Marekani: Mbunge Mwanamke Kutoka Republican Afariki

Marekani: Mbunge Mwanamke Kutoka Republican Afariki

Dalton Elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
925
Reaction score
1,954
Mia Love, mbunge wa kwanza mwanamke mweusi wa chama cha Republican nchini Marekani amefariki akiwa na umri wa miaka 49 huko Utah, imetangaza familia yake.

Taarifa hiyo imesema, aliaga dunia kwa amani siku ya Jumapili, akiwa amezungukwa na familia nyumbani kwake huko Saratoga Springs.

Love, mtoto wa wahamiaji kutoka Haiti, alikuwa mbunge wa jimbo la Utah katika Bunge la Marekani.
Binti yake Abigale alisema mapema mwezi huu kwamba Love alikuwa akipatiwa matibabu ya saratani ya ubongo.
Maisha ya kisiasa ya Mia Love yalianza rasmi mwaka 2003 aliposhinda kiti katika baraza la jiji la Saratoga Springs, na baadaye akawa meya akiwa na umri wa miaka 34.

Mwaka 2014, alichaguliwa kuwa mbunge katika Bunge la Marekani na kuweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza mweusi wa chama cha Republican kuchukua nafasi hiyo, na alihudumu kwa mihula miwili.
 
Mia Love, mbunge wa kwanza mwanamke mweusi wa chama cha Republican nchini Marekani amefariki akiwa na umri wa miaka 49 huko Utah, imetangaza familia yake.

Taarifa hiyo imesema, aliaga dunia kwa amani siku ya Jumapili, akiwa amezungukwa na familia nyumbani kwake huko Saratoga Springs.

Love, mtoto wa wahamiaji kutoka Haiti, alikuwa mbunge wa jimbo la Utah katika Bunge la Marekani.
Binti yake Abigale alisema mapema mwezi huu kwamba Love alikuwa akipatiwa matibabu ya saratani ya ubongo.
Maisha ya kisiasa ya Mia Love yalianza rasmi mwaka 2003 aliposhinda kiti katika baraza la jiji la Saratoga Springs, na baadaye akawa meya akiwa na umri wa miaka 34.

Mwaka 2014, alichaguliwa kuwa mbunge katika Bunge la Marekani na kuweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza mweusi wa chama cha Republican kuchukua nafasi hiyo, na alihudumu kwa mihula miwili.
Miaka yote republican hawakuona umuhimu wa mtu mweusi hasa mwanamke, hadi inaonekana ni jambo la kushangaza kuwa na Mbunge mweusi. Wabaguzi.
 
Back
Top Bottom