Mapungufu ya Kikwete: Constructive Criticisim!

hizi sentensi huwa zinasemwa sana na majuha wa CCM

Juzi mnyika kasema hivi hivi
leo ww unasema hivi hivi

kesho sijui nani atasema

You are dead wrong my dear pasco........all i can say no is think again and you have a room to correct that view!
Mkuu Waberoya, nilipikusoma unawaita watu majuha, kwanza nilishtuka, niliposoma tena nikajifariji kumbe hao majuha ni wa CCM!. Hata kama ni ukweli unawaona CCM majuha, huku sii kuwatukana?!. Si niliomba tuepuke matukano na lugha za staha?!.

Nikirudi kwenye mada, please lets be realistic, hivi ni kweli ni rais Kikwete ndiye anategemewa afanye kila kitu?!. Hao mawaziri wake na wasaidizi wake wanafanya kazi gani?!. Rais aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania, baada ya ahadi hiyo lilibaki jukumu la timu yake kupanga malengo na kujadili utekelezaji, sasa kama malengo yamepangwa na hayakufikiwa kosa ni la nani?.

Thank God nilikuwepo alipotembelea baadhi ya taasisi akapanga malengo na baada ya miaka mitano akapita tena, kule kule watu wale wale na nyimbo zile zile!. Ni nani hakutimiza wajibu wake?!.

Waberoya wewe uu miongoni mwa ma greti thinka wetu humu jukwaani, kama ni mtazamo huo ni ujuha, weka basi na mtazamo wako ambao sio wa kijuha kama mtazamo huu!.
 
Sasa nitoe constructive criticisms.

JK ni Rais anayependa sifa, hilo ni tatizo ambalo litagharimu sana legacy yake. Hotuba yake ya kwanza kwa Bunge lake akiwa kama Rais, aliahidi mambo mengi sana ambayo kama angeyatekeleza yangeweza kumpa umaarufu mkubwa sana, lakini ilipokuja kwenye utekelezaji ilikuwa ni zero. Mfano, aliahidi kurudisha nyumba zilizouzwa na serikali ya Mkapa, hakutimiza. Aliahidi kupitia upya mikataba mipya, hakuna kilichofanyika. Aliahidi kupambana na ufisadi, lakini akawa wa kwanza kuficha uvundo wa ufisadi wa Mkapa, Chenge na wengineo wengi ambao walikuwa wamegubikwa na tuhuma za ufisadi ambazo ushahidi wake ulikuwa wazi kabisa.

Mwaka 2005 hakuuzwa na Ilani ya Chama chake, bali aliuzwa na mtandao, vyombo vya habari na ule unafiki wake kwamba yeye ni mtu wa watu. Ndio maana kila kukicha utamuona yuko kwenye misiba. A day baada ya kuchaguliwa kuwa Rais alidamkia Muhimbili, watu wakasema sasa tumepata Rais atakayejali afya za walalahoi. Sasa kama Rais anajali afya za walalahoi na watendaji wakuu wa Wizara ya Afya wana tuhuma kibao, kwanini hizo tuhuma zisifuatiliwe? Halafu leo anasema hawezi kufanya mabadiliko kwa shinikizo la madaktari, sasa kama wameona kwamba viongozi wa wizara hawafai, wao wafanye nini?

Nani anafanya assessment ya utendaji kazi wa kiongozi? Ni Appointing Authority au yule anayeongozwa? Mjomba alishasema tutapima size ya kiatu after 5 yrs, so the Drs have all the rights za ku-judge utendaji kazi wa mawaziri wa wizara yao.

Nije swala la Katiba, pia JK kwa kupenda sifa na alipoona kwamba upinzani unapata umaarufu, alikurupuka na kuahidi katiba mpya. Bahati mbaya hakujua kwamba Katiba mpya inamuweka mahali pagumu zaidi maana wana CCM walikuwa hawataki mabadiliko. Matokeo yake mwanzo kwenye hotuba akawasema wapinzani na kudai kwamba atajaribu u-dictator na baadaye akaja kulamba matapishi yake kwa kuwaruhusu wapinzani wapeleke mapendekezo yao na alikubaliana nao. JK alifanya hivyo baada ya kuona wananchi wako against msimamo wa chama chake. Ndio maana nasema kwamba JK anapenda sana sifa na hiyo ni weakness mbaya sana.

Kitendo cha kupata 61% kwenye uchaguzi uliopita, lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa JK, hakutegemea ashuke kutoka 80% mpaka hapo, na hapo NEC (Tume ya Uchaguzi) ilikuwa imemsaidia sana kuchakachua na yeye anajua hilo. Kama wasingemsaidia, hata hizo 61 zisingefika. Ndipo akaunda Kamati ya Mukama kuchunguza kiini cha CCM kufanya vibaya kwenye huo uchaguzi. Ndipo ikaja Falsafa ya Vua Gamba, ambayo nayo imezidi kumuweka pabaya maana ameshindwa kuitekeleza kama wananchi walivyokuwa wakitegemea.

To conclude, ni kwamba kwa kuwa Rais wetu anapenda masifa, mara nyingi huwa ni mkurupukaji wa kuweka ahadi tamu na nzuri kusikika masikioni mwa wananchi bila kuzifanyia tathimini ya kina ili kuona kama ni ahadi ambazo zinatekelezeka au la. Matokeo yake sasa, Pinda ndo amekuwa mbebeshwa lawama halafu JK yuko kimya hasemi kitu kabisa na hasa akishapima upepo kwamba wananchi wako against. Ninamuonea huruma Pinda kwa kuwa wakati mwingine ni ngumu sana kufanya kazi na mtu ambaye anapenda credit iende kwake all the time na mabaya yote wabebeshwe wengine.
Keil, asante kwa hizi nondo na hii ndio ninayoita in good faith!. Thanks!.

Ila pia kuna baadhi ya ahadi, alitekeleza, mikataba alipitia upya na sheria ya madini ilirekebishwa japo Barrick waligomea na serikali ikanyea na kuwanyenyekea!.

Ufisadi aliridhia uchunguzi wa EPA ufanyike na kesi kibao kazipandisha mahakamani!. Mahalu. Mramba, Yona, Mgonja hadi Jeethu Patel wamesimamishwa kizimbani!? Mlitaka afanye nini zaidi?. Au asimame yeye aendeshe mashitaka baadae akalie kiti atoe hukumu na ikibidi awe bwana jela kuhakikisha wanatumikia vifungo!.

Yeye si ametimiza wajibu wake?. Sehemu ambayo sijamwelewa na sitamwelewa mpaka kesho kutwa ni ule msamaha wa mijizi ya EPA!.
 
Jamani msitafute mchawi, mkulu ndo tatizo. haiwezekani umepangwa kupiga penati halafu na ww unatoa pasi!!!. Sina haja ya kutaja mambo ambayo yy kama yy alikuwa anatakiwa kutoa kauli ya mwisho, anamwachia Pinda.
 
Yamezungumzwa mengi sana kuhusu JK ktk kumsifia na mapungufu yake lakini kama Pasco alivyosema binadamu hakosi kasoro na zitazo jitokeza lazima zipimwe ktk kiwango fulani kuweka upungufu huo. Na katika kupima mapungufu hayo inawezekana kuwa ni chupa ilijaa nusu au chupa ilipungua nusu ujazo..

Binafsi yangu nitasema kwamba matatizo ya Tanzania yetu ni zaidi ya JK.. tuna Culture conflict yaani tupo dunia ya kusadikika. WATU na MAZINGIRA yenyewe ni mzigo mkubwa sana ambao JK hakuuweza. Labda niseme kwamba cheo cha Urais ni kikubwa sana ukilinganisha na uwezo wake na sio swala la mapungufu yake tena. JK ameichukua nchi ktk hali ambayo haina DIRA hilo kwanza, pili Ubepari haupo ktk misngi inayofanana na tamaduni zetu hata iwe free market. Na alipoingia madarakani alifikiria anaweza kuibadilisha nchi kwa kuweka maono yake - vision ambayo ilikuwa kuyabadilisha MAZINGIRA yetu kwa manufaa ya WATU - Maisha bora kwa kila Mtanzania.

Lakini toka Azimio la Zanzibar na Ubepari, tumezaa Utaifa mpya wa darwin kama poriu la Serengeti. Competition bila viwanda ama uzalishaji ukazaa inequality..nayo ika constitute diverse ktk makundi ya kijamii, conflict of interests, valueless attitude, and crime norms kuibuka kiasi kwamba wakaibuka untouchables, sheria ikawa haina nguvu tena. Kushindwa kwa JK hakukuanza alipoingia madarakani bali kumetokana na watu na mazingira aloyakuta ambayo kulikuwa na watu above the law!.

Ndio maana ahadi zake zote zilikuwa hadi hewa, kutokana na kwamba alipoingia Ikulu aliwakuta WATU (wananchi wenyewe) ambao hawataki kubadilika wao isipokuwa kuyabadilisha mazingira yao ili wapatiwe maisha bora. Na wale wachache waliokuwa naye ktk safari ndefu ya kupata madaraka haya pia walikuwa na fikra za kujenga mazingira yatakayoweza kubadilisha maisha yao bila dira ya kitaifa. Ubepari sio dira na hauwezi kuchukuliwa kirahisi kama free market economy bali huja madudu yake.

Hizi ndizo siasa zilizoasisiwa na Mwinyi, Mkapa na leo hii tunaye JK ambao wote kwa kiwango chao cha utawala ktk kiti cha Urais walikuwa wakilenga kubadilisha maisha yao na sio kutumia mazingira tulinayo yaweze kukuza uchumi wetu na hata kuboresha maisha ya wananchi. Mtanisamehe kusema kwamba hawa wote hawakuwa na sifa za urais bali waandaliaji wa harusi (Wedding planner) kwa kuwaahidi wananchi harusi kubwa lakini wasijue harusi hiyo itaweza kudumu kwa muda gani. Matokeo yake ndio tumezaa Ufisadi ambao wao wanasema sio tatizo, Ufisadi ukazaa ubinafsi ambao ukazaa Udini na matabaka yote haya yamejenga umaskini zaidi na zaidi. Ubepari kwa Tanzania ni sawa na kuomba mvua zinyeshe ili muanze kulima badala yake yakatokea mafuriko ambayo viongozi wote wameshindwa.

