Marekani hakuna Rais daktari, CPT, Engineer wala Advocate? Kwanini hawapendi kusoma?

Sio shida. Kwanza Makanyaga Kakosea kidogo John Adams hana udugu na Andrew Jackson.

John Adam rais wa 2 ni Baba wa John Quincy Adams rais wa 6.


William Harrison rais wa 9 ni Babu wa Benjamin Harrison rais wa 23.

Theodore Roosevelt rais wa 26 ana udugu na FDR (Franklin Delano Roosevelt) rais wa 32. Hata First Lady wa FDR, Eleanor Roosevelt ni mpwa wa Theodore Roosevelt. Hivyo walioana ndugu.

JFK, Rais wa 35, mdogo wake RFK (Alikuwa AG wakati wa uongozi wa kaka yake na baadae Senetor) ilikuwa agombee mwaka 1968 ila aliuawa na Sirhan Sirhan. Ted Kennedy ( alikuwa Senator kwa muda mrefu) mdogo wao mwingine akataka kugombea mwaka 1980. Mwanae Ted anayeitwa Patrick Joseph Kennedy aliwahi kuwa US Rep. Nadhani mnamjua Robert F. Kennedy Jr. mtoto wa RFK aliyeuawa 1968 alitaka kugombea mwaka huu.

George H. W. Bush rais wa 41 ni Baba wa George W. Bush rais wa 43. Mdogo wake George W. Bush, Jeb Bush (alikuwa Governor), alitaka kugombea mwaka 2016.
Sijakosea. Unachokisema vwewe ndiyo KILE AMBACHO nimeandika

 
Hata Tanzania hakuna Rais aliewahi kuwa na PHD, wote ni za kupewa kwa heshima halafu machawa wanambadilisha na kumuiya Dr. Hata JPM alipata ya kubumba pale UD, kila kitu alifanyiwa. Wanasiasa wengi TZ wanatafuta PHD za kubumba ili apate cheo, mfano Mwigulu awezi kufanya presentation ya uchumu kwenye jopo la wasomi
 
Na viongozi wa Afrika ndio wanaongoza kwa kuzitaka , wakikutana Umoja wa Mataifa pale US-New York , kila Rais wa Afrika akisimama utaskia Hon Doctor ABC, alafu anaenda kukopa kwa mtu ambaye hana hiyo doctor, professa etc.

Mimi usiponiita Engineer D
Sikuitikii na Sifanyi unalotaka nifanye…
Over…Allaaaa
Kwani Ukiniita Engineer utapungukiwa na Nini???
Wivu tuuu??
Hebu ita Engineer D
Naaam!
Sema?
Tena Ngoja Tukazie watuongezee Seminar za ERB zaidi!
Tukaliongelee hili…
Tena Ita Professional Engineer D.
Yaani P.Eng. D
 
Reason ni kwamba upumbavu,ujinga na ushamba bado ni mwingi afrika kuzidi sehemu zingine za dunia,na professionalism mtu huipata ili atambulike na si aitumie kuleta positive impact kwenye jamii ndo maana hupenda ajulikane yeye ni dr, wakili, injinia n. K for show off. Mambo haya ni kinyume kabisa kwa watu wa sehemu zingine nje ya afrika.
 
Marekani ambayo kabla kupata uhuru mwaka 1776 , ilitawaliwana Uingereza na wakapata Rais wa kwanza George Washington.
Tangu wapate uhuru, haijawahi kutokea Rais yeyote , awe msomi wa chuo, daktari wa hospitali[MD] au wa falsafa phD,au mjuzi wa hesabu [CPA] ambaye amewahi kujinasibu na prefix ya cheo chake.

Je, ni ulimbukeni kutumia phD, CPA, Advocate kwenye majina ya marais? Je, haya majina wanayojipa kwenye vyeo vyao yana-reflect maendeleo kwenye nchi zao?

OBAMA [Profesa wa Sheria]

LIST YA MARAIS WOTE WA MAREKANI.

