You've spoken my mindHuyu ni kiongozi mkubwa katika nchi na amepitia katika kipindi cha presha
Kwa nini hakutulia??? au kulikuwa na ulazima wa yeye kusema kitu? what if kama Magufuli alikuwa anataka ampe nafasi ingine ya serikalini?
Nyuma ya pazia kuna nini ambacho Nape anahisi kachukiwa sana wakati kitu alichofanya is obvious ilikuwa lazima ajiuzulu yeye , bila hata kuondolewa. Hakukuwa na haja ya Kamati wakati mwisho wa matokeo ya kamati ni kupeleka report kwa Rais ambaye aliishaamua na kusema pale ubungo
Naamini rais sio malaika, wala sio kuwa Nape hana namba ya simu ya Magu kiasi ambacho wangeongea kuhusu hili swala na kupata baraka zake, kufanya jambo kama lile au kuendelea nalo likiwa linakinzana na bosi wako lina maana gani?? (tuache mihemko wengi tuna mabosi hapa)
Namna ya kudeal na lile swala ilikuwa lazima kuwe na kamati? au angebadili methodology? what was the mission behind? tuwaze nje ya box
Nape inaonekana alijua anafanya nini, na alijua outcome ya mission ilikuwa aidha
1. Rais awe kwenye wakati mgumu wa maamuzi
2. au Nape aondoke yeye
mkuu kamuwahi
ila siamini kama kwa level ya Nape hakujua kuwa kuna kitu kinaendelea..(?????) Yes unaweza kuwa hero, unaweza kuwa na malengo mema na mazuri kabisa ( kutimiza wajibu wako) ila kufanikisha kazi yako kwa ufanisi kunahitaji akili pia na approach kufikia lengo
mimi mtu wa chini niliona kabisa Nape anakinzana na rais, yeye hakuona? au yeye anafanya kazi kama msaidizi wa nani? kama sio msaidizi wa rais....naona Logic inagoma kuona kama Nape alikuwa yeye kama yeye na hana affiliation na Magufuli ambaye ni bosi wake
Imani yangu na msimamo wangu, Makonda ataondoka kupitia mahakama kwa sasa, kuvamia clouds was the best opportunity ya kumuweka kwenye majengo ya mahakama....ingemlazimisha rais kumuondoa
Kuna watu wanafikiri wanaweza kuendesha nchi wakiwa nje ya Ikulu. Nonsense
Rais ameonyesha kwamba anashinikizwa kufanya maamuzi kufuata matakwa ya watu na alitoa msimamo hadharani kukataa, hivi Nape hakumuelewa!??
Kauli ya JPM kwamba hapangiwi WA kuteua au kutengua ilibeba ujumbe mzito.Tunajua kuwa Marais wote baada ya Mwl.Nyerere walikumbwa na tatizo hili. Utakumbuka JK aliwahi sema Urais wangu hauna UBIA, Mkapa hivohivo, Mwinyi yeye ndio aliwahi kufungasha mizigo kabisaaa, akatoka Ikulu akarudi Zenj kupinga kuingiliwa na Mwl. Nyerere, inadaiwa wazee walimfuata kumnasihi
Nape naye anampush JPM, kamlazimisha ndani kashindwa sasa katokea nje kumchonganisha na RAIA, huyu in mtata haswa.
Mtakumbuka enzi za JK mwenyekiti CCM Nape alichomekea Falsafa ya kujivua gamba bila Ridhaa ya wenzie, hii ilikuwa operation kubwa ya kuwafukuza kina Lowasa CCM
