WISTON MWINUKA
Member
- Apr 29, 2012
- 81
- 4
Habari ndugu zangu wana JF!Leo naomba kwa pamoja tujadili juu ya mstakabari wa taifa letu hususani katika suala la amani na uwepo wa CCM,...Viongozi wa nchi mbalimbali barani Afrika na vyama vyao mashuhuri wameangushwa kwa kile kinachodaiwa kuwa ni ukosekani wa haki na maendeleo kwa wananchi pamoja na kutotimizwa kwa ahadi kedekede walizo ahidiwa,Angalia pale Libya,Tunisia,Misri,syria,Ivory coast,na kwingineko ambako waafrika waliamua kuchukua jukumu la kuirudisha amani yao iliyopotea,kila mtu ameshuhudia madhara yaliyotokana na uzembe tu pamoja na kiburi cha viongozi.Ikumbukwe tu kwamba viongozi waliopinduliwa walieshimika saana nchini mwao na katika bara la Afrika,mfano:Gaddafi aliaminika kuwa mkombozi wa Libya,haya leo yuko wapi?...Ikiwa mti mbichi watendewa hivi vipi kwa mti mkavu?....Je! CCM inaamini itatawala milele?kama sivyo ni nini Je CCM imejifunza?...Nawasilisha.