  1. George Washington (1789-1797)
  2. John Adams (1797-1801)
  3. Thomas Jefferson (1801-1809)
  4. James Madison (1809-1817)
  5. James Monroe (1817-1825)
  6. John Quincy Adams (1825-1829)
  7. Andrew Jackson (1829-1837)
  8. Martin Van Buren (1837-1841)
  9. William Henry Harrison (1841)
  10. John Tyler (1841-1845)
  11. James K. Polk (1845-1849)
  12. Zachary Taylor (1849-1850)
  13. Millard Fillmore (1850-1853)
  14. Franklin Pierce (1853-1857)
  15. James Buchanan (1857-1861)
  16. Abraham Lincoln (1861-1865)
  17. Andrew Johnson (1865-1869)
  18. Ulysses S. Grant (1869-1877)
  19. Rutherford B. Hayes (1877-1881)
  20. James A. Garfield (1881)
  21. Chester A. Arthur (1881-1885)
  22. Grover Cleveland (1885-1889)
  23. Benjamin Harrison (1889-1893)
  24. Grover Cleveland (1893-1897)
  25. William McKinley (1897-1901)
  26. Theodore Roosevelt (1901-1909)
  27. William Howard Taft (1909-1913)
  28. Woodrow Wilson (1913-1921)
  29. Warren G. Harding (1921-1923)
  30. Calvin Coolidge (1923-1929)
  31. Herbert Hoover (1929-1933)
  32. Franklin D. Roosevelt (1933-1945)
  33. Harry S. Truman (1945-1953)
  34. Dwight D. Eisenhower (1953-1961)
  35. John F. Kennedy (1961-1963)
  36. Lyndon B. Johnson (1963-1969)
  37. Richard Nixon (1969-1974)
  38. Gerald Ford (1974-1977)
  39. Jimmy Carter (1977-1981)
  40. Ronald Reagan (1981-1989)
  41. George H. W. Bush (1989-1993)
  42. Bill Clinton (1993-2001)
  43. George W. Bush (2001-2009)
  44. Barack Obama (2009-2017)
  45. Donald Trump (2017-2021)
  46. Joe Biden (2021-present)
MADAKTARI WALIKUWA HAWA.
1. James Madison
2. William Henry Harrison
3. Andrew Johnson:

MAWAKILI/WANASHERIA

1. Barack Obama: Obama alipata digrii yake ya sheria kutoka Shule ya Sheria ya Harvard na alifanya mazoezi ya sheria huko Illinois kabla ya kuingia katika siasa. Aliwahi kuwa Rais wa 44 wa Merika kutoka 2009 hadi 2017.

2.Bill Clinton: Clinton alipata digrii yake ya sheria kutoka Shule ya Sheria ya Yale na alifanya mazoezi ya sheria huko Arkansas kabla ya kuingia katika siasa. Aliwahi kuwa Rais wa 42 wa Merika kutoka 1993 hadi 2001.

3.
Gerald Ford: alipata digrii yake ya sheria Yale Law School and practiced law in Michigan kabla ya kuingia kwenye siasa . Alikuwa raisi wa 38 US tangu 1974 to 1977.

4. Richard Nixon: alipata digrii yake ya sheria Duke University Law School and practiced law in California kabla ya kuingia kwenye siasa. He served as the 37th President of the United States from 1969 to 1974.

5. Franklin D. Roosevelt: Roosevelt alihudhuria Shule ya Sheria ya Columbia lakini hakumaliza shahada yake ya sheria. Alifanya sheria kwa muda mfupi kabla ya kuingia kwenye siasa. Aliwahi kuwa Rais wa 32 wa Merika kutoka 1933 hadi 1945.

6 Thomas Jefferson: Jefferson pia alikuwa mwanasheria kitaaluma. Alilazwa katika baa ya Virginia mnamo 1767 na akafanya sheria kwa miaka kadhaa kabla ya kuingia kwenye siasa. Jefferson aliwahi kuwa Rais wa tatu wa Merika kutoka 1801 hadi 1809.

7. James Madison: Madison alipata elimu yake ya kisheria kutoka Chuo cha William na Mary na alifanya sheria huko Virginia. Alikuwa mmoja wa waandishi wa msingi wa Katiba ya Merika na aliwahi kuwa Rais wa nne wa Amerika kutoka 1809 hadi 1817.

8. James Monroe: Monroe alisoma sheria chini ya Thomas Jefferson na kufanya sheria huko Virginia. Aliwahi kuwa Rais wa tano wa Merika kutoka 1817 hadi 1825.

9. John Quincy Adams: Adams alikuwa mwanasheria aliyeelimishwa na Harvard ambaye alitekeleza sheria kabla ya kuingia kwenye siasa. Aliwahi kuwa Rais wa sita wa Merika kutoka 1825 hadi 1829.

10. Andrew Jackson: Jackson alianza kusomea sheria katika ujana wake na alilazwa katika baa ya North Carolina mwaka wa 1787. Alifanya mazoezi ya sheria huko Tennessee na aliwahi kuwa Rais wa saba wa Marekani kuanzia 1829 hadi 1837.

11. Abraham Lincoln: Lincoln ni mmoja wa wakili-marais maarufu katika historia ya U.S. Alifanya mazoezi ya sheria huko Illinois na aliwahi kuwa Rais wa 16 wa Merika kutoka 1861 hadi 1865.

12. Franklin Pierce: Pierce alihudhuria shule ya sheria katika Chuo cha Bowdoin na alifanya mazoezi ya sheria huko New Hampshire. Aliwahi kuwa Rais wa 14 wa Merika kutoka 1853 hadi 1857.

13. Benjamin Harrison: Harrison alisomea sheria katika Chuo Kikuu cha Miami na kufanya mazoezi ya sheria huko Indiana. Aliwahi kuwa Rais wa 23 wa Merika kutoka 1889 hadi 1893.

14.Rutherford B. Hayes: Alisoma Harvard Law School na kufanya kazi Ohio. Alikuwa raisi wa 19 wa Marekani toka 1877 mpaka 1881.

