Mapenzi yanavyozidi kuangamiza vijana

Mapenzi yanavyozidi kuangamiza vijana

KATAA NDOA
NDOA NI UTAPELI, NDOA NI VITA, NDOA NI UBATILI MTUPU.

KATAA KABISA NDOA, OKOA AFYA YAKO YA AKILI, KIBUNDA CHAKO NA UHAI WAKO
umeambiwa ni wapenzi we unang'ang'ana na ndoa. Ungesema kataa mapenzi ungeeleweka
 
Ngono usipokuwa Makin lazima ikutoe katika game mzee babycareb dronedrake anaweza kuonekana mshindi maana ni Bora di libolo ivunjike kuliko kunichoma visu vikali . Vya tumbo .
 
Ukweli sasa hivi suala la mapenzi limepotea kabisa hasa kwa wanawake.

Wanaume tunaumia sana kwenye mapenzi sababu utakuta unatoa mali zako, muda wako still bado kuimbe hicho hicho hakijali hakiridhiki mwishowe kwa wanaume wenye roho nyepesi wanaamua kuua au kujiua.

Mapenzi ya siku hizi hayajalishi unapesa au laah yatakutesa vile ulivyo na vile ulivyoingia..

Unaweza usiteswe na mapenzi. Wanzoni yakakutesa unafamilia na watoto au yakakutesa umeshaanza kukata nguvu.

Mwanamke atakubadirikia kama hakujui na watoto nao wakafata ya mama yao. Hapo ndipo utaiona dunia chungu umejitoa kwa kila kitu badaye hakuna anayekujali na umri ndo huo.

Au mwanamke akuroge ufe. Yaan ni tabu tupu.

MUNGU WATAZAME Hawa viumbe wa kiume. Wanamengi moyoni.
Tuishi nao kwa akili, tukiendekeza hisia tumeisha
 
Sema de libolo kama asemavyo mkuu wa hizi kazi Mzee wakupambania unabidi de libolo uipatie chakula kiasi
 
Mapenzi Mapenzi Mapenzi nakuita mara tatu
Bora wakina sie Single, Singular na Singwengwe
 
_20230918_233430.JPG
 
Kwamba kajichoma kisu tumboni yeye mwenyewe halafu akapiga kelele za kuomba msaada, kifo hakijaribiwi, ukijaribu unakufa.
 
Komaa na uanaume wako wa kubeba vitu ambavyo habibebeki. Hatimaye hakuna la maana

Sijalia na sitolia tunazungumzia uhalisia.
Wewe umetaka kuonewa huruma na ndio kulia kwenyewe huko.

Mwanaume ni problem solver, sasa wewe unalia namna hiyo mkeo afanyaje?
 
Ukosahihi sana, wanawake hawajali kabisa, k wanagawa free tu, suala la hatuwafikishi kileleni ni upumbafu wao tu. Tunahangaika kutafuta kibunda tuyahidumie lakini hayajali kabisa. Wanaume tunateseka sana, wivu haukwepeki ukupenda
Bado hoja inakuja sasa huyo kiumbe anachepuka na nani? Kama sio mwanaume mwenzio kwaio Mimi navyo jua uharibifu usha ingia kotekote. Maana unapo salitiwa na mkeo kumbuka yupo mme wa mtu kasaliti mkewe kaja kwa mkeo. Mungu atusaidie
 
Bado hoja inakuja sasa huyo kiumbe anachepuka na nani? Kama sio mwanaume mwenzio kwaio Mimi navyo jua uharibifu usha ingia kotekote. Maana unapo salitiwa na mkeo kumbuka yupo mme wa mtu kasaliti mkewe kaja kwa mkeo. Mungu atusaidie
Uko sahihi, ila mwanamke ndio anatongozwa, na yanajirahisisha, hayakatai
 
Tukiwakataza vijana wasichukulie mapenzi serious hawaelewi.

Huko Dodoma kijana mmoja kamchinja mpenzi wake na kisha kujichoma kisu tumboni na kufariki sababu ikiwa ni wivu wa mapenzi.

Kijana alivyo mpumbavu ameshajichoma kisu utumbo uko nje akaanza kupiga kelele kuomba msaada wa kupelekwa hospitali.

Vijana acheni kuchukulia mapenzi serious kiasi hicho. Mwanaume achana na mambo ya kupenda.

=====

Mama mzazi wa marehemu Esther, Rachel Izengo amesema jina la mtoto wake ni Esther Ramadhani Isugilo na siyo Samira Mathias ambalo lilizoeleka mtaani.

Esther amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumatatu Septemba 18, 2023 kwa madai ya kuchinjwa na mpenzi wake aliyefahamika kwa jina moja la Amos.

Mapema leo asubuhi mmliki wa nyumba aliyokuwa amepanga Esther ambako kulifanyika mauaji hayo, Yohana Nhembelo alisema ndugu wameomba chumba kilichofanyika kisifanyiwe usafi hadi watakapofika na kukiangalia.

Amesema amepata taarifa ya kifo cha mtoto wake kupitia kwa majirani saa 10.00 usiku wa kuamkia leo akiwa mkoani Shinyanga ambako ndiko anakoishi.

Amesema alianza safari muda huo na kufika jijini Dodoma saa 8:00 leo ili kujua sababu ya kifo cha binti yake ambaye ni mtoto wa kwanza kati ya watoto watatu alionao.

“Nimesikitishwa sana na kifo cha mwanangu cha kuchinjwa kwa sababu ni kifungua mimba na sikutarajia kama atakufa kwa kifo kama hiki. Binti yangu alikuwa ni mtu wa watu,”amesema huku akiangua kilio baada ya kushuhudia chumba kichofanyika mauaji hayo.

Ndugu wa marehemu wamesema baada ya kuangalia hali ya mwili wa mtoto wao ndipo watafanya uamuzi wazike wapi.

Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Martin Otieno amesema kuwa chanzo cha mauaji ya wapenzi hao waliokutwa wamefariki dunia usiku wa kuamkia ni wivu wa mapenzi.

Kamanda huyo amesema mwanaume aliyejulikana kwa jina moja la Amos alimchoma kisu maeneo ya shingoni Esther maeneo ya shingoni kama mara tatu na kupelekea koromeo kutoka nje na akawa amemchoma kwenye mkono begani kisha yeye kujichoma kisu kwenye kitovu na kupelekea utumbo wote kutoka nje.

(Imeandikwa na Sharon Sauwa)
Vijana acheni kuchukulia mapenzi serious kiasi hicho. Mwanaume achana na mambo ya kupenda

Omba sana Mungu yasikukute..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom