Kuna baadhi ya silaha haziko effective haraka mfano mshale au mkuki.
Utendaji kazi wake hutegemea mtu kakupiga sehemu gani na mlikua umbali gani wakati anakupiga mshale, mara zote anayechomwa mshale hafi papo hapo (achana na movies) na kama atapata msaada wa matibabu hupona kabisa.
Note: sijasema msaada wa haraka kwa kua mshale unaweza kukaa nao mwilini hata siku mbili na usife, kuna kesi ya jamaa kuchomwa mishale zaidi ya mitano na akatembea mwenyewe kwenda kwenye matibabu. Na akapona.
Hapa Tanzania kuna jamaa alichomwa mkuki wa mdomo ukatokea shingoni na akapona.
Hata kama mshale/mkuki utakua ni wa sumu bado hauwezi kuua kwa haraka, nyoka mwenye sumu kali kabisa duniani, death adder, sumu yake huua baada ya saa 6. Na ukienda hospitali utapona.
Kiumbe chenye sumu kali kabisa, Stone fish, huua baada ya saa saba na hapa uhakika wa kufa upo kwa kua stone fish haijapatikana kinga yake bado, na anapatika Australia.
Huyo mmsasai au mmang'ati wa kwenda kuchukua sumu ya stone fish na kurudi nayo huku ili akuchome kweli atakua amedhamiria kukuua.