Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
Wapendwa,
Hakuna ubishi kuwa huu wimbo ni wa zamani sana na sijui mwaka gani ulitungwa na kuchezwa ila kwa kweli naupenda sana maudhui yake!!
Wakubwa wanasema umejaa mafumbo matupu, anayejua unafumba nini, naomba atujuze.
WIMBO: Chura
ALBUM: Sina hakika
KUNDI: JKT Taarab
MASHAIRI
1. Chura nakuulizia unipe jibu makini,
kwa kila inyapo mvua wakimbilia bwawani
Huna nguo za kufua na wala huna sabuni,
nijibu yapate tua maji utayafanyani
Chorus
Chura punguza vituko na wako uhayawani,
umezua sokomoko watu hawaeleni
Ukivunjika mgongo, dawa atakupa nani?
2. Mwenzenu nilikisia ni mlinzi kisimani,
mtu utamzuia maji akiyatamani
Akaja dada Rukia na ndooye mkononi,
chura ukajing`atua ukajitosa pembeni
Chura punguza vituko &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];
3. Chura bora kuamua wende kulima shambani,
mazao kujipatia wende kuuza sokoni
Nguo kujinunulia isitiri maungoni,
au ukitaka ndoa nenda kaoe nyumbani.
Chura punguza vituko &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];
Tuendelee kuburudika kwa raha zetu na tukifurahia na kumshukuru Mungu kuingia mwaka mpya 2012..
Naomba mwenye audio clip, tafadhari atuwekee,
Mbarikiwe sana wapendwa.
Glory to God!!
Hakuna ubishi kuwa huu wimbo ni wa zamani sana na sijui mwaka gani ulitungwa na kuchezwa ila kwa kweli naupenda sana maudhui yake!!
Wakubwa wanasema umejaa mafumbo matupu, anayejua unafumba nini, naomba atujuze.
WIMBO: Chura
ALBUM: Sina hakika
KUNDI: JKT Taarab
MASHAIRI
1. Chura nakuulizia unipe jibu makini,
kwa kila inyapo mvua wakimbilia bwawani
Huna nguo za kufua na wala huna sabuni,
nijibu yapate tua maji utayafanyani
Chorus
Chura punguza vituko na wako uhayawani,
umezua sokomoko watu hawaeleni
Ukivunjika mgongo, dawa atakupa nani?
2. Mwenzenu nilikisia ni mlinzi kisimani,
mtu utamzuia maji akiyatamani
Akaja dada Rukia na ndooye mkononi,
chura ukajing`atua ukajitosa pembeni
Chura punguza vituko &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];
3. Chura bora kuamua wende kulima shambani,
mazao kujipatia wende kuuza sokoni
Nguo kujinunulia isitiri maungoni,
au ukitaka ndoa nenda kaoe nyumbani.
Chura punguza vituko &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];
Tuendelee kuburudika kwa raha zetu na tukifurahia na kumshukuru Mungu kuingia mwaka mpya 2012..
Naomba mwenye audio clip, tafadhari atuwekee,
Mbarikiwe sana wapendwa.
Glory to God!!