Mapinduzi Yaliyoshindwa ya DARUSO 2002/3

Status
Not open for further replies.

CC: Ben Saanane

tehteh so Mary ndio klikuwa Kiduku cha Zitto ? Kumbe kaanza siku nyingi haya mambo.
 
Last edited by a moderator:
0767 533 433

0785 533 433

Alberto

Nakumbuka nlikuwa first year msando ulikuja nkruman na kauli ya bora kuishi siku moja kama simba kuliko ... Pale zitto,kule mary mugulusi,you guys were rocking,please remain good for Tanzanians na hasa upinzan dhidi ya ccm,you were born to influence
 
Duu imenikumbusha mbali sana nakumbuka Alberto alikuwa Speaker na ZZK alikuwa Secretary General!

ZZK alikuwa anatoka FASS! Hata Omary alikuwa ni mbunge toka FASS! Nakumbuka FASS ilikuwa na wabunge wengi kuliko Faculty yeyote!

Hivi Kayombo yupo wapi sasa? Mwenye simu zake pls
 
Nakumbuka nlikuwa first year msando ulikuja nkruman na kauli ya bora kuishi siku moja kama simba kuliko ... Pale zitto,kule mary mugulusi,you guys were rocking,please remain good for Tanzanians na hasa upinzan dhidi ya ccm,you were born to influence

Wee kweli tulikuwa wote! Ahhaaaaaa haa
 
Nakumbuka akina Kervin Njunwa walifukuzwa chuo kwa muda! Duu long tym ago
 
H.C Dk. Kikwete hakuwahi kuwa Rais wa DARUSO

Kipindi munachozungumzia ni chenu na hakikuwahi kuwa na impact yoyote kwa mTZ wa kawaida. Hayo yote musemayo was just part of your student politics commonly geared by money need, sexuality or even blind imitation of life. Then, nini sababu ya kuleta topic kama hii hapa jukwaa la siasa. Au hata JF! is this a forum of lost and found? Do you assume everyone of us to be interested with UD bussiness? wengine hatukusoma hapa nchini na tunaona kama mulikuwa watotot hadi chuo kikuu! pAre you forcing to be something you can't be anymore?

Ktk historia ya nchi hii vipo vipindi viwili tu ambavyo UD ilitikisa nchi kwa leadership na moral reasoning. Ni kipindi cha Kuikataa JKT ya Nyerere na Kipindi cha utawala wa mwinyi yaani DARUSO ya Bw. matiko. Hivi ni vipindi viwili ambavyo siasa ya wanafunzi iligeuka kuwa ni ajenda ya nchi.

Siwakatishi tamaa lakini poleni kwa kudhani kwamba you did your best. Haitoshi na ninachokiona kwa uhakika. Hii siyo topic ya kuleta Jf maana haijawahi kuwa mjadala wa kutamaniwa na wa Tz wengine. Hayo ni yenu.

so, Mod., can you shift this trd to mambo mchanganyiko?
 

Inasaidia kujua tabia ya mtu inashangaza wewe umeshindwa kukonect dots..mkuu hata ule mgomo wa 2001 wa kugomea uchangiaji gharama za elimu.ya juu huukubali?
 
Maybe we should discuss facts and not who went out with who ? Dada wa. FOE

Hahahaa kumbe wewe ni mdada wa FOE? Enzi hizo wadada walikuwa wnanahesabika kule!

Halafu FOE mlikuwa mnaniudhi sana eti mlikuwa hamtaki sie mangwini tosemee kwenye lecture rooms zenu as if mlikuja nazo toka home.

Mlikuwa washenzi mwili mzima, though sie sheria tuliwashikisha adabu siyo kwa kutumia sheria bali kwa kibano cha uhakika mpaka mkaikimbia FOE kwa muda na Luwanga hakutufanya chochote.

Ila mlikuwa mnanifurahisha kila ikifika kipindi cha kufanya mtihani wa DS mlikuwa mnajazana kule ATB na seminar rooms usiku, mkizamia discussions za mangwini, na vikaratasi vyenu vya kubebea nondos.

Siasa za maspana na mangwini zilinifanya niichukie FOE nzima ispokuwa watu wawili tuu. Mmoja ni mama mmoja (secretary) alikuwa anatutaipia papers zetu kwenye kompyuta ya FOE (laptop hazikuwemo enzi hizo). Wa pili ni mangi mmoja pale sehemu ya kula alikuwa ananijazia sahani yangu nipendavyo na nyama za kutosha.

Wengine mlikuwa mnanizingua tuu. Tega sikio mwezi ujao nitaweka uzi wa Mr. Panchi na jinsi alivyosababisha mpaka Levina akaamua kujiua. Yaani wana-FOE kama vile mlikuwa hamjui hata lugha ya kutongozea?
 
..... na mimi nilikuwa UD kipindi hiki ila nilikuwa too busy kubalance academic na ujasilimali hivyo sikushiriki kabisa politics za Daruso..."
Aaaaaaawapi! Wewe utakuwa kati ya wale ambao watu walikuwa wakipanga mkakati wa kuandamana kesho yake unajidai either mama yako yuko Muhimbili au eti unatangulia town tutakukuta huko.

