Shobi
JF-Expert Member
- May 31, 2015
- 3,401
- 4,371
Ni August 9, 2016 ambapo stori inayochukua headlines kwenye magazeti ya Tanzania ni kuhusiana na kukamatwa kwa mke wa marehemu wa bilionea Erasto Msuya.
Kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima limeripoti kwamba Miriam Msuya alikamatwa
juzi na Jeshi la Polisi nyumbani kwake Sakina Arusha kisha kusafirishwa hadi Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi kuhusu tuhuma za mauaji ya Aneth Msuya ambaye ni dada wa bilionea Erasto Msuya.
Gazeti la Tanzania Daima leo August 9 2016 limeripoti kuwa mke wa Msuya alikamatwa baada ya msichana wa kazi wa marehemu Aneth Msuya kumtaja kuhusika. Mfanyakazi huyo wa ndani ni mmoja kati wa watu wanaoshikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji
hayo.
Sasa millardayo.com & Ayo TV imempata kamanda wa polisi Arusha Liberatus Sabas na kayaongea haya;
"Nadhani kama mtakuwa mnakumbuka hilo tukio lilitokea jiji Dar es Salaam
kwahiyo hapa baada ya uchunguzi kufanyika jeshi la Polisi likamkamata mke wa marehemu Erasto Msuya ambae ni Miriam Msuya na kusafirishwa Dar es Salaam kwa ajili ya uchuguzi wa kina, alikamatwa Alhamisi iliyopita. "
========
Kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima limeripoti kwamba Miriam Msuya alikamatwa
juzi na Jeshi la Polisi nyumbani kwake Sakina Arusha kisha kusafirishwa hadi Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi kuhusu tuhuma za mauaji ya Aneth Msuya ambaye ni dada wa bilionea Erasto Msuya.
Gazeti la Tanzania Daima leo August 9 2016 limeripoti kuwa mke wa Msuya alikamatwa baada ya msichana wa kazi wa marehemu Aneth Msuya kumtaja kuhusika. Mfanyakazi huyo wa ndani ni mmoja kati wa watu wanaoshikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji
hayo.
Sasa millardayo.com & Ayo TV imempata kamanda wa polisi Arusha Liberatus Sabas na kayaongea haya;
"Nadhani kama mtakuwa mnakumbuka hilo tukio lilitokea jiji Dar es Salaam
kwahiyo hapa baada ya uchunguzi kufanyika jeshi la Polisi likamkamata mke wa marehemu Erasto Msuya ambae ni Miriam Msuya na kusafirishwa Dar es Salaam kwa ajili ya uchuguzi wa kina, alikamatwa Alhamisi iliyopita. "
========
