Ndg wana JF,
Huyu mama ajulikanaye kwa jina la Mary Chitanda (Kiswahili Kitanda) naona anazidi kuwa katika wakati mgumu kutokana na matamshi yake ya utata. Ikumbukwe kuwa mama huyu ndiye hasa chanzo cha mgogoro wa nafasi ya Umeya Ausha mjini.
Wiki iliyopita aliwabwatukia maaskofu kwa kile alichokiita kuwa maaskofu wavue majoho ili wapambane kwenye siasa. Hii ilikuwa baada ya maskofu kukemea mauaji ya Arusha yaliyofanywa na polisi wakati wa maandamano ya amani ya chadema; vilevile maaskofu walidai kuwa hawamtambui meya huyo ambaye alichaguliwa kinyume na taratibu.
Lakini kuonesha kuwa hata viongozi wa juu wa ccm hawako pamoja na mama huyo, jumapili iliyopita Waziri Steven Wasira ambaye alikuwa anamwakilisha Rais katika sherehe za kumsimika Askofu mkuu wa jimbo kuu la Mwanza aliwataka Maaskofu na viongozi wa dini kuikemea serikali pindi wanapoona inafanya maovu.
Vile vile juzi wakati waziri huyo alipokuwa anahojiwa na kituo cha TV cha TBC1 aliendelea kusisitiza kuwa kwa kukemea maovu ya serikali sio siasa hivyo alishikilia msimamo wake kuwa viongozi wa dini waendelee kuikosoa serikali pale wanapoona inakwenda kinyume na maadili.
Swali langu:
Huyu Mary Kitanda ni nani hasa hata apinge kauli ya Rais (iliyotolewa kwa niaba yake na Waziri Wasira). Anapata wapi kiburi cha kubwabwaja na kutishia amani ya nchi. Kikwete unamuona au humuoni huyu mama.
Quote:
Ukicheka na nyani shambani utayavuna mabua.
Huyu mama ajulikanaye kwa jina la Mary Chitanda (Kiswahili Kitanda) naona anazidi kuwa katika wakati mgumu kutokana na matamshi yake ya utata. Ikumbukwe kuwa mama huyu ndiye hasa chanzo cha mgogoro wa nafasi ya Umeya Ausha mjini.
Wiki iliyopita aliwabwatukia maaskofu kwa kile alichokiita kuwa maaskofu wavue majoho ili wapambane kwenye siasa. Hii ilikuwa baada ya maskofu kukemea mauaji ya Arusha yaliyofanywa na polisi wakati wa maandamano ya amani ya chadema; vilevile maaskofu walidai kuwa hawamtambui meya huyo ambaye alichaguliwa kinyume na taratibu.
Lakini kuonesha kuwa hata viongozi wa juu wa ccm hawako pamoja na mama huyo, jumapili iliyopita Waziri Steven Wasira ambaye alikuwa anamwakilisha Rais katika sherehe za kumsimika Askofu mkuu wa jimbo kuu la Mwanza aliwataka Maaskofu na viongozi wa dini kuikemea serikali pindi wanapoona inafanya maovu.
Vile vile juzi wakati waziri huyo alipokuwa anahojiwa na kituo cha TV cha TBC1 aliendelea kusisitiza kuwa kwa kukemea maovu ya serikali sio siasa hivyo alishikilia msimamo wake kuwa viongozi wa dini waendelee kuikosoa serikali pale wanapoona inakwenda kinyume na maadili.
Swali langu:
Huyu Mary Kitanda ni nani hasa hata apinge kauli ya Rais (iliyotolewa kwa niaba yake na Waziri Wasira). Anapata wapi kiburi cha kubwabwaja na kutishia amani ya nchi. Kikwete unamuona au humuoni huyu mama.
Quote:
Ukicheka na nyani shambani utayavuna mabua.