Maybe we should discuss facts and not who went out with who ? Dada wa. FOE
Hii chai yako haijakaa vizuri umetia sukari sna wewe hauna uwezo huo; we ni mtu wa wanawake inasemekana ulikuwa Biz na mtoto mmoja wa Kike Mkerewe babae akiwa Lecturer UDSM; sidhani kama unaweza kuwa robo ya Omary na Chembe ya Zitto Zuberi, alafu mbona una ID Mbili humu katika hii story??!!!!!
Wazee ninapoisoma thread hii, ndio nafunguka macho na kujisikia vibaya sana kwa vile na mimi nilikuwa UD kipindi hiki ila nilikuwa too busy kubalance academic na ujasilimali hivyo sikushiriki kabisa politics za Daruso, my honest opinion niliwaona wanavugu vugu karibu wote wa Daruso kama vi puppets fulani hivi, huku wengine wakiitumia Daruso kuganga njaa.Nakumbuka wakati niko Mlimani, mwaka 2002/3 kulitokea Mapinduzi yalishindwa dhidi ya Serikali Halali ya Wanachuo iliyokuwa chini ya Rais Francis Kayombo! <br />
<br />
Najiulizaga what was the Motive Behind that mapinduzi na nani waliokuwa Nyuma ya yale Mapinduzi(Ambayo hata hivyo hayakufanikiwa)? Mkuu Waberoya nadhani ulikuwamo katika ile Serikali iliyokoswa koswa kupindulia naomba unitoe Kizani
Maybe we should discuss facts and not who went out with who ? Dada wa. FOE
Hii chai yako haijakaa vizuri umetia sukari sna wewe hauna uwezo huo; we ni mtu wa wanawake inasemekana ulikuwa Biz na mtoto mmoja wa Kike Mkerewe babae akiwa Lecturer UDSM; sidhani kama unaweza kuwa robo ya Omary na Chembe ya Zitto Zuberi, alafu mbona una ID Mbili humu katika hii story??!!!!!
sikumbuki kutaka kujilinganisha na Omary wala Zitto. Na sihitaji kuwa hata robo ya Omary au chembe ya Zitto. Ni mjadala ambao hauna tija. Ingekuwa rahisi ukianzisha thread yako ya "Albert ni mtu wa wanawake na alikuwa anatoka na Mkerewe ambaye baba yake alikuwa Lecturer".
sina tatizo na maoni yako kwa sababu ni kweli sichukii wanawake hata kidogo.
wakati namaliza maelezo yangu niliandika kwamba wengine wanaweza kusahihisha nilipokosea kwa kumbukumbu au vinginevyo. Unaweza kusahihisha pale nilipokosea. Ni haki yako.
Historia ni nzuri sana. Nadhani wale tulioshiriki siasa za DARUSO tuandike ili kuweka kumbukumbu. Hata hivyo, mapinduzi yale mimi sikushiriki. Nilisimamishwa masomo kwa kudhani tu kuwa Zitto alishiriki.
LOL! Alberto Msando you never cease to amaze me! jibu lako lina maana pana sana, kwa kifupi umejibu vizuri sana
Kuna kijana alikuwa anaitwa Msando kwa sasa sijui yupo wapi. Huyo ndo anaweza kutupatia kilichojiri
In our days wazee wa. FOE lazima upige kura ! Na unasaini kabisaa..hiyo ni 2000 wakati wa Kitila Mkumbo..not sure kama ndio alikuwa presdaa ama vipi?..however personnaly sioni kama a good freedom fighter can be the best kupewa wizara au urais..have watched my share of trade union leaders getting posns and fail..so do the freedom fighters they are needed to get the revolution on bt then step out watching trouble makers..not running the show!
Nilikuwepo siku hiyo wakati nikisoma degree ya kwanza. Nakumbuka aliyetangaza rasmi kuwa Kayombo amepinduliwa ni James Zotto pale Rodney Square na si Msando. Zotto kwa sasa ni Mhadhiri Msaidizi Idara ya Historia na Akilojia pale Mlimani. Kilichofuata katika orodha ya waloisimamishwa masomo baada ya mapinduzi hayo Zotto alikuwemo. Hivyo aliyefanya mapinduzi ni Zotto na si A. Msando. I know zotto si mtu muongeaji sana ila ni mtu anayependa kusema ukweli na hataki kuburuzwa. Masele-PhD candidate Univesrsity of Alberta Canada
I am happy also you think highly of Zitto and Omary who remain my friends. i do the same even if in few occasions I get irky for some things done or said by them. That is what confirms a friendship, the ability to remain friends in disagreements. I will reiterate that I never would try to be them or like them, we both have different paths to take.
Remain blessed.
