Marafiki wa kusafiri nao (Travelling Partners)

Marafiki wa kusafiri nao (Travelling Partners)

Sipendelei sana hii labda uwe na familia, mkeo vinginevyo mhhhhh naona chenga.
 
Ni wazo zuri sana. Kwa wenye hobby ya kusafiri tunakuelewa. Huwa napanga na jamaa zangu kusafiri by road around East Africa ila hatujafanikiwa hata mara moja. Najua sababu wengi wa kundi langu tumeshakua watu wazima sasa (above 35) so majukumu ya kifamilia na kazini yanatubana. Wengine wanatu-discourage kuwa hizo safari ni ufuska tu (mpango kazi wa Kigali ulihusishwa sana na totoz) hivyo watu wanakufa moyo/nafsi zinawasuta.
Ningependa sana kujoin group yako. Ila safari ya Egpyt nimeshaifanya. Sioni sababu ya kurudi tena hapo wakati kuna sehemu kibao za kwenda sijaenda. Nitajiunga nawe/nanyi siku ya kwenda elsewhere in Africa, Middle East na Asia (Ulaya na Amerika inabidi mfuko uwe mzuri sana). Kama ni mpenzi wa mpira pia, ikitokea Taifa Starz tunaenda Cameroon next year (nina imani kwelikweli mwakani Mungu ibariki Tanzania itapigwa AFCON) basi organise hii safari kijana wangu. Nitakua tayari 100%....yaani siku tunafuzu tu naanza kutenga fungu la safari.
 
Safi sana mkuu, nimerudi from Kenya on 26th September nlikaa 2 nights 3 days. Inaweza kuwa rahisi kupitia Tanga kama upo Dar maana Dar to Mombasa nadhani ni TZS 25,000-30,000 halafu Mombasa to Nairobi ukisafiri na first class bus ni 40,000. Pale Nairobi mimi nlilala Machakos nyumba nzuri tu and I paid TZS30,000 kwa siku kwa hiyo ilikuwa jumla 60,000 kwa night mbili. Kenya is visa-free to Tanzanian (s) kwa hiyo hutokuwa na gharama za visa. Milo ni kama bongo tu na I would suggest upae night 3 Nairobi na night 2 Mombasa.

Go for it aisee
Mkuu kwahio nikiwa nina passport tu naenda kenya bila shida yoyote?
 
Back
Top Bottom