Ni rahisi sana kumlaumu JK, lakini yeye ni reflection yetu sisi, leo nenda maofisini utakuta asilimia 20 ya waajiriwa ni ndugu au marafiki waliopeana pande. Humjui mtu huwezi upata ajira, humjui mtu huwezi kutoa mzigo wako bandarini kwa bei nafuu, humjui mtu huwezi kupata mkopo benki acha mbali kumpatia nafasi ya shule mwanao, haya yote hayafanyi JK bali sisi wenyewe toka ngazi ya mawaziri hadi mchoma nyama mitaani. Tupo ktk Culture conlfict
 
JK ni Rais wa Watanzania wote Wehu, Majuha, Maprof, Vichaa, tusubiri Rais wa Wasomi nadhani ndiyo atakuja baada ya JK.
 
Ila pia kuna baadhi ya ahadi, alitekeleza, mikataba alipitia upya na sheria ya madini ilirekebishwa japo Barrick waligomea na serikali ikanyea na kuwanyenyekea!.

Hapo kuna utata mkubwa sana, angekuwa na nia njema asingekubai kusaini mkataba mpya wa Buzwagi kwa kutumia sheria ya zamani. Zitto alipofungiwa Bungeni na wananchi kuonekana wako upande wa Zitto, ndipo JK akaja na Tume ya Bomani na kumuweka Zitto, yote hiyo ilikuwa ni harakati za kujaribu kuwa-win waTanzania ambao walishangazwa na jinsi Bunge la CCM lilivyozima hoja ya Buzwagi na kumfungia Zitto. Kama isingekuwa hoja ya Zitto mpaka sasa hayo makampuni yangekuwa bado yanalipa mrahaba wa 3%. Halafu kuongezea tu, Barrick ndio wamiliki wa migodi mingi ya dhahabu na wana jeuri kwa kuwa wana-connections serikalini na ndio maana serikali ilinywea.

Ufisadi aliridhia uchunguzi wa EPA ufanyike na kesi kibao kazipandisha mahakamani!. Mahalu. Mramba, Yona, Mgonja hadi Jeethu Patel wamesimamishwa kizimbani!? Mlitaka afanye nini zaidi?. Au asimame yeye aendeshe mashitaka baadae akalie kiti atoe hukumu na ikibidi awe bwana jela kuhakikisha wanatumikia vifungo!.

Mkuu wangu, ofisi ya Rais haitakiwi kuridhia uchunguzi wa jinai yoyote, bali ni taasisi husika ndizo zinatakiwa kufanya uchunguzi as soon as wakishapata clue/dokezo la jinai. Kama Kikwete alikuwa na nia ya kuwashughulikia hao, kwanini akiwa kwenye kampeni za 2010 alisema Mramba ana kesi ndogo sana na atashinda? Rais akitoa kauli hiyo unafikiri DPP na waendesha mashitaka watapeleka credible evidence mahakamani? Je, Hakimu/Jaji anayesikiliza shauri hilo huoni kwamba anaweza kuwa biased? Ndio maana hata vyombo vya habari huwa vinazuwiwa kuandika news za kesi na hasa kama vyombo vya habari vinaonekana kuelekea kutoa msimamo wa aina fulani. Hao wote uliowaorodhesha mwisho wa siku watakuja kuachiwa na kwamba kesi zao zilipelekwa mahakamani ili kumpa sifa kwamba he is fighting corruption, lakini ukweli ni kwamba ni sanaa juu ya sanaa.

Yeye si ametimiza wajibu wake? Sehemu ambayo sijamwelewa na sitamwelewa mpaka kesho kutwa ni ule msamaha wa mijizi ya EPA!.

Angekuwa alitimiza wajibu iwapo angekuwa amezipa uhuru Taasisi za Polisi, PCCB na DPP wa kufanya kile wanachoona kwamba ni halali. Nina uhakika kwamba kesi nyingi zinazohusu vigogo zinakwenda mahakamani baada ya kupata go-ahead ya Ikulu. Mahakama nayo iliingia humo humo, ndio maana Marehemu Ditopile aliingizwa mahakamani kwa kutumia mlango unaotumiwa na majaji, na hakuna Jaji hata mmoja aliyelaani. Mashitaka yakabadilika kutoka kuua kwa kukusudia mpaka kuua kwa kutokusudia. Wewe ni Mwanasheria na unajua vizuri sana haya mambo. WikiLeak walishamtoa Hosea akilalamika kwamba JK ndio kikwazo cha vita ya ufisadi. Hiyo pekee inaweza kutuma msg kwamba hayo unayosema alijaribu ilikuwa ni usanii wa kutaka sifa.
 
Hapo kuna utata mkubwa sana, angekuwa na nia njema asingekubai kusaini mkataba mpya wa Buzwagi kwa kutumia sheria ya zamani. Zitto alipofungiwa Bungeni na wananchi kuonekana wako upande wa Zitto, ndipo JK akaja na Tume ya Bomani na kumuweka Zitto, yote hiyo ilikuwa ni harakati za kujaribu kuwa-win waTanzania ambao walishangazwa na jinsi Bunge la CCM lilivyozima hoja ya Buzwagi na kumfungia Zitto. Kama isingekuwa hoja ya Zitto mpaka sasa hayo makampuni yangekuwa bado yanalipa mrahaba wa 3%. Halafu kuongezea tu, Barrick ndio wamiliki wa migodi mingi ya dhahabu na wana jeuri kwa kuwa wana-connections serikalini na ndio maana serikali ilinywea.

