Marekani yaitumia Islamic State Kuivamia Philippines

Marekani yaitumia Islamic State Kuivamia Philippines

Rais wa Philippines Duertete amesema serikali ya Marekani kupitia magaidi wa Islamic State wamevamia jimbo la mindanao na kuuteka mji Mkuu wake Marawi. Vita katika mji huo mkuu umechukua wiki 3 na mpaka sasa majeshi ya Philippines yameshindwa kuwaondoa wapiganaji ISIS. Raia na wanajeshi wengi wamepoteza maisha yao.
Toka Rais Duertete aingie madarakani ameonyesha chuki kubwa kwa nchi za magharibi mpaka ilifikia hatua kumwita aliyekuwa Rais wa Marekani Barrack Obama mwanaharamu, uhusiano wa nchi hiyo na marekani umezorota sana kiasi ambacho Rais Duertete aliamuru majeshi ya Marekani kuondoka nchini humo. Hawa magaidi wa ISIS wanapigana huko Syria na Iraq kwa msaada wa serikali ya Marekani kupitia shirika lake la ujasusi CIA
Imebidi kwa Rais Duertete kuipigia magoti Marekani ili imsaidie vita hivyo. Kwa miaka mingi nchi ya Philippines ilikuwa na vita na kikundi cha kigaidi Abusayaf lakini haikuwa kutokea vita vikubwa kama zilizotokea wiki 3 zilizopita.
 
Durtete Alimwita obama... Anamfananisha na mwana wa kahaba... Kwanini Trump hatumi hiki kikundi N.Korea...

Kim atazaa na mke wa trump walai....
 
Inawezekana hata hawa wa kibiti kuna mkono wa marekani, maana sio kwa kutuendesha huku.
 
Wewe acha ubishi usio na mizizi. Ninaifahamu hiyo nchi kuliko unavyoweza kuwaza. Siku zote umaskini huwa hauishi na ujinga unadumu kama ukiambatana na uwongoo.

Yanayosemwa nje siyo yaliyomo ndani. Kushindwa kwake kaitka ulinzi , uovu wake katika mahusiano sasa anataka kuwasingizia America? Hata kama hayo mashenzi ISIL yameongezeka lakini hana sababu ya kuiingiz aAmerica katika hili bila sababu. Ni hasidi tu.

Wewe hujasikia watu wakisema waarabu wanahcinjana kwa sababu Wazungu walitegeneza silaha?

Wewe hujasikia waislam wenyewe wakisema wanauana kwa kuwa ujinga ujinga tu?

CCM inaua taifa kwa ufisadi rushwa, ubinafsi, juinga na uongozi mbovu lakini kinachosemwa siyo kushindwa kwao bali watasingizia "wapinzani ndio wanasababisha tuwe na katiba mbovu, tushindwe kutoa huduma bora za afya, tukose mipango bora ya maana na upumbaveu mwingi tu? Unataka kusema nini? Kama wewe huijui hiyo nchi nyamaza basi!
 
Durtete Alimwita obama... Anamfananisha na mwana wa kahaba... Kwanini Trump hatumi hiki kikundi N.Korea...

Kim atazaa na mke wa trump walai....
Thubutuuuu.... Huyo Kim amshukuru ChinA vinginevyo ni mweupe sanaaaaa
 
Huyu si ndo yule jeuri, acha anyoooshweee cheza na Amerikano weye
 
Siku US itakapoanguka ndiyo siku amani ya duniani itapatikana
Amani haitopatikana duniani, ni hivyo mpaka yesu atakaporudi. Haitatokea...

Ebu angalia historia ya mataifa superpower yaliyowahi tawala dunia...

Kuanzia roma, uingereza, ujerumani na sasa marekani....

Kulikuwa hakuna amani, na kuna makundi ya raia yaliishi kwa shida kutoka na tawala hizo....
 
Ila hii habari tumelishwa matango pori, kwa mujibu wa Dairy Mirror la uk, usa wameenda Marawi kumsaidia Durtete kupambana na isis
US juzi waliwapa silaha hasa bunduki Philippines kupambana na IS , US Ana mbinu Sana Ni mbinu za kinafiki kwa hiyo sio rahisi kujua yuko upande gani ?
 
Meli ya kivita ya marekani imegongana na meli ya mizigo ya Philippines kwenye pwani ya Japan mabaharia 7 wa kimarekani wanasemekana wamefariki dunia.
 
