi Signs Saaaafi, saafi saana
But why long term exclusivity in that business?
 
Huyu ni yule aliekuwa bibi wa aliekuwa mh wazirimkuu wa tanzania
bw f sumaye amempa tenda nyingi tu ila nahisi wameachia kuna wengine hivi sasa
huyu mama alikuwa anachangia mamilio ccm hasa uchaguzi mill 500/700


sasa wewe asipewe tenda atawalipa ni ni siku ya uchaguzi big up maama l
 
Mama kama ujatoka mpaka sasa inabidi usubiri mbingu zikutoe hakika umefanya mengi
kuna mwingine alikuwa anapewa tenda za kuleta mabendera fulana na tkt nyingine za ccm kwenye uchaguz huyu mganga wake mkali hata tripu hii anakamata tenda mama mmoja wa kihaya yuko masaki..gemu yake kubwa naomba yasitukute yaliomkuta prof
 
Nadhani kuna hoja ya msingi hapa.

Hata kama wanafanya kazi yao vizuri nadhani kuna ukiritimba na usiri usiokuwa wa lazima (kama kweli hakuna vested interests).

Kwa nini kusiwepo ushindani, je gharama halisi za hizo namba plates ndizo hizo analipa mteja? Hakuna 10 ya watu hapa? Ni soko huria pekee ndilo litatuambia kuwa tunalipa gharama halali.

Mimi ningependekeza kuwepo na utaratibu kama ule wa kwenye clearing ambapo TRA wamesajili makampuni yanayoweza kufanya hiyo service, na kwenye namba plates kuwepo pia na uhuru wa mteja kuamua anatengenezewa namba plate wapi na si kuamuliwa na TRA.
 
Back
Top Bottom