Mkuu wangu, ofisi ya Rais haitakiwi kuridhia uchunguzi wa jinai yoyote, bali ni taasisi husika ndizo zinatakiwa kufanya uchunguzi as soon as wakishapata clue/dokezo la jinai. Kama Kikwete alikuwa na nia ya kuwashughulikia hao, kwanini akiwa kwenye kampeni za 2010 alisema Mramba ana kesi ndogo sana na atashinda? Rais akitoa kauli hiyo unafikiri DPP na waendesha mashitaka watapeleka credible evidence mahakamani? Je, Hakimu/Jaji anayesikiliza shauri hilo huoni kwamba anaweza kuwa biased? Ndio maana hata vyombo vya habari huwa vinazuwiwa kuandika news za kesi na hasa kama vyombo vya habari vinaonekana kuelekea kutoa msimamo wa aina fulani. Hao wote uliowaorodhesha mwisho wa siku watakuja kuachiwa na kwamba kesi zao zilipelekwa mahakamani ili kumpa sifa kwamba he is fighting corruption, lakini ukweli ni kwamba ni sanaa juu ya sanaa.

Angekuwa alitimiza wajibu iwapo angekuwa amezipa uhuru Taasisi za Polisi, PCCB na DPP wa kufanya kile wanachoona kwamba ni halali. Nina uhakika kwamba kesi nyingi zinazohusu vigogo zinakwenda mahakamani baada ya kupata go-ahead ya Ikulu. Mahakama nayo iliingia humo humo, ndio maana Marehemu Ditopile aliingizwa mahakamani kwa kutumia mlango unaotumiwa na majaji, na hakuna Jaji hata mmoja aliyelaani. Mashitaka yakabadilika kutoka kuua kwa kukusudia mpaka kuua kwa kutokusudia. Wewe ni Mwanasheria na unajua vizuri sana haya mambo. WikiLeak walishamtoa Hosea akilalamika kwamba JK ndio kikwazo cha vita ya ufisadi. Hiyo pekee inaweza kutuma msg kwamba hayo unayosema alijaribu ilikuwa ni usanii wa kutaka sifa.
Keil, asante, kusema ukweli sikukujua keil uko deep kihivi, I'm learning a lot, thanks!.
 
Yamezungumzwa mengi sana kuhusu JK ktk kumsifia na mapungufu yake lakini kama Pasco alivyosema binadamu hakosi kasoro na zitazo jitokeza lazima zipimwe ktk kiwango fulani kuweka upungufu huo. Na katika kupima mapungufu hayo inawezekana kuwa ni chupa ilijaa nusu au chupa ilipungua nusu ujazo..

Binafsi yangu nitasema kwamba matatizo ya Tanzania yetu ni zaidi ya JK.. tuna Culture conflict yaani tupo dunia ya kusadikika. WATU na MAZINGIRA yenyewe ni mzigo mkubwa sana ambao JK hakuuweza. Labda niseme kwamba cheo cha Urais ni kikubwa sana ukilinganisha na uwezo wake na sio swala la mapungufu yake tena. JK ameichukua nchi ktk hali ambayo haina DIRA hilo kwanza, pili Ubepari haupo ktk misngi inayofanana na tamaduni zetu hata iwe free market. Na alipoingia madarakani alifikiria anaweza kuibadilisha nchi kwa kuweka maono yake - vision ambayo ilikuwa kuyabadilisha MAZINGIRA yetu kwa manufaa ya WATU - Maisha bora kwa kila Mtanzania.

Lakini toka Azimio la Zanzibar na Ubepari, tumezaa Utaifa mpya wa darwin kama poriu la Serengeti. Competition bila viwanda ama uzalishaji ukazaa inequality..nayo ika constitute diverse ktk makundi ya kijamii, conflict of interests, valueless attitude, and crime norms kuibuka kiasi kwamba wakaibuka untouchables, sheria ikawa haina nguvu tena. Kushindwa kwa JK hakukuanza alipoingia madarakani bali kumetokana na watu na mazingira aloyakuta ambayo kulikuwa na watu above the law!.

Ndio maana ahadi zake zote zilikuwa hadi hewa, kutokana na kwamba alipoingia Ikulu aliwakuta WATU (wananchi wenyewe) ambao hawataki kubadilika wao isipokuwa kuyabadilisha mazingira yao ili wapatiwe maisha bora. Na wale wachache waliokuwa naye ktk safari ndefu ya kupata madaraka haya pia walikuwa na fikra za kujenga mazingira yatakayoweza kubadilisha maisha yao bila dira ya kitaifa. Ubepari sio dira na hauwezi kuchukuliwa kirahisi kama free market economy bali huja madudu yake.

Hizi ndizo siasa zilizoasisiwa na Mwinyi, Mkapa na leo hii tunaye JK ambao wote kwa kiwango chao cha utawala ktk kiti cha Urais walikuwa wakilenga kubadilisha maisha yao na sio kutumia mazingira tulinayo yaweze kukuza uchumi wetu na hata kuboresha maisha ya wananchi. Mtanisamehe kusema kwamba hawa wote hawakuwa na sifa za urais bali waandaliaji wa harusi (Wedding planner) kwa kuwaahidi wananchi harusi kubwa lakini wasijue harusi hiyo itaweza kudumu kwa muda gani. Matokeo yake ndio tumezaa Ufisadi ambao wao wanasema sio tatizo, Ufisadi ukazaa ubinafsi ambao ukazaa Udini na matabaka yote haya yamejenga umaskini zaidi na zaidi. Ubepari kwa Tanzania ni sawa na kuomba mvua zinyeshe ili muanze kulima badala yake yakatokea mafuriko ambayo viongozi wote wameshindwa.