Bahati mbaya sana Dunia inapambaa na kitu wasichokijua, kwani stage ya kwanza kupambana na kitu chochote kwanza ni kukijua kuanzia mienendo yake na wao ni kina nani kutofautisha na wengine, cha kushangaza mpaka leo DUNIANI hakuna tafasiri moja inayoelezea Gaidi ni nani zipo zaidi ya tafasiri 15 ambazo zinaelezea gaidi ni nani lakini wataalamu wa maswala ya matukio ya mashambulizi ya kustukiza na yenye kuleta hofu wameshindwa kukubaliana maana sahihi ya UGAIDI na GAIDI ni nani na wanaposhindana ni vigezo vipi vinatumika kumuita mtu gaidi? au ni vigezo gani vinatumika kumtoa mtu kuitwa gaidi? mfano wapigania Uhuru wote (freedom fighter) walikuwa wanaitwa magaidi mfano Mandela lakini kwa waafrica tulikuwa tunamwona kama mpigania uhuru na haki za waafrica weusi nchini South Africa lakini makaburu na wazungu walikuwa wanamuona ni Gaidi na aliwekwa mpaka kwenye list ya Magaidi Duniani amekuja kufutwa kwenye list tena mmoja wa viongozi wakuu Duniani Margaret Thatcher aliwai kumuita Mandela na ANC kuwa ni “typical terrorist" haya kuna nchi duniani zinavamia nchi zingine na kufanya mauaji ya kinyama mfano Israel wanavyofanya kwa watoto wa kiparestna je hule ni nini?

Leo kundi la (ISIS) inasemekana wanapata ufadhiri kutoka US sasa unajiuliza hawa magaidi na hawa wapinga ugaidi wana mpango gani tena? nadhani ni wakati sahihi ktk kupambana na ugaidi na magaidi duniani siku wapambana na ugaidi wakiwa serious kupambana na ugaidi tutapata tafasiri moja ya ugaidi ni nini na gaidi ni nani na wote tutajua tunapambana na nani na nina uhakika ugaidi utakuwa history kama ilivyokuwa ucominist
Usiseme dunia haijui, sema hujui
 
Usiseme dunia haijui, sema hujui
OK niambie Gaidi ni nani na Ugaidi ni nini na ni vigezo vipi vinatumika kumjua huyu ni Gaidi na vigezo vp vinatumika kumtoa mtu kwenye list ya kuitwa Gaidi kama ilivyofanywa kwa Mandela na wapigania uhuru wengine? pia niambie vitendo vya Ugaidi vinafanywa na watu tu au hata nchi inaweza kufanya vitendo vya ugaidi mfano Israel; wanavyofanya kwa watoto wa Palestine je vile si vitendo vya Ugaidi ? sasa kwa nini Israel haijawekwa au kuitwa ni nchi ya KIgaidi???
 
OK niambie Gaidi ni nani na Ugaidi ni nini na ni vigezo vipi vinatumika kumjua huyu ni Gaidi na vigezo vp vinatumika kumtoa mtu kwenye list ya kuitwa Gaidi kama ilivyofanywa kwa Mandela na wapigania uhuru wengine? pia niambie vitendo vya Ugaidi vinafanywa na watu tu au hata nchi inaweza kufanya vitendo vya ugaidi mfano Israel; wanavyofanya kwa watoto wa Palestine je vile si vitendo vya Ugaidi ? sasa kwa nini Israel haijawekwa au kuitwa ni nchi ya KIgaidi???
Ugaidi ni kulipua watoto?
 
OK niambie Gaidi ni nani na Ugaidi ni nini na ni vigezo vipi vinatumika kumjua huyu ni Gaidi na vigezo vp vinatumika kumtoa mtu kwenye list ya kuitwa Gaidi kama ilivyofanywa kwa Mandela na wapigania uhuru wengine? pia niambie vitendo vya Ugaidi vinafanywa na watu tu au hata nchi inaweza kufanya vitendo vya ugaidi mfano Israel; wanavyofanya kwa watoto wa Palestine je vile si vitendo vya Ugaidi ? sasa kwa nini Israel haijawekwa au kuitwa ni nchi ya KIgaidi???
Kuna tofauti 2 za ugaidi Good Terrorism and Bad Terrorism nchi ya Marekani, Israeli, Saud Arabia etc ni good terrorism na bad terrorism ni Iran, North Korea, Hamas, Hizzbollah etc ni baada terrorism.
 
Kuna tofauti 2 za ugaidi Good Terrorism and Bad Terrorism nchi ya Marekani, Israeli, Saud Arabia etc ni good terrorism na bad terrorism ni Iran, North Korea, Hamas, Hizzbollah etc ni baada terrorism.
Duh inamaana kuna jambazi mzuri na jambazi mbaya?????? sikuwahi kudhani kuwa kuna UGAIDI mzuri na UGAIDI mbaya
 
Duh inamaana kuna jambazi mzuri na jambazi mbaya?????? sikuwahi kudhani kuwa kuna UGAIDI mzuri na UGAIDI mbaya
Good terrorism ni ambaye analinda maslahi ya Marekani. Na bad terrorism anayepinga maslahi ya marekani
 
Ukiambiwa ni marekani wako nyuma ya hii kitu unaweza usibishe maana jamaa kafukuza US Army kutoka Philipines, ISIS tunaaminishwa wana bif na marekani hawana sababu ya kuvamia nchi ambayo imewafukuza wamarekani.
ISIS ni mmarekani
 
Back
Top Bottom