Disaini ya watu hawa walikuwa wanaboa kweli. Mnapanga fresh halafu kesho asubuhi haonekani. Fisi.

...my honest opinion niliwaona wanavugu vugu karibu wote wa Daruso kama vi puppets fulani hivi, huku wengine wakiitumia Daruso kuganga njaa.

Inawezekana maana enzi hizo ulikuwa unakuta mtu ana cheo Daruso halafu wakati huo huo ni mwajiriwa wa Usalama wa Taifa.

Wakati huo watu walikuwa wasiri kwenye mikakati na njia pekee kwa watawala kupata inside information ilikuwa ni kupandikiza informers wao huko.

Sidhani kama bado wanafanya hivyo tena maana kwanza malalamiko mengi are personal (pesa za kujikimu) na pili siku hizi watu wako tayari kumwaga siri kwa buku kadhaa tuu.

Hard to trust people nowadays.
 
...guys,may I know a little bit about Introduction of HELSB during your university era!? And the trip to SA!?

HELSB is very new to me na sijui hata inafanyaje kazi. Ila post yangu inayofuata hapo chini itakupa some background.
 
lakini hebu tafakari, kundi lile la udsm kipindi kile kuanzia kunji la 2001 hadi 2005, ndilo linalo drive mapambano ya mabadiliko tz kwa sasa.

Agreed lakini pia inawezekana waliopita UDSM kabla ya hapo ndiyo waliopigania mazingira kuendesha hayo mapambano ya mabadiliko sasa. Wengine tumezeeka na kuwa wazee wa busara tuu, wengine ni marehemu kwa sasa na wengine wameamua kuachana kabisa na siasa kutokana na misukosuko waliyokumbana wakati ule wa mfumo wa chama kimoja.

Kama alivyosema David Djumbe, "changamoto zinazojitokeza wakati wa uongozi vyuoni huwa ni mtihani sana na ndio maana wale wanaomaliza migogoro hiyo vizuri huwapa ujasiri zaidi na hatimaye wengi wao huweza kuwa viongozi wazuri...lakini wale wanaoumizwa na changamoto hizo wengi hukosa ujasiri wa kuongoza tena na hivyo kupotea kabisa kwenye siasa..."

Kuna mpaka wengine walishawahi kuwa Rais wa Duruso kwa siku tatu tuu kabla ya kufukuzwa chuo. Cheki hii post ya Kashaijabutege, "Jasson Kishozi (RIP) alikuwa Rais wa DARUSO (Overall-Mlimani na Muhimbili) kwa kipindi cha siku tatu 6-9 Februari 1992. Alifukuzwa Chuo Kikuu na wenzake 9 ambao walisimama kidete kupinga mfumo mbovu wa uchangiaji wa gharama za elimu ya juu na kutetea uanzishwaji wa vyama vingi. Wanafunzi hao 10 walifukuzwa tarehe 10 Februari 1992. Waliofukuzwa tarehe hiyo ni hawa:

1. Mh. James Mbatia (Electrical Engineering-4th year)-Mwenyekiti NCCR-Mageuzi
2. Dr. Harun Kimaro (MD 5th year)-Marehemu (Alikuwa mshauri wa MDC Zimbabwe)
3. Fabian Lutalemwa (Pharmarcy 4th year)
4. Rwekamwa Rweikiza (B.com Marketing-2nd year)-Alikuwa Rais wa Daruso Mlimani siku 3.
5. Idrissa Alnoor Ruta (Engineering Civil 4th year)-Mrehemu
6. Ludovick Kashaju Bazigiza (BA Ed 4th year)-Marehemu
7. Mosena Nyambabe (Engineering-Civil)
8. Dr. Kelivin Mmari (Electrical Engineering-2nd yr)-Ni lecturer wa IT Oregon University, USA
9. Jasson Kaishozi (BA Ed-2nd yr)-Marehemu
10.......Kimweri (BA Economics 3rd year)-Marehemu

Baada ya kufukuzwa Kaishozi alikaa mtaani na baada ya miaka mitano alirudi kusoma sheria [inasemekana baada ya Generali Ulimwengu kumwombea kwa Prof. Luwanga na Luwanga kumkubali on the condition kuwa hatajihusisha tena na siasa za chuo]. Alipomaliza alipata kazi kwenye ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, kama wakili wa serikali. Kesi iliyompa umaarufu ni ile ya ZOMBE, ambapo yeye ndiye alikuwa mkuu wa jopo upande wa mashitaka (serikali)."

Chanzo: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/87973-ulimjuaje-marehemu-jasson-kaishozi-wakili-kesi-ya-zombe.html
.

Kwenye uzi huo huo, Tiba nae anaongezea,

 
huyu Omary Lyas ni nani?
usaliti wa zitto upo damuni
Kuna uzi uliwekwa humu na Waberoya, "Esoteric: Uhusiano wa Zitto, JK, Salim AS, Ridhiwan, Omar Ilyas..." Japo ulifungwa, ukiupitia waweza pata picha halisi ya hawa waungwana.
 

Mortality kwenye hilo kundi la watu 10 imenitisha kabisa. Nusu yao ni marehemu. Mazingira ya vifo vyao yalikuwaje?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…