Ni rahisi sana kumlaumu JK, lakini yeye ni reflection yetu sisi, leo nenda maofisini utakuta asilimia 20 ya waajiriwa ni ndugu au marafiki waliopeana pande. Humjui mtu huwezi upata ajira, humjui mtu huwezi kutoa mzigo wako bandarini kwa bei nafuu, humjui mtu huwezi kupata mkopo benki acha mbali kumpatia nafasi ya shule mwanao, haya yote hayafanyi JK bali sisi wenyewe toka ngazi ya mawaziri hadi mchoma nyama mitaani. Tupo ktk Culture conlfict
Mkuu Mkandara, kusema ukweli you deserve to be a true teacher, imparting knowledge in a very good way. Hii "culture conflict" ndio naisikia kwako, najisikia kama nimerudi darasa la DS la Rugumamu!.Thanks for this!.

Sijakuelewa uliposema "ni rahisi kumlaumu JK lakini sii yeye bali reflection yetu sisi" unamaanisha wakulaumiwa ni sisi na sio JK?.
 
Nadhani tujilaumu sisi kwa kushindwa kuelimisha uma umuhimu wa kutumia haki yao ya msingi ya kupiga kura.

Pia tujialumu kwa kupitisha mtu mtu ambaye tuna hakika hata apewe miaka 1000 hawezi pata dira ya kuongoza nchi.

Kwa hayo, tunahitaji jilaumu.

Sijakuelewa uliposema "ni rahisi kumlaumu JK lakini sii yeye bali reflection yetu sisi" unamaanisha wakulaumiwa ni sisi na sio JK?.
 
Mkuu Mkandara, kusema ukweli you deserve to be a true teacher, imparting knowledge in a very good way. Hii "culture conflict" ndio naisikia kwako, najisikia kama nimerudi darasa la DS la Rugumamu!.Thanks for this!.
Sijakuelewa uliposema "ni rahisi kumlaumu JK lakini sii yeye bali reflection yetu sisi" unamaanisha wakulaumiwa ni sisi na sio JK?.
Shukran mkuu wangu maana najua swali lako linabeba uzito mkubwa zaidi ya kutazama mapungufu ya JK kama rais.
Niliposema Jk ni reflection yetu ina maana hiyo kweli. Ebu nambie tulimchagua Jk kwa sababu gani? Na hata mara ya pili baada ya kufanya vibaya Kwa nini tumlaumu yeye na sio sisi wenyewe ikiwa maamuzi yetu wenyewe hutegemea kuhadaiwa na kudangaywa hata kama vitu vyenyewe havi make sense.

Mimi nilipokuwa Dar last year nimegundua kwamba JK anachukiwa zaidi na Watanzania waishio nje kuliko ndani na hasa Dar. Na nilipojaribu kujichanganya na marafiki wa zamani niliwakuta wao wasanii kuliko hata JK mwenyewe.Yaani kwa mtu anayetoka nje hasa sisi tulokulia wakati wa Nyerere tunapata wakati mgumu sana Tanzania na inatokana na watu kubadilika na kuwa wabinafsi kupita maelezo.
.
Mnavyomuona JK ndivyo sisi tunaokuja nchini huwaona kina JK kila kona. Ndio maana nasema tupo ktk culture conflict ambayo tumeshindwa kuimudu. Matatizo yetu sio ktk mahitaji tena ila Uhaba wakati uwezo hatuna ila tunataka tuishi kama Ulaya.
 
Kwanza, ameshindwa kuset national priorities. Leo hii hatujui Tanzania inasimamia nini. Its undefined save for its intention to fight malaria and HIV/AIDS and this being an agenda from American people.

2. Weakness ya pili ni kumchagua Pinda kuwa PM. Alifanya akidhani atapata mtu wa kumcontrol bt amejimaliza. . . The guy is very incompetent
 
Mkuu Edson, du!. Huyu binti yako si mchezo, nitaipeleka hii barua Daily News waitumie kwenye barua za wasomaji na pia gazeti la Uhuru ili waitafsiri!.

Ila pia lazima tukubali kuna nondo fulani zinaandikika vizuri kwa lugha za wenzetu. Bora barua hii imeandikwa kwa kizungu, maana akiyaandika haya kwa lugha yetu, adhimu ya Kiswahili, tutaishia kuonekana kama unamtukana mtukufu rais!.

Mkuu Pasco, binti kanifurahisha. Ati akipewa nafasi anaweza kabisa kuongoza nchi.
Ningependa kufanya nae kazi kwa karibu maana inaelekea si tuu kwamba ni mzuri wa akili bt everythn! Natamani mkulu angepata hii asome, maana anatafanya watanzania wote tuonekane waajabu
 
Mkuu Waberoya, nilipikusoma unawaita watu majuha, kwanza nilishtuka, niliposoma tena nikajifariji kumbe hao majuha ni wa CCM!. Hata kama ni ukweli unawaona CCM majuha, huku sii kuwatukana?!. Si niliomba tuepuke matukano na lugha za staha?!.

