yaani tatizo nazani walijiunga na hawakupata mda wa kuyajenga kwa kina ni nini hasa kifanyike na wanaungana kwa lipi na lipi.
ilitakiwa wakubaliane kila chama kiendelee kusaka wafuasi wake kila kona na mwisho wa siku itafahamika tuu nani anakubalika na nani hakubaliki kwa kipimo cha uchaguzi mdogo./serikali za mitaa.
jimbo ambalo chama kimeongoza kwa kuwa na viongozi wengivwa serikali za mitaa ndio kiungwe mkono na vyama vingine lakini hili la kusema kugawana majimbo sawa kwa sawa ni kosa kubwa sana maana kile chama kinachokubalika sana na ambacho ni tishio kwa ccm kitakuwa kinatoa point zake zote na kumkabidhi ccm.
kwa mfano kuwe namajimbo 100 na chadema tuseme ikawa ilishinda majimbo 30 na vyama vingine vya upinzani vikashinda majimbo 10 na ccm wakashinda 60. sasa unapo sema mgawanyo wa majimbo uwe sa wa ni kuwa hapo piga uwa utapunguza majimbo kwa cdm na kuongeza kwa ccm.
maana ubaya kuna vyama vingine kuna sehem uungwaji mkono na wananchi ni 0 kabisaaa so unapo wakabidhi jimbo hilo unatoa mwanya kwa ccm kushindaa.