DungaMawe
JF-Expert Member
- Jul 31, 2022
- 1,461
- 4,409
Ashura ni nini ulitaka kutoka kwangu sikukupa, japo sikuwa na kazi ya kueleweka lakini nilipambana kwa ajili yako na mtoto wetu huku nikijipa moyo wanaume tumeumbwa kuteseka, licha ya magumu yote niliamini ipo siku Mungu ataniona.
Ooh, lakini imekuwa tofauti kwangu kumbe hata mtoto uliyesema ni wangu Ashura umenidanganya umezaa na mtu mwingine, bora angekuwa ni mtu wa mbali kumbe ni kaka yangu wa damu na sasa mnapanga mniroge niwe kichaa.
Ashura ahadi zote ulizonipa kumbe ulikuwa ukinilaghai, kumbe mwenzangu kwa kushirikiana na kaka yangu mlipanga kunimaliza na hata kile kidogo nilichokuwa nacho mnataka kukichukua.
Ashura siamini kama ni wewe ndio umekuja kuwa hivi, lakini mimi ndio nilikuwa mpumbavu, walimwengu waliambia kuhusu wewe sasa nitaficha wapi uso wangu mimi!
NI BORA NIFE TU NIKAMPUNZIKE KULIKO KUISHI KWENYE HII DUNIA ILIYOJAA MATESO.
Kwaherini wana JF tutaonana mbinguni kwa Baba.
Ooh, lakini imekuwa tofauti kwangu kumbe hata mtoto uliyesema ni wangu Ashura umenidanganya umezaa na mtu mwingine, bora angekuwa ni mtu wa mbali kumbe ni kaka yangu wa damu na sasa mnapanga mniroge niwe kichaa.
Ashura ahadi zote ulizonipa kumbe ulikuwa ukinilaghai, kumbe mwenzangu kwa kushirikiana na kaka yangu mlipanga kunimaliza na hata kile kidogo nilichokuwa nacho mnataka kukichukua.
Ashura siamini kama ni wewe ndio umekuja kuwa hivi, lakini mimi ndio nilikuwa mpumbavu, walimwengu waliambia kuhusu wewe sasa nitaficha wapi uso wangu mimi!
NI BORA NIFE TU NIKAMPUNZIKE KULIKO KUISHI KWENYE HII DUNIA ILIYOJAA MATESO.
Kwaherini wana JF tutaonana mbinguni kwa Baba.