Nikirudi kwenye mada, please lets be realistic, hivi ni kweli ni rais Kikwete ndiye anategemewa afanye kila kitu?!. Hao mawaziri wake na wasaidizi wake wanafanya kazi gani?!. Rais aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania, baada ya ahadi hiyo lilibaki jukumu la timu yake kupanga malengo na kujadili utekelezaji, sasa kama malengo yamepangwa na hayakufikiwa kosa ni la nani?.

Thank God nilikuwepo alipotembelea baadhi ya taasisi akapanga malengo na baada ya miaka mitano akapita tena, kule kule watu wale wale na nyimbo zile zile!. Ni nani hakutimiza wajibu wake?!.

Waberoya wewe uu miongoni mwa ma greti thinka wetu humu jukwaani, kama ni mtazamo huo ni ujuha, weka basi na mtazamo wako ambao sio wa kijuha kama mtazamo huu!.

Pasco usinichefue na kauli zako za kishabiki! Rais kama mtendaji mkuu wa serikali anaweka malengo na kusubiri miaka mitano kwenda kufanya tathmini ya utekelezajo?! Hii aibu ya karne!

Yaani JK aligombea urais akijua ataweka malengo na kuanza kufanya utalii duniani akijua mambo yataenda yenyewe bila yeye kufanya tathmini za muda mfupi na mrefu kuona kama mambo yako sawa au kunahaja ya kufanya marekebisho? Huo ni udhaufu mkubwa sana ambao Watz hatukupaswa kumsamehe.

Mimi ninavyoona ni kwamba JK hana hata ufahamu kidogo kwenye menejimenti na utawala. Anafanya kazi zake kwa kudra za mwenyezi Mungu; kama vile tusivyoweza kubadili ratiba ya jua ndivyo JK anavyoiendesha TZ yetu! Anaacha nature ijitafutie balance yenyewe! Shame on JK, shame on TZans!
 
Mapungufu yake ni kutokuwa serious kwenye serious issues.

Vyombo vya habari vilimnukuu Mahalu katika utetezi wake mahakamani kuwa wakati akiwa waziri alimpa go ahead Mahalu katika ununuzi wa nyumba ya ubalozi wa Italy, na kwamba kuna siku alimpelekea taarifa juu ya mwenendo mzima wa mchakato lakini hakujibu kitu na badala yake alitabasamu tu.
 
..... Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.

Pasco, birds of like feathers flock together.
Hao watendaji ambao unadhani hawawajibiki ipaswavyo kawateua yeye kwa hiyo ni taswira yake mwenyewe, na wengine kafanya nao kazi kwa zaidi ya miaka kumi na zaidi, kwa hiyo hii si hali ya bahati mbaya na haiwezi kuwa excuse ya kutowawajibisha ama yeye mwenyewe kutowajibika kwa makosa ya uteuzi wake. Kama anaona wanamwangusha basi angetengua uteuzi wao kama alivyotengua uteuzi wa ndg Albert Mnali, yule DC aliyewacharaza bakora walimu kule Kagera. Simple! Kwa kuwa umeomba tutoe ukosoaji wa kujenga, basi naendelea kama hivi:-

1. Atengeneze upya (kwa muda uliosalia) maono na dira ya chama na serikali yake ili kurekebisha mapungufu mengi ya kiutendaji tunayoyaona leo kwenye kila sekta. Maisha bora kwa kila Mtanzania yameshindikana, Tanzania yenye neema huwa tunaota ndotoni, ari, nguvu na kasi mpya hakuna mahali zinaonekana. Leo petroli haishikiki, Dar lita shilingi 2174 (sijajua pale Kasulu inauzwaje).

2. Apunguze matumizi yasiyo ya lazima ya rasilmali za serikali. Hapa naongelea matumizi ya magari ya bei mbaya ya wakurugenzi wa idara na vitengo vya serikali, na safari za nje ya nchi zisizo za lazima za watendaji wa serikali. Gharama za uendeshaji wa magari hayo ni za juu, hivyo katika misafara ya viongozi zile convoy zipunguzwe uwingi. Sambamba na hilo apunguze matumizi yasiyo ya lazima kama vile sherehe zisizo na mashiko, ili kiasi cha pesa kinachopatikana kiende kusaidia sekta kama vile kilimo na afya.

3. Atenge vipaumbele vichache tu vya taifa, ambavyo hata viongozi wajao waige na kuviendeleza. Hawezi akaweka kila kitu kuwa ni kipaumbele kama ilivyo sasa. Mkapa aliweka kipaumbele kwenye elimu (MMES, MMEM nk.) na miundombinu. Yeye angeweza kuweka kipaumbele kwenye kilimo ama maliasili.

4. Awawajibishe viongozi wasiotimiza majukumu yao, asiwaonee aibu. Masaburi kauza shirika la serikali (UDA) bado anapeta mtaani. Wezi wa EPA bado wapo serikalini. Chenge amekula cha juu katika rada, bado anapeta. Hatuwezi kwenda mbele kimaendeleo kwa namna hii.
Naomba kuwasilisha.
 
