Mapitio ya wimbo: JKT Taarab - Chura

Mapitio ya wimbo: JKT Taarab - Chura

Ms Judith

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2010
Posts
2,563
Reaction score
936
wapendwa,

nimeweka wimbo wa CHURA wa JKT Taarab kwenye lik hii hapo chini:

https://www.jamiiforums.com/entertainment/208761-chura-jkt-taarab-walitisha-sana-enzi-hizo.html

naomba tujadili usahihi wa maneno hayoo yaliyokolezwa rangi nyekundu

WIMBO: Chura
ALBUM:
sina hakika
KUNDI:
JKT Taarab

Chura nakuulizia unipe jibu makini,
kwa kila inyapo mvua wakimbilia bwawani
Huna nguo za kufua na wala huna sabuni,
nijibu yapate tua maji utayafanyani

Chorus
Chura punguza vituko na wako uhayawani,
umezua sokomoko watu hawaeleni
Ukivunjika mgongo, dawa atakupa nani?


2.
Mwenzenu nilikisia ni mlinzi kisimani,
mtu utamzuia maji akiyatamani
Akaja dada Rukia na ndooye mkononi,
chura ukajing`atua ukajitosa pembeni

Chura punguza vituko ………………………

3.
Chura bora kuamua wende kulima shambani,
mazao kujipatia wende kuuza sokoni
Nguo kujinunulia isitiri maungoni,
au ukitaka ndoa nenda kaoe nyumbani.

Chura punguza vituko ………………………

1.
mimi nafikiri badala ya kusema nilikisia, ilipaswa kusemwa nilidhania au nilifikiria, manake makisio ninayoyajua mimi ni "estimates" kwa kiingereza na haiwezekani kwa vyovyote vile kuwa dhana iliyoko kwenye hilo shairi ni "estimate"

2.
na hapo kujing'atua, ukiachilia mbali msuala ya vina na mizani, tusema mwalimu nyerere aling'atuka au naye alijing'atua madarakani??

3.
kuhusu "kujitosa pembeni", hapo pembeni ni wapi, ni kisimani au nje ya kisima, na kama ni nje ya kisima, inawezekana kitu au mtu kujitosa nchi kavu? au kujitosa lazima iwe majini (kisimani/mtoni/ziwani/baharini nk)?

4.hiyo sentensi nadhani iko sawa kisarufi, ila kimantiki ni suala la tafsiri ya neno nyumbani na wakati tu kwamba kwa wakati wa sasa, haisisitizwi kuwenda kuoa nyumbani na kwa wakati huu mtu aweza kuoa popote hata nchi za ng'ambo.

pia baadhi ya mila haziruhusu kuona nyumbani (close relatives). japo kishairi inaeleweka kuwa ililenga kubalance vina na mizani, isipokuwa kama dhana ya neno nyumbani kama inavyotumika, imelenga dhana sawa na "home town/city/country" nk vinginevyo kama ni close relative itakuwa jambo lisilowezekana kwa mila nyingi za kiafrika

nyie mnaonaje wapendwa?

mbarikiwe sana

Glory to God
 
Lugha ya kishairi mara nyingi hainyooki la ujumbe hufika kama inavyotakiwa, pamoja na yote umemwelewa Chura?

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Hii ni fasihi. Na katika fasihi watunzi hutumia maneno anuai hata ya lugha za kigeni ili mradi wapate vina muafaka katika mpangilio wake. Na katika muktadha huo inafika wakati wanaweka maneno kimakosa, sasa hapo hunabudi msomaji ufahamu nini maudhui ya Mtunzi au Mwandishi. Lugha ni Fasihi . Lakini umelielewa Shairi maana yake?
 
wapendwa,

nimeweka wimbo wa CHURA wa JKT Taarab kwenye lik hii hapo chini:

https://www.jamiiforums.com/entertainment/208761-chura-jkt-taarab-walitisha-sana-enzi-hizo.html

naomba tujadili usahihi wa maneno hayoo yaliyokolezwa rangi nyekundu



1.
mimi nafikiri badala ya kusema nilikisia, ilipaswa kusemwa nilidhania au nilifikiria, manake makisio ninayoyajua mimi ni "estimates" kwa kiingereza na haiwezekani kwa vyovyote vile kuwa dhana iliyoko kwenye hilo shairi ni "estimate"

2.
na hapo kujing'atua, ukiachilia mbali msuala ya vina na mizani, tusema mwalimu nyerere aling'atuka au naye alijing'atua madarakani??

3.
kuhusu "kujitosa pembeni", hapo pembeni ni wapi, ni kisimani au nje ya kisima, na kama ni nje ya kisima, inawezekana kitu au mtu kujitosa nchi kavu? au kujitosa lazima iwe majini (kisimani/mtoni/ziwani/baharini nk)?