15. William Howard Taft: Alisoma chuo cha Yale akifanya kazi huko Ohio. Alikuwa raisi wa 27 tangu 1909 to 1913 na baadae akawa jaji mkuu wa Marekani .

16. Calvin Coolidge: Alisoma Law na kuwa wakili huko Massachusetts. Alifanya kazi za uwakili kabla ya kuingia kwenye siasa na kuwa raisi wa 30 tangu 1923 to 1929.

17. Woodrow Wilson: Wilson alisoma shule ya sheria kwa vitendo Chuo kikuu Virginia na kufanya kazi ya uwakili,alikuwa raisi wa 28 wa marekani toka 1913 mpaka 1921.

18. Chester A. Arthur: Arthur practiced law in New York City before entering politics. He served as the 21st President of the United States from 1881 to 1885.

19.Grover Cleveland: Cleveland studied law and was admitted to the bar in 1859. He practiced law in New York and served as the 22nd and 24th President of the United States from 1885 to 1889 and again from 1893 to 1897.

20. Chester A. Arthur: Alikuwa wakili New York City kabla hajaingia siasani. Akawa raisi wa 21wa Marekani toka 1881 mpaka 1885.

Hao wote, madaktari, CPA, MAprofessor na Mawakili hawatumii tittle zao, kwanini Afrika ?

Kwanini Maraisi wa kisasa , hasa Afrika wanapenda recognition ya udaktari ?
Marekani hawajimbulishi kwa academic titles isipokuwa za wanajeshi na za waganga tu. Mtu hawezi kuamka akajitambulisha kuwa mimi ni Injinia Kichuguu, au mimi ni Profesa Kichuguu, au mimi CPA Kichuguu, au Mimi ni Wakili Msomi Kichuguu. Title hujionyesha zenyewe wanapoandika majina yao: Kwa mfano Kichuguu, PE; Kichuguu, PhD; au Kichuguu, JD, Esq; Kichuguu CPA. Waganga ndio wanaoitwa Dr Kichuguu kwa sababu ya kazi zao siyo kwa sababu ya academic credentials. Vile vile wanajeshi watambulika vivyo Col Kichuguu, Let Gen Kichuguu na kadhalika kwa sababu ya hierarchy za kijeshi. Wakiingia kwenye siasa wanaacha kutumia titles hizo

Katika wanasiasa wote wa marekani ninajua katika miaka ya hivi karibuni, ni Dr Henmry Kissinger tu ndiye aliyejulikana kwa title ya Dr. Kabla ya kuingia kwenye siasa alikuwa Profesa wa Harvard University. Lakini wengine wote hawatumii academic titles. Watu wenye academic credentials za nguvu waliowahi kufanya kazi za kisiasa siku za nhivi karibuni ni pamoja Condoleeza Rice, Steven Chu ( huyu ana Nobel Prize) , David Petreaus (pamoja na kuwa general ana PhD ya nguvu) hawakutumia credintial za nje ya vyeo vyao vya kisiasa kama secretary Rice, secretary Chu na Director Peteraus
 
Alafu mbona naona karibu marais wote wa marekani ni wanasheria mbona sisi uku ni walimu au tunakosea kuchagua viongozi wetu wawe walimu?
Sasa maskini a.k.a mnyonge anaambiwa achague mafiga matatu, ndio tunaletewa takataka.
 
Wananchi ndio mumewaendekeza viongozi wa nchi zenu, mtu mpaka anajiita profesa wa jalalani.
Kuna mwingine atajiita prof wa mafinyofinyo ya kule ofisini. Mama Angela Merkel PhD in Nuclear Chemistry na Wala hutosikia dokta sijui Nini lakini hapa kwetu Babu Tale kamnunilia mama ntilie sufuria mbili tayari akajiita Dr. Taletale kisa ame solve tatizo la ukosefu wa sufuria Kwa mama ntilie Hawa jamaa wanatia hasira unaweza m'bomoa mtu njia ya haha Nene na biological mallet basi tu.
 
Hahaaaa kama yule shetani aliyegonga punda alipopona hosp. Akamshukuru magufuli Kwa kupona Ile ajali
magufulimania, bado ipo kwa watu, hata AFANDE SELE anaamini Magufuli ndio raisi na anamlilia japo kishalambishwa asali na ka NGO cha kuchota fedha wizarani.
 
Kuna mwingine atajiita prof wa mafinyofinyo ya kule ofisini. Mama Angela Merkel PhD in Nuclear Chemistry na Wala hutosikia dokta sijui Nini lakini hapa kwetu Babu Tale kamnunilia mama ntilie sufuria mbili tayari akajiita Dr. Taletale kisa ame solve tatizo la ukosefu wa sufuria Kwa mama ntilie Hawa jamaa wanatia hasira unaweza m'bomoa mtu njia ya haha Nene na biological mallet basi tu.
umenikumbusha, Angel Makel anakutana na mtoto kutoka Tanzania hajui hata kusoma anajiita dokta, kapewa udaktari chuo cha kata.
 
Back
Top Bottom