Mapinduzi yamekuwa yakitokea Mlimani karibu miaka yote hasa kuanzia miaka ya 1990s mwanzoni. Nimekuwepo pale miaka ya 1990s katikati mpaka karibu na mwisho. Kuna sababu mbili: 1. ni pale serikali iliyochaguliwa na wanafunzi na kuonekana mwiba kwa utawala kununukiwa na utawala baada ya muda kama miezi sita na kushindwa kuwatumikia wanafunzi na kuegemea utawala, 2. ni pale kundi fulani la wanafunzi lilowania uongozi kwa maslahi binafsi na kukosa ridhaa ya kuongoza ufanya mbinu za mapinduzi ili waweze kula bure pale DARUSO bar, kupata mahitaji karibu bure kama accommodation.
Ndio maana kulikuwa na chombo muhimu sana kilichokuwa kinashikisha adabu utawala, ma-lecturer, serikali ya DARUSO, serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wanafunzi wote, wasaliti na mambo yote yahusuyo maadili ya Kitanzania - chombo hiki kilikuwa kinaiitwa Mzee Punch na logo yake ilikuwa hiyo hapo chini.
View attachment 18612
Hii kitu ilimfanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi atoe machozi baada ya kuchorwa akiwa mtupu!
Usaliti uko kwenye damu zao.Wewe mchokozi sana, mapinduzi yaliongozwa na akina Zitto, Ridhwan Kikwete, A.Msando na Omary Lyas
walikuwa wanasema tulishinda kijanja kijanja na hawakuwa na imani na ushindi wetu.
Kumbuka kabla ya Kayombo alikuwepo Rugemarila na kabla ya Ruge alikuwapo injinia mmoja, the war was engineers will never take over the DARUSO again!
Vita baridi au upinzani wa wahandisi na wasio wahandisi ( ambao tulikuwa tunawaita Mangwin) umekuwapo pale miaka mingi sana. cha ajabu hii vita iko mpaka level ya admistartion ya chuo.Utakumbuka walimu wa sociology, lawasa, FASS, Political science huwa hawapendi kabisa kuongozwa na wahandisi, na hii Luhanga alipata shida sana, mpaka kuliwa kichwa wakati anafanya degree ya sheria!
Leo hii Mkandala anafanya madudu hutawasikia wahadhiri wasio wahandisi wakipiga kelele sana!!...ni 'wao'
Back to the maada:
Nilikuwapo wakati kura zinahesabiwa za urais wa Kayombo, sikuona mchezo mchafu. Ila Ruge alimpa shavu Kayombo na hii ikawahudhi baadhi ya watu. na Ruge ndiye aliyesaini mikataba ya bodi ya mikopo hii watu wanayolia leo, sasa hii ikafanya hata Kayombo aliyekuwa supported na Ruge kuonekana kuwa atafuata nyayo zake tu! sasa hii sababu changanya na ule upinzani wa jadi wa maininjia na mangwin basi hapakukalika. Zitto akaenda kutokea bungeni na kuwa kuliongoza bunge la wanafunzi ambapo kupitishwa kwa mawaziri kulikuwa kasheshe pia.
Kayombo ni mhandisi yuko kiwanda cha chai Iringa nadhani ina future ana mpango agombee ubunge kule sijajua kwa chama gani
It was good days, memorable and from that generation today we have good politicians, I mean watu wanaojua siasa sio biashara, ukijua siasa tamu sana unaweza ukawapelekesha watu unavyotaka , na siasa ni hatari sana kama unapata viognozi wenye kujali maslahi yao, basi unaweza ukawapumbaza watu. Personally nimefanya kazi na Zito na Omar Lyas, Kizuri cha zito ambacho huwa nampa shavu, huwa anaquality ya kuangalia mbaaali sana, hili sina wasiwasi naye. Ridhwan nilijua tu alikuwa maneno mengi na misimamo, kama ya akina Zitto na nikajua labda atakuwa kiongozi mzuri, sijaona bado!! A. Msando is another 'animal' in politics sijui yuko wapi.
Our tactic of ushindi ilikuwa kila second year engineering anaenda na watu wawili kupiga kura, tukaenda kuwabembeleza sociology (you know) na haikuwa shida kwa B.com kuwa upande wetu... ule uchaguzi ushindi haukuwa rahisi, lakini kura hazikuchakachuliwa, ILIKUWA TU NI MBINU YA waliotaka kupindua kujitetea katika hilo. HALI ILIKUWA TETE
Marehemu Chachage ndio alituita kundi la serikali na wale waliotaka kutupindua kutusuluhisha na kuweka mambo asawa atleast. Ukweli Kayombo alikuwa na support ya administration si kwa ubaya.
Siyo siri, DARUSO inasaidia sana ku-shape viongozi, kinachotia uchungu viongozi wengi waliopitia DARUSO wako CCM na unajua what is happening there...ufisadi tu
kwani umekumbuka nini mkuu?