4.hiyo sentensi nadhani iko sawa kisarufi, ila kimantiki ni suala la tafsiri ya neno nyumbani na wakati tu kwamba kwa wakati wa sasa, haisisitizwi kuwenda kuoa nyumbani na kwa wakati huu mtu aweza kuoa popote hata nchi za ng'ambo.

pia baadhi ya mila haziruhusu kuona nyumbani (close relatives). japo kishairi inaeleweka kuwa ililenga kubalance vina na mizani, isipokuwa kama dhana ya neno nyumbani kama inavyotumika, imelenga dhana sawa na "home town/city/country" nk vinginevyo kama ni close relative itakuwa jambo lisilowezekana kwa mila nyingi za kiafrika

nyie mnaonaje wapendwa?

mbarikiwe sana

Glory to God

Mjadala uendelee...
 
Lugha ya kishairi mara nyingi hainyooki la ujumbe hufika kama inavyotakiwa, pamoja na yote umemwelewa Chura?

Chama
Gongo la Mboto DSM

Mkuu chama wa Gongs,

Hebu fanya maarifa hapo, huyu chura ni nani? mi mpaka leo bado kumjua

Natanguliza shukrani

Asprin
Boko Basihaya, DSM.
 
Last edited by a moderator:
Hii ni fasihi. Na katika fasihi watunzi hutumia maneno anuai hata ya lugha za kigeni ili mradi wapate vina muafaka katika mpangilio wake. Na katika muktadha huo inafika wakati wanaweka maneno kimakosa, sasa hapo hunabudi msomaji ufahamu nini maudhui ya Mtunzi au Mwandishi. Lugha ni Fasihi . Lakini umelielewa Shairi maana yake?

Mkuu mtemiwaWandamba,

Tafadhali saidia mimi kujua maana ya huu ushairi. Huyu chura ni nani anazungumziwa?
 
Last edited by a moderator:
Ms Judith katika thread yako ya kwanza nimeona umetoa like kwa SOBY kuwa ni kiharage
kila mahali kiharage huwa kipo km hakiukung'olewa na kinakaa karibu na kisima kwa vile hudhaniwa huwa ni mlinzi kinatisha sana kwa umbo lakini si lolote hadi hii leo hakizuii lolote na ukitaka kuteka maji chenyewe huondoka na kushangilia mafuriko
Ubeti wa 2.
Mwenzenu nilikisia ni mlinzi kisimani,
mtu utamzuia maji akiyatamani
Akaja dada Rukia na ndooye mkononi,
chura ukajing`atua ukajitosa pembeni
Hizi ni lugha za kughani mashairi na hazifuati kina ila maana huwa nyingi na ndio maana huona watu wengi wanazishobokea
Fuatilia wimbo wa TOT katika Rapping anaposema
anakalia KIGOGO na si MBURAHATI
AU
Gonga mbele x 3 kama mwenyewe hayupo zunguka
Nyuma gonga x 2 km hayupo mwaga mzigo


Kwa hiyo ni kazi kwelikweli km mke wangu akianza kushobokea Taarabu na nyimbo hizo naona km ataniacha?
Na mara nyingi naona 80% ya wapenda Taarabu ndoa zao ..............
 
Last edited by a moderator:
Lugha ya kishairi mara nyingi hainyooki la ujumbe hufika kama inavyotakiwa, pamoja na yote umemwelewa Chura?

Chama
Gongo la Mboto DSM
Mkuu chama wa Gongs,

Hebu fanya maarifa hapo, huyu chura ni nani? mi mpaka leo bado kumjua

Natanguliza shukrani

Asprin
Boko Basihaya, DSM.
Mkuu mtemiwaWandamba,

Tafadhali saidia mimi kujua maana ya huu ushairi. Huyu chura ni nani anazungumziwa?


Churaaaaa...... churaaaaaaaaaaa...........ni


Alex-Chalamila-cut.jpg
 
Jf is never boring. Haya twendeni kwa mrisho mpoto sasa
 
Sizonje.............hii ndiyo nyumba yetu......milango ipo ila wanapita madirishani....
 
CHURA ni me ambaye kukipambazuka, yeye hukaa vipembezoni(chobingo) kutongoza mabinti, mtunzi anamuuliza CHURA kwamba ni hohehahe hana a wala be huyo binti (maji) akimpata atampeleka wapi.
Beti ya pili ameendelea kumuonya aache tabia hiyo maana tayari ni kama wanamvizia watamuumiza atahudumiwa na nani wakati hana mke.
Ubeti WA tatu umejitosheleza. Pia rekebisha hapo si mgongo ni ukivunjika ugoko
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom