Mapokezi ya Rais wa Bank ya Afrika ni zaidi ya Rais wa Nchi

Habari ni habari, nini maana ya forum?...ni kujuzana yanayojiri, unataka kusema kuwa hoja hii haipaswi kufahamika kwa wadau? Au huwa hausafiri na kujifunza mambo?, USHAURI WA BURE: Tembea na ujifunze kwa watu, ili kujua wenzako wanafanya nini, kwanini, wapi na lini..hiyo itakusaidia sana.

Karibu Arusha, Mkutano ni wa delegates zaidi ya 3000, hakuna pa kulala kama sio mwenyeji wa Arusha labda uwe ulifanya booking mwezi uliopita( Mwezi April)

mkuu mwache huyo. Hoja yako ina mashiko
 
Haya ..niko Arusha,Mkutano wa Bank ya Maendeleo ya Afrika (African Development Bank) kwa hapa umekuwa hosted na Wizara ya Mkulo(nakumbuka tulikaa vikao vingi sana kuhakikisha mkutano huu unafanyika Afrika Mashariki, Mkulo akapiga debe kwamba "Tanzania Tunaweza Bila Kuwezeshwa"kweli ukaja Arusha... lugha tunayoitumia ni Kiingereza na Kifaransa....wafaransa wa kizungu na wa kiafrika...kiswahili NO, mimi naongea kiswahili,. nakutana na mmoja wa waandaaji wa mkutano huu wa kimataifa wa wachumi."votre nom siil vous plait?=Your name please? najitambulisha,naye pia anajitambulisha kwangu, ana uraia wa nchi mbili Ghana na Ufaransa, ni dada mcheshi, mzungu, na ni mara yake ya kwanza kuja Tanzania, tunasalimiana, lakini ghafla Magavana wanaanza kuingia, mnisamehe sijapiga picha..waandishi wa habari usiseme.

Msafara wa rais wa bank ya maendeleo ya Afrika anakaribia kuingia hapa...maafisa usalama kama kawaida.Askari wamejipanga kwa ajili ya kutoa heshima kwa Rais, wote wana silaha...wanapokea maelekezo. mkutano haufanyiki hapa hotelini, ni eneo la AICC(Arusha International Conference Center) hapa ni kula na kulala tu...na vikao vingine vidogovidogo(billateral meetings, working conferences na Launching of AGF, Mabenki yote yana uwakilishi hapa.Wawakilishi wa bank mbalimbali wako hapa, makampuni ya simu pia, TANAPA wanaongoza kwa kuutangaza utalii.

Naiona red carpet kutoka mlangoni hadi kwenye kambarau (lift)ya hotel....

Pikipiki za polisi ziko nne, zinaingia kwa mbwembwe, askari wa usalama barabarani wako hadi ndani ya hotel wanaelekeza magari kila mahali..haya zinaingia gari za polisi kama nne, Field Force Unit, Ambulance ya polisi, Magari aina ya PRADO hayana idadi...yote yana nembo ya kampuni ya ANGONI. Magari madogo madogo na yale ya kukodi hayana idadi. La mheshimiwa silioni,..huyu hapa anashuka, ni mtu wa makamu kidogo, amevaa shati la rangi ya kijivu, suruali nyeusi, na miwani ya jua,. tunampokea anatupa mikono mmoja baada ya mwingine..anasema jambo karibu Tanzania, no anaongea kiswahili, jamani anaongea kiswahili safi...(nimerudi nyumbani,,,,anasema) ni mwafrika kutoka Africa ya...aaaaaaaaaaaaahh, kumbe ni Mheshimiwa Donald Kaberuka, Mnyarwanda anayeitumikia Bank hiyo kwa kipindi cha pili(Miaka Mitano).Anaelekezwa kwenda katika kambarau (lift)..anaingia...end of story. tuliobaki nje, raia na maafande wa usalama wote tunaelekea maeneo yetu muhimu.

