SIKU chache baada ya baba mzazi wa kachala wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Juma Diamond Platnum, mzee Abdul Juma kufunguka kuwa mwanaye huyo hamthamini toka amepata mafanikio, watu waliodai wao ni ndugu wa tumbo moja na mkali huyo wa muziki wa kizazi kipya wameibuka na kusema baba mzazi wa Diamond alishafariki dunia mwaka 2004, Ijumaa Wikienda lina ripoti kamili.
CHANZO CHATIRIRIKA
Baada ya habari ya kuibuka kwa baba wa Diamond kuchapishwa kwenye gazeti ndugu la hili (Amani) mwishoni mwa wiki iliyopita, chanzo makini kiliwatonya mapaparazi wetu kuwa baba aliyejitokeza (Abdul Juma) siyo wa damu.
Jamani nyie Amani mmeandika baba wa Diamond ni mzee Abdul Juma, mbona tunavyojua sisi, baba wa Diamond anaitwa Salum Idd na alishafariki dunia tangu mwaka 2004, kama mnataka ukweli zaidi fuatilieni, kilisema chanzo hicho huku kikiahidi kutoa ushirikiano.
MAPAPARAZI WAINGIA KAZINI
Mapaparazi wetu walianza kazi ya kufuatilia nyeti hiyo ambapo kwa msaada wa chanzo, Julai 12, mwaka huu walifanikiwa kutinga nyumbani kwa msichana aliyedai ni dada kwa baba mmoja na Diamond.
Msichana huyo anaishi Kariakoo, jijini Dar es Salaam na mdogo mwingine wa Diamond aitwaye Idd Salum ambaye naye anaimba kama kaka yake.
TUJIUNGE NA IDD ALIYEPO KARIAKOO
Baada ya salamu za hapa na pale na mapaparazi wetu kujitambulisha kwa familia hiyo, lilifuata swali kama kweli wao ni ndugu wa damu moja na Diamond.
Idd: Mbona kila kitu kipo wazi, hata yule mzee Abdul Juma anaelewa kila kitu kwamba sisi na Diamond ni ndugu, Diamond ni kaka yetu na amekuwa akinisaidia mimi katika shida na raha, baba yetu alishafariki dunia tangu mwaka 2004.
Yeye (Abdul) ni baba mlezi tu na anafahamu wazi kuwa yeye ni baba mlezi wa Diamond na kwamba baba yetu alishatutoka.
IDD AIBUA JIPYA
Kwa mujibu wa mdogo huyo wa Diamond, Idd, mwaka 1989, mama Diamond (Sanura Khassim Sandra) alipewa ujauzito na Salum (baba yake) kisha waligombana na kuachana.
Akasema baada ya kuachana, mama Diamond alikutana na Abdul ambaye alikubali kuwa naye kimapenzi na kuulea ujauzito huo wa mtoto (Diamond).
KWA HABRI KAMILI BOFYA HAPA GUMZO LA JIJI: MAPYA YAIBUKA KUHUSU BABA WA DIAMOND
CHANZO CHATIRIRIKA
Baada ya habari ya kuibuka kwa baba wa Diamond kuchapishwa kwenye gazeti ndugu la hili (Amani) mwishoni mwa wiki iliyopita, chanzo makini kiliwatonya mapaparazi wetu kuwa baba aliyejitokeza (Abdul Juma) siyo wa damu.
Jamani nyie Amani mmeandika baba wa Diamond ni mzee Abdul Juma, mbona tunavyojua sisi, baba wa Diamond anaitwa Salum Idd na alishafariki dunia tangu mwaka 2004, kama mnataka ukweli zaidi fuatilieni, kilisema chanzo hicho huku kikiahidi kutoa ushirikiano.
MAPAPARAZI WAINGIA KAZINI
Mapaparazi wetu walianza kazi ya kufuatilia nyeti hiyo ambapo kwa msaada wa chanzo, Julai 12, mwaka huu walifanikiwa kutinga nyumbani kwa msichana aliyedai ni dada kwa baba mmoja na Diamond.
Msichana huyo anaishi Kariakoo, jijini Dar es Salaam na mdogo mwingine wa Diamond aitwaye Idd Salum ambaye naye anaimba kama kaka yake.
TUJIUNGE NA IDD ALIYEPO KARIAKOO
Baada ya salamu za hapa na pale na mapaparazi wetu kujitambulisha kwa familia hiyo, lilifuata swali kama kweli wao ni ndugu wa damu moja na Diamond.
Idd: Mbona kila kitu kipo wazi, hata yule mzee Abdul Juma anaelewa kila kitu kwamba sisi na Diamond ni ndugu, Diamond ni kaka yetu na amekuwa akinisaidia mimi katika shida na raha, baba yetu alishafariki dunia tangu mwaka 2004.
Yeye (Abdul) ni baba mlezi tu na anafahamu wazi kuwa yeye ni baba mlezi wa Diamond na kwamba baba yetu alishatutoka.
IDD AIBUA JIPYA
Kwa mujibu wa mdogo huyo wa Diamond, Idd, mwaka 1989, mama Diamond (Sanura Khassim Sandra) alipewa ujauzito na Salum (baba yake) kisha waligombana na kuachana.
Akasema baada ya kuachana, mama Diamond alikutana na Abdul ambaye alikubali kuwa naye kimapenzi na kuulea ujauzito huo wa mtoto (Diamond).
KWA HABRI KAMILI BOFYA HAPA GUMZO LA JIJI: MAPYA YAIBUKA KUHUSU BABA WA DIAMOND