Caroline Danzi
JF-Expert Member
- Dec 19, 2008
- 3,713
- 1,263
Wana JF ... hili limekaa vipi?.. Mie nimetoka Mkoani nimekuja Jijini(DAR).. kwa Mapumziko kidogo, kusalimia ndugu na marafiki zangu....
sasa jamani ugumu nimeukuta ktk ishu moja... Rafiki zangu wa Ukweli,,nimesoma nao kabisa,,,tumeishi pamoja chuoni... tumekula bata(kujirusha) pamoja wakati nipo nao chuo...!!! Maajabu nimewatafuta niwaone wamekua watu wa ma promise yasiyokua na fulfilment... Sasa mie nikajiuliza hawa vijana wanaoishi dar... wanatuchukulia vipi sie tunaotoka Mkoa... wanadhani ua tunakuja lia NJAA..kwao auuu??? Acheni ujinga bana, tunakuja na hela zetu za mavuuno ...!!!
Sisi tumefunzwa ukarimu, nakupa majina ya wafuatao ukifika dar uje tukupe raha za duniani, LAT, KakaKiiza, The Finest, Mwenzetu, Jrated, LD, Husninyo, Newmzalendo, Babalao, Manundu, Carmel etc.
Hao madenti wenzako ni masharobaro, wanahisi unanuka vumbi la mkoa si unajua tena! lol