Amesoma hapahapa Tanzania na Uingereza na Mwaka 1997 alikuwa waziri wa fedha wa Rwanda...Si tu anapewa salamu za ki-protokali, bali pia nimeangalia wingi wa askari eneo hili na aina ya ulinzi kwa mtu ambaye kwangu naona bora angepokewa kawaida kama viongozi wengine na sio mapokezi zaidi ya yale ya rais wa nchi...haya ngoja tuone mapokezi ya Kikwete kesho hapahapa katika hotel ya Mount Meru, Arusha

​Mkulo ana wizara?
 
Rais anaongea , mawaziri, kibao, kila mtu mfaransa hapa....niko busy mniache kidogo ila Wizara ya Fedha imenunua TV aina SAMSUNG za inchi 65, ziko 60 na kila moja ni zaidi ya TSH 10M, zinazotumika ni 19 AICC, na Mount Meru Hotel 3 tu..mimi sijui zingine ziko wapi,eti wameamua kupotezea
 
Rais anaongea , mawaziri, kibao, kila mtu mfaransa hapa....niko busy mniache kidogo ila Wizara ya Fedha imenunua TV aina SAMSUNG za inchi 65, ziko 60 na kila moja ni zaidi ya TSH 10M, zinazotumika ni 19 AICC, na Mount Meru Hotel 3 tu..mimi sijui zingine ziko wapi,eti wameamua kupotezea

Mchanga wa Macho huo ni kawaida watu kutumia mikutano kama hii kuiibia serikali ,na hapo bado utukuta ukodishwaji wa magari hewa,bili hewa za hoteli na migarama kibao ambayo haihusiki na mkutano .kuna watu wakitoka hapo nyumba inaanzia kiwanja hadi fensi na mlinzi getini ndio anasimama kutafuta mpangaji. kama ulisikia ya CHOGM uganda ,walivyonunua magari hewa kwa ajili ya mkutano na hapa yapo sana tuuuuuuuuu..
 
Mikutano mikubwa kama hiyo ni ufisadi mtupu .CAG wetu Utouh fuatilia ,itakuwa kama mkutano wa Jumuia ya Madola Uganda ambapo Makamu wa Rais Prof Buganda alifisadi na atimaye akatupiliwa mbali Rais huku kesi mahakamani ikinendelea.Huo Mkutano Mkulo mzee wa Malawi alipania na amekula chake kabla bunge alijamtimua.
 
Ni kweli, nafasi hakuna...zote zenye majina haya zimejaa pia ( INNS, RESORTS, GUEST HOUSES, MOTELS, DELUXES)nakwambia zote zimejaa. mkutano unaanza kesho, AICC, Simba Hall. Pia Kumbi za Mbayuwayu,Tausi,Mbuni na Manyara ziko booked hadi mkutano uishe.

Mbona ****** Bar $ G. House kuna nafasi bana.
 
hahaha Herald Hunter;3944722 ripoti yako ni kama live...
Haya ..niko Arusha,Mkutano wa Bank ya Maendeleo ya Afrika (African Development Bank) kwa hapa umekuwa hosted na Wizara ya Mkulo(nakumbuka tulikaa vikao vingi sana kuhakikisha mkutano huu unafanyika Afrika Mashariki, Mkulo akapiga debe kwamba "Tanzania Tunaweza Bila Kuwezeshwa"kweli ukaja Arusha... lugha tunayoitumia ni Kiingereza na Kifaransa....wafaransa wa kizungu na wa kiafrika...kiswahili NO, mimi naongea kiswahili,. nakutana na mmoja wa waandaaji wa mkutano huu wa kimataifa wa wachumi."votre nom siil vous plait?=Your name please? najitambulisha,naye pia anajitambulisha kwangu, ana uraia wa nchi mbili Ghana na Ufaransa, ni dada mcheshi, mzungu, na ni mara yake ya kwanza kuja Tanzania, tunasalimiana, lakini ghafla Magavana wanaanza kuingia, mnisamehe sijapiga picha..waandishi wa habari usiseme.

Msafara wa rais wa bank ya maendeleo ya Afrika anakaribia kuingia hapa...maafisa usalama kama kawaida.Askari wamejipanga kwa ajili ya kutoa heshima kwa Rais, wote wana silaha...wanapokea maelekezo. mkutano haufanyiki hapa hotelini, ni eneo la AICC(Arusha International Conference Center) hapa ni kula na kulala tu...na vikao vingine vidogovidogo(billateral meetings, working conferences na Launching of AGF, Mabenki yote yana uwakilishi hapa.Wawakilishi wa bank mbalimbali wako hapa, makampuni ya simu pia, TANAPA wanaongoza kwa kuutangaza utalii.