Mkuu Waberoya, nilipikusoma unawaita watu majuha, kwanza nilishtuka, niliposoma tena nikajifariji kumbe hao majuha ni wa CCM!. Hata kama ni ukweli unawaona CCM majuha, huku sii kuwatukana?!. Si niliomba tuepuke matukano na lugha za staha?!.

Nikirudi kwenye mada, please lets be realistic, hivi ni kweli ni rais Kikwete ndiye anategemewa afanye kila kitu?!. Hao mawaziri wake na wasaidizi wake wanafanya kazi gani?!. Rais aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania, baada ya ahadi hiyo lilibaki jukumu la timu yake kupanga malengo na kujadili utekelezaji, sasa kama malengo yamepangwa na hayakufikiwa kosa ni la nani?.

Thank God nilikuwepo alipotembelea baadhi ya taasisi akapanga malengo na baada ya miaka mitano akapita tena, kule kule watu wale wale na nyimbo zile zile!. Ni nani hakutimiza wajibu wake?!.

Waberoya wewe uu miongoni mwa ma greti thinka wetu humu jukwaani, kama ni mtazamo huo ni ujuha, weka basi na mtazamo wako ambao sio wa kijuha kama mtazamo huu!.

Mkuu matusi si sawa kweli

1. Ila mbona na wewe unachoandika ni ku high light kwamba team leader ndo mzizi wa tatizo????
2. Is this your perspective as well????
3. Au ndo hii unaiita "huruma" ??? ndo maana I asked you kwa nini umeamua kutumia neno "constructive critcism" hujajibu badala yake umegonga like.....kwa swali hili like yako haisaidii mkuu but objective answers

Mytake; An open ended dialogue like the one you have set....will neva get you the reality as the variable you have used "constructive criticism" is immesurable nilikuuliza yale maswali ili kuku-alert kwamba huu uzi utaleta matusi na lugha isiyopendeza because it is a subjective one..........so you now reap what you previously sow
 
Mkuu matusi si sawa kweli

1. Ila mbona na wewe unachoandika ni ku high light kwamba team leader ndo mzizi wa tatizo????
2. Is this your perspective as well????
3. Au ndo hii unaiita "huruma" ??? ndo maana I asked you kwa nini umeamua kutumia neno "constructive critcism" hujajibu badala yake umegonga like.....kwa swali hili like yako haisaidii mkuu but objective answers

Mytake; An open ended dialogue like the one you have set....will neva get you the reality as the variable you have used "constructive criticism" is immesurable nilikuuliza yale maswali ili kuku-alert kwamba huu uzi utaleta matusi na lugha isiyopendeza because it is a subjective one..........so you now reap what you previously sow

kuitwa JUHA si tusi ni sifa ni sawa mtu anakuambia;
wewe unaakili
wewe mweupe
wewe mnene
wewe taahila
wewe mjinga
wewe Fisadi
zoote hizo ni sifa na sifa haziwezi kuwa tusi, tatizo kunasifa nzuri na mbaya, Nikujitahidi tuu kutoka kwenye sifa mbaya na kwenda kwenye nzuri! KISWAHILI KIGUMU WAKUUU!
 
Shukran mkuu wangu maana najua swali lako linabeba uzito mkubwa zaidi ya kutazama mapungufu ya JK kama rais.
Niliposema Jk ni reflection yetu ina maana hiyo kweli. Ebu nambie tulimchagua Jk kwa sababu gani? Na hata mara ya pili baada ya kufanya vibaya Kwa nini tumlaumu yeye na sio sisi wenyewe ikiwa maamuzi yetu wenyewe hutegemea kuhadaiwa na kudangaywa hata kama vitu vyenyewe havi make sense.

Mimi nilipokuwa Dar last year nimegundua kwamba JK anachukiwa zaidi na Watanzania waishio nje kuliko ndani na hasa Dar. Na nilipojaribu kujichanganya na marafiki wa zamani niliwakuta wao wasanii kuliko hata JK mwenyewe.Yaani kwa mtu anayetoka nje hasa sisi tulokulia wakati wa Nyerere tunapata wakati mgumu sana Tanzania na inatokana na watu kubadilika na kuwa wabinafsi kupita maelezo.
.
Mnavyomuona JK ndivyo sisi tunaokuja nchini huwaona kina JK kila kona. Ndio maana nasema tupo ktk culture conflict ambayo tumeshindwa kuimudu. Matatizo yetu sio ktk mahitaji tena ila Uhaba wakati uwezo hatuna ila tunataka tuishi kama Ulaya.

Well analysed lakini hapo kwenye bold sijakupata vizuri

1. Does it stand to mean we we are incapable of living European standard???

2. When mentioning "culture conflict" sijui kama unamaanisha IDEOLOGY at the same time coz to me hata kama watu (individually) wako kwenye hiyo cultural shock still ni state ideology ndo iko resonsible kuweka hatamu na kuifuatilia na hii
si kazi ya mtanzania mmoja mmoja!!!!

