#COVID19 Marekani yaruhusu watu waliopewa chanjo za Sinopharm na Sinovac

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
1636508829905.png

Marekani imetangaza kuwa kuanzia tarehe 8 Novemba watu waliopata chanjo kwa ukamilifu kutoka nchi zote duniani wataruhusiwa kuingia nchini Marekani kwa ajili ya utalii. Uamuzi huu umetangazwa kwa njia ya Twitter na naibu msemaji wa Ikulu ya Marekani Bw. Kevin Munoz. Uamuzi huu unafuatia marufuku iliyowekwa tangu mwanzoni mwa mwaka 2020, wakati Marekani ilipoweka zuio kwa watu wa nchi zote ikiwemo wa Uingereza, Umoja wa Ulaya na China.

Kufunguliwa kwa utalii kwa Marekani kunatoa ujumbe wa aina mbili, kwanza ni kuwa hali ya janga la COVID-19 nchini Marekani inazidi kuboreka baada ya mpango kabambe wa chanjo. Hii ina maana sekta ya utalii nchini Marekani hasa kuelekea katika kipindi cha sikukuu za Krismas na mwaka mpya itakuwa na uhai. Lakini pia sekta ya usafiri hasa wa ndege ambayo imekuwa na hasara kubwa kutokana na zuio la janga la COVID-19, inapata matumaini kwa kuweza kusafirisha abiria kwenda na kurudi nchini Marekani.

Kinachofurahisha zaidi, na pengine kuleta maswali kiasi ni kuhusu maelekezo ya chanjo zilizotajwa, kuwa watu walipewa chanjo hizo kikamilifu ndio watakaoweza kuingia Marekani. Kituo cha kupambana na kudhibiti maradhi cha Marekani - CDC kimesema ni watu waliopata kwa ukamilifu chanjo zilizoidhinishwa na Idara ya usimamizi wa chakula na dawa ya Marekan FDA, na Shirika la Afya duniani WHO, ndio watakaoruhusiwa kuingia Marekani. Chanjo hizo ni Moderna, Johnson & Johnson, Pfizer-BioNTech, Oxford-AstraZeneca/Covishield, Sinopharm na Sinovac.

Orodha hii ya chanjo kimsingi inatokana na uamuzi uliofanywa na wataalam kwa sababu za kisayansi na kutokana na ushahidi. Hali hii pia inaweza kuondoa wasiwasi walionao baadhi ya watu katika nchi nyingine duniani, waliokuwa wanasita kupewa baadhi ya chanjo kwa hofu kuwa chanjo hizo ni hafifu kwa kuwa hazikubaliwi na baadhi ya nchi za magharibi, au watakataliwa kuingia katika nchi fulani kutokana na kutopewa chanjo za nchi za magharibi. Taarifa hiyo ya naibu msemaji wa ikulu ya Marekani inaweza kutoa mchango hasi katika kazi ya utoaji wa chanjo duniani.

Si muda mrefu tulikuwa tusikia mara nyingi kauli kuhusu ubaguzi wa chanjo na utaifa wa chanjo. Ingawa malalamiko hayo hayawezi kufutika kabisa, ukweli ni uamuzi huu wa Marekani ni mwanzo mzuri kwenye mwelekeo sahihi. Kama wanasayansi wamethibitisha kuwa chanjo fulani ni salama na ina ufanisi, ukweli huo hautabadilika hata kama wanasiasa watasema vipi. Na pia uamuzi huo unathibitisha kuwa siku zote wanasayansi na wataalamu wa afya wataendelea kufanya maamuzi kwa mujibu wa matokeo ya kisayansi, na sio kwa matakwa ya baadhi ya wanasiasa wenye nia ovu.

Kwa sasa baadhi ya watu waliokuwa wanasita kupokea chanjo ya China kutokana na habari hasi na za upotoshaji kutoka kwa baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, sasa watakuwa na moyo wa kupokea chanjo hiyo. Wakati bado idadi kuwa ya watu wanahofu ya kupata chanjo, kauli kama hii kutoka ikulu ya Marekani inawaondoa watu hofu iliyoletwa na wapotoshaji.
 
Back
Top Bottom