Naiona red carpet kutoka mlangoni hadi kwenye kambarau (lift)ya hotel....

Pikipiki za polisi ziko nne, zinaingia kwa mbwembwe, askari wa usalama barabarani wako hadi ndani ya hotel wanaelekeza magari kila mahali..haya zinaingia gari za polisi kama nne, Field Force Unit, Ambulance ya polisi, Magari aina ya PRADO hayana idadi...yote yana nembo ya kampuni ya ANGONI. Magari madogo madogo na yale ya kukodi hayana idadi. La mheshimiwa silioni,..huyu hapa anashuka, ni mtu wa makamu kidogo, amevaa shati la rangi ya kijivu, suruali nyeusi, na miwani ya jua,. tunampokea anatupa mikono mmoja baada ya mwingine..anasema jambo karibu Tanzania, no anaongea kiswahili, jamani anaongea kiswahili safi...(nimerudi nyumbani,,,,anasema) ni mwafrika kutoka Africa ya...aaaaaaaaaaaaahh, kumbe ni Mheshimiwa Donald Kaberuka, Mnyarwanda anayeitumikia Bank hiyo kwa kipindi cha pili(Miaka Mitano).Anaelekezwa kwenda katika kambarau (lift)..anaingia...end of story. tuliobaki nje, raia na maafande wa usalama wote tunaelekea maeneo yetu muhimu.

Amesoma hapahapa Tanzania na Uingereza na Mwaka 1997 alikuwa waziri wa fedha wa Rwanda...Si tu anapewa salamu za ki-protokali, bali pia nimeangalia wingi wa askari eneo hili na aina ya ulinzi kwa mtu ambaye kwangu naona bora angepokewa kawaida kama viongozi wengine na sio mapokezi zaidi ya yale ya rais wa nchi...haya ngoja tuone mapokezi ya Kikwete kesho hapahapa katika hotel ya Mount Meru, Arusha
 
Last edited by a moderator:
Usijali ndugu yangu na pia samahani kwa wanajamii wote kwa kuandika kwa kifupi .Maana yake ni African Guaranteed Fund (AGF).
 
hapa kuna wakubwa ambao tayari walishachukua shekeli zao mapema: Miundombinu, Uchukuzi, Mambo ya Ndani, Fedha,nk..Kuna shuttles(magari maalum ya abiria) Delegate hata kama ni mmoja tu anabebwa hakuna kumsubiri mwingine hapa. Mfano huyu yuko Ngurdoto na anataka kwenda Mount Meru Hotel Hotel, anaondoka saaa hiyo bila kujali kuna mwingine.

Aina za shuttle, 1.Dar Express(Hii ni kufuru basi la abiria 65 kutumiwa na mtu mmoja, magari hayo yapo standby, yanapaki maeneo ya hotel tajwa ( Kibo Palace, Mount Meru Hotel, Impala, Naura Spring, Palace Hotel pia lakini kidogo kutokana na ufinyu wa parking, 2. Magari aina ya coaster, penye msafara wa kenge na mamba pia wamo, hawakosekani.Mnisamehe kutokuwa na uwezo wa kuwatumia picha kutokana na sababu chanya nyingi...ila nawaahidi kutuma mara baada ya mkutano.

Naendelea kuwasilisha.
 
Ndio. anayo. Huyu Mustafa Mkaidi Mwenye Kula...huijui wizara yake, "Ni Waziri wa Wizara ya Ubadhirifu" makao yake kwa sasa yapo nyumbani kwake.....NEWS: wale faru wa Kikwete kule serengeti wote wameuawa..walikuwa watatu tu. Ila wauaji hawakukamatwa kwani walikuwa wamejidhatiti. Waliofukuzwa kazi kwa uzembe huo ni foleni kuwataja, ila kwa haraka Mkubwa wa int.....nsia naye kafukuzwa katika uzembe huo.Nimedokeza hili kwani rafiki yake wa siku nyingi, Mzee Festus G Mogae(Rais wa zamani wa Botswana) Kaniuliza leo mbuga ipi nzuri na ina aina gani ya wanyama wapo. Ndio maana nimeikumbuka hii.Subiri, laptop yangu ni ya kizamani kidogo, Hapa namuona Ngozi Okonjo Iweala...nitawaambia ni nani..........waaaaaait kidogo natoka nitarudi.
 
mkutano unaendelea ila chief of protocol wa rais huenda akapigwa chini kwa kukiuka maadili ya kiapo alichokula, kutoa miongozo yote ya safari na mikutano ya rais, kasababisha rais kukaa nje kwa takriban dakika 25 hivi kwani chumba chake kwa ajili ya mikutano ya ndani(Constituency meeting Room kilitumiwa na mmoja wa mawaziri wa fedha kutoka west africa. Tukio hili lilimgharimu kupewa onyo mara kadhaa na hatimaye kuambiwa na secretary wa ofisi ya rais kuwa asubiri maamuzi ya katibu wa rais ambaye ndiye mwajiri wake ...hii ni kulingana na katiba ya bank hiyo.
 
Herald Hunter hata mimi nimependa ilivyoripoti. Graphology ya key board yako kama Hutaki Unaacha!.

Kwa taarifa tuu, AFDB ndiye the top best imployer Tanzania anayelipa top salary na top benefits!. Amewapita mpaka UN, Mashirika ya kimataifa kama DFID na makampuni ya madini kama kina ABG wamewaacha mbali!.

Amini usiamini, every cent spent itakuwa imetolewa nao hao hao AFDB!.
 
Rais ndio anawasilisha hoja zake kabla ya kumpangia nani apate nini kwa mradi gani...(african guaranteed fund-AGF launching), Hapa Mount Meru Hotel...we acha tu...Hii miradi ya maendeleo bwana, nina wasiwasi na masharti yake...
 
Mkutano ndio umeisha, Dola za marekani milioni 50 kuzinufaisha nchi mbalimbali za Bara hili (Afrika) kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo. Inategemea nani kajipanga vipi..na anahitaji msaada (mkopo) wa dola ngapi na kwa mradi upi. Hii ni kutokana na Kitengo kimoja cha ufadhili kupitia udhamini wanaoutoa.

Kilichobaki ni picha za matukio jinsi yalivyokuwa...Yule Protocol Officer wa Rais katupwa nje, ni kijana mdogo kama miaka 28 hadi 32 na si zaidi ya hapo, najua pia atakuwa na familia inayomtegemea. Ninhgekuwa rais ningemsamehe.
 
Mhe. Rais JK Kaingia kuja kumsalimia Rais mwenzake wa Bank, ila hapa mimi naona kuna tatizo...Huyu mwenzake yuko juu chumbani..kagoma kushuka ground floor ambako wameandaliwa..inabidi Mhe. Rais wetu amfuate huko huko juu ili wasalimiane...hapa hakuna lililo kuu zaidi ya kusalimiana...JK ana majukumu yanayomkabili, ana takiwa akampokee Rais wa Burundi...kuwa Kiongozi sio mchezo, hapa ansema ana muda mchache sana na anahitaji awahi kumpokea kiongozi mwenzake wa Burundi.

Leo acha nimsifu JK japo kidogo...chumba alichoandaliwa naye amekikataa kwani kimeandaliwa ki-mkutano zaidi, hivyo kinapaswa kulipiwa $400 kwa dakika 30 tu watakazookaa. Bila kujali kasimama na nani kawabwatukia maafisa wake kuwa hicho chumba kwanini kilipiwe wakati yeye amekuja tu kumsalimia "jamaa" yake. "Jamani mimi nimekuja tu kumsalimia, sasa kwanini mme-complicate mambo namna hii, hiki chumba si kinalipiwa? sasa nani atakilipia?aliuliza (wote kimya na samahani mheshimiwa ndio ikawa njia mbadala, haya haoooooo... JK anasema yuko radhi kukaa mahali popote hajali pakoje.
 
Back
Top Bottom