3. Tuchukue azimio la Arusha kwa mfano....wananchi mmoja mmoja walikuwa na role gani ambayo leo wameiacha????? I was expecting kipindi hiki ndo ingekuwa worse hii shock unayoizungumzia koz it was an even breaking but now with 50 years of independence and experience this could not be the basket to carry the failures with

4. Wakati wa uhujumu uchumi hakuna sehemu nimewahi kusoma lawama kupelekwa kwa wananchi the way you argue in a language of "our reflexion " ila baada ya Tatizo kujulikana state ndo ilideal na wahujumu because IDEOLOGY was stable and the system was working

Thus; Unless we have a strong and determined state IDEOLOGY and the proper system to ensure effectiveness and sustainability of the IDEOLOGY even engels will never get us to greener pastures


Good living standards leaving alone the European style are possible if and only we first know the importance of having an IDEOLOGY and to die fighting for it; for the little I know hii ilikuwa nguzo muhimu sana kwa uongozi wa marehemu J.K. Nyerere (RIP)
 
Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.

Na stratergy ya ya kufanikisha hiyo ndio ipi? Je kulikuwa na SMARTness kwenye hiyo objective kama at all alifika that far?
 
Yamezungumzwa mengi sana kuhusu JK ktk kumsifia na mapungufu yake lakini kama Pasco alivyosema binadamu hakosi kasoro na zitazo jitokeza lazima zipimwe ktk kiwango fulani kuweka upungufu huo. Na katika kupima mapungufu hayo inawezekana kuwa ni chupa ilijaa nusu au chupa ilipungua nusu ujazo..

Binafsi yangu nitasema kwamba matatizo ya Tanzania yetu ni zaidi ya JK.. tuna Culture conflict yaani tupo dunia ya kusadikika. WATU na MAZINGIRA yenyewe ni mzigo mkubwa sana ambao JK hakuuweza. Labda niseme kwamba cheo cha Urais ni kikubwa sana ukilinganisha na uwezo wake na sio swala la mapungufu yake tena. JK ameichukua nchi ktk hali ambayo haina DIRA hilo kwanza, pili Ubepari haupo ktk misngi inayofanana na tamaduni zetu hata iwe free market. Na alipoingia madarakani alifikiria anaweza kuibadilisha nchi kwa kuweka maono yake - vision ambayo ilikuwa kuyabadilisha MAZINGIRA yetu kwa manufaa ya WATU - Maisha bora kwa kila Mtanzania.

Lakini toka Azimio la Zanzibar na Ubepari, tumezaa Utaifa mpya wa darwin kama poriu la Serengeti. Competition bila viwanda ama uzalishaji ukazaa inequality..nayo ika constitute diverse ktk makundi ya kijamii, conflict of interests, valueless attitude, and crime norms kuibuka kiasi kwamba wakaibuka untouchables, sheria ikawa haina nguvu tena. Kushindwa kwa JK hakukuanza alipoingia madarakani bali kumetokana na watu na mazingira aloyakuta ambayo kulikuwa na watu above the law!.

Ndio maana ahadi zake zote zilikuwa hadi hewa, kutokana na kwamba alipoingia Ikulu aliwakuta WATU (wananchi wenyewe) ambao hawataki kubadilika wao isipokuwa kuyabadilisha mazingira yao ili wapatiwe maisha bora. Na wale wachache waliokuwa naye ktk safari ndefu ya kupata madaraka haya pia walikuwa na fikra za kujenga mazingira yatakayoweza kubadilisha maisha yao bila dira ya kitaifa. Ubepari sio dira na hauwezi kuchukuliwa kirahisi kama free market economy bali huja madudu yake.

Hizi ndizo siasa zilizoasisiwa na Mwinyi, Mkapa na leo hii tunaye JK ambao wote kwa kiwango chao cha utawala ktk kiti cha Urais walikuwa wakilenga kubadilisha maisha yao na sio kutumia mazingira tulinayo yaweze kukuza uchumi wetu na hata kuboresha maisha ya wananchi. Mtanisamehe kusema kwamba hawa wote hawakuwa na sifa za urais bali waandaliaji wa harusi (Wedding planner) kwa kuwaahidi wananchi harusi kubwa lakini wasijue harusi hiyo itaweza kudumu kwa muda gani. Matokeo yake ndio tumezaa Ufisadi ambao wao wanasema sio tatizo, Ufisadi ukazaa ubinafsi ambao ukazaa Udini na matabaka yote haya yamejenga umaskini zaidi na zaidi. Ubepari kwa Tanzania ni sawa na kuomba mvua zinyeshe ili muanze kulima badala yake yakatokea mafuriko ambayo viongozi wote wameshindwa.

Ni rahisi sana kumlaumu JK, lakini yeye ni reflection yetu sisi, leo nenda maofisini utakuta asilimia 20 ya waajiriwa ni ndugu au marafiki waliopeana pande. Humjui mtu huwezi upata ajira, humjui mtu huwezi kutoa mzigo wako bandarini kwa bei nafuu, humjui mtu huwezi kupata mkopo benki acha mbali kumpatia nafasi ya shule mwanao, haya yote hayafanyi JK bali sisi wenyewe toka ngazi ya mawaziri hadi mchoma nyama mitaani. Tupo ktk Culture conlfict

Duh! mkuu post nzuri ya kiume kabisa kabisa kabisa kabisa

JK kazaliwa Tanzania, kakulia tanzania, kalelewa tanzania, kaishi tanzania , kachaguliwa na watanzania , ni rais wa watanzania..JK ndiyo jamii yenyewe.

ukweli mchungu huu
 
Back
Top Bottom