Mapenzi yanaumiza...

Itovanilo

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2018
Posts
2,310
Reaction score
5,157
MUNGU umeumba vitu vyote kwenye ulimwengu huu,ukavitakasa na ku vibariki lakini Kati ya viumbe vyako vyote,kuna huyu kiumbe bin Adam, ulimuumba kwa namna ya pekee kabisa,

Kuanzia body appearance nikimaanisha utendaji kazi wa viungo vyote pamoja na kumpa akili na maarifa. Pamoja na yote hayo,ipo namna ambayo MUNGU umempa upendeleo kwa kila kitu,mfano:kwenye mapenzi binadamu ana enjoy kila sehemu kuanzia kutongoza kwenyewe, romance na hata tendo lenyewe.sijajua kuhusu wanyama na ndege wanafaidi vipi,kwakuwa Mimi siyo zoologist,ila naamini sisi tumezidi kwakuwa tuna akili na utashi.

Lakini mbona mapenzi yanaumiza sana? yaani hata Mimi, lahaulaaaah! Mwenyezi MUNGU kwani ile adhabu ya like kosa pale bustanini bado tunaitumikia Hadi leo?

Hakika mapenzi yanaumiza,acha yaue watu,acha watu wakufuru,acha mtu ajute kuzaliwa? mapenzi kweli ni sumu,ee mwenyezi MUNGU Kama kila unachompa mja wako huwa unagawa kwa asilimia basi kwangu isomeke hivi, 0.00001 ili asilimia zilizobaki unijalie mambo mengine.

Yaani hata Mimi, sikufikiria hiki kitu kitani. Mwenye nyimbo ya bwana mdogo Belle 9 iitwayo sumu ya penzi aiweke hapa
 
Ushauri wangu kwako
Tafuta pesa
Pili, tafuta pesa
Tatu, wewe endelea kutafuta pesa

Utakuja kunishukuru baadae

Ila pole mkuu, ni kweli inauma sana, ila ndio hivyo huna budi kukubaliana na matokea sasa

Hapo utakuta umeachwa kwa nyodo sana, daah, inauma kweli

Hata hivyo kila mtu ana changamoto zake mkuu, hatuna budi kufarijiana na kuendelea kuishi

Hata iweje maisha lazima yaendeleee
 
Ukitaka mwanamke akung'ang'anie na kukupenda kwa dhati;
1. Mpe surprise za upendo kadri muda unavyokuruhusu.
2. Usimsimange/ usiwe na gubu kwake.
3. Mwambie ukweli pale unaposhindwa kumtimizia kile anachoomba.
4. Muombe msamaha haraka pale utakapokua umemkosea.

Mbali ya hapo ndio huja hizo kauli za " mapenzi huumiza ".
 
Sawa mkuu,ila pesa siyo kila kitu tena pesa siyo vijisenti
 
Ahsante mkuu,waweza kuwa navyo vyote ila ukashindwa kuzitambua kanuni
 
Mimi napiga tu nyeto hayo mapenzi nimewaachia nyie.
 
Ni kweli, lakni ni vyema ukawa nazo
Pesa hainunui msamaha, Wala haitengenezi thamani ya moyo ila inatengeneza thamani ya mwili,

ndiyo maana unaweza sema unapendwa kumbe siyo,Bali unatimiza mahitaji ya mtu.

Kama hakuwa na nyumba atajenga.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…