Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,186
- 10,924
Ikiwa ni siku ya 110,zaidi ya miezi 3 tangu vita vianze mapigano makali yameripotiwa kwenye mpaka wa Israel na Gaza na kupelekea Israel kuamua kurudisha baadhi ya vikosi ilivyokuwa imeviondoa kaskazini ya Gaza.
Katika mapigano ya jana Hamas ilifanikiwa kurusha makombora kadhaa kulenga maeneo ya kusini ya Israel jambo lililoishangaza jeshi hilo la IDF.Baadhi ya makombora hayo yalidakwa na mfumo wa Iron Dome wa Israel.
Kwa upande mwengine Israel imefikia makubaliano mapya kati yake na Hamas kuhusiana na upelekwaji wa misaada maeneo tofauti ya Gaza.
Katika makubaliano hayo yaliyosimamiwa na Qattar na Ufaransa sharti kubwa la Israel ni kwamba misaada hiyo iwafikie mateka ambao bado wanashikiliwa na Hamas.
Katika mapigano ya jana Hamas ilifanikiwa kurusha makombora kadhaa kulenga maeneo ya kusini ya Israel jambo lililoishangaza jeshi hilo la IDF.Baadhi ya makombora hayo yalidakwa na mfumo wa Iron Dome wa Israel.
Kwa upande mwengine Israel imefikia makubaliano mapya kati yake na Hamas kuhusiana na upelekwaji wa misaada maeneo tofauti ya Gaza.
Katika makubaliano hayo yaliyosimamiwa na Qattar na Ufaransa sharti kubwa la Israel ni kwamba misaada hiyo iwafikie mateka ambao bado wanashikiliwa na Hamas.