Vizuri sana, hivyo tunakubaliana kabisa kwamba nyinyi wanawake wa kizazi hiki suala la uvumilivu halipo na ni ma opportunist, maana mwanaume akiwa chini yako hasa kiuchumi huyo unamuona hafai, yaani pamoja na kuletewa mfumo wa maisha ambao umewapa nafasi sawa na wanaume ya kunufaika karibu kwenye kila kitu na nyie mkaukumbatia lakini bado mnataka kuishi na wanaume ambao wamewapiga gap kiasi fulani kwenye nyanja kadhaa za kimaisha... mnataka nini hasa au wanaume wa sayari gana hasa? Tusisingizie nature kila muda, hata nature kuna muda inatutaka tuchanganye na akili kidogo kama ambavyo tumechanganya na kuamua kumpa elimu na fursa za kushikilia uchumi mwanamke.
Hapa bila kutumia akili nyinyi wanawake ndio mnajikuta kwenye losing side. Ukifuata hiyo misingi eti mwanaume lazima anizidi kila kitu ndio ana qualify kuwa mume wangu, mwisho wa siku unajikuta una options chache sana za hao wanaume, maana kadri mmavyozidi kujiendeleza kielimu,kiuchumi vile vile pia unapunguza idadi ya wanaume wenye qualifications zenu na hatimae kukosa kabisa.
Kiutamaduni,kiiimani na kijamii regardless wakati uliopo,mwanaume ndio anatakiwa kujiandaa kimaisha angalau hata msingi tu halafu ndio aje aungane na binti ambaye bado yuko kwenye zero wanyanyue huo msingi wote kwa pamoja huku mwanaume ndio akiwa kiongozi. Mahusiano/ndoa nyingi zenye afya wahusika wanakuwaga wamepita huku.
Mkishakutana wote wawili kila mtu amesha jiestablish kiuchumi sio kitu kibaya, lakini fahamu tu hapo hapatakuwepo na mwanamke bali wote ni wanaume tofauti yenu ni jinsia tu. Maana kabla ya kukutana kila mtu kafanya maandalizi ambayo kikawaida yapaswa yafanywe na mwanaume, hapo ni nadra sana kuwepo na nidhamu ya mume na mke alkadharika pia pepo la ubinafsi lazima liwaandame na hayo mahusiano/ndoa hayatakuwa na furaha ya kweli.
Lets put it buntly for any marriage to be frabjous,blissful,peaceful and bed of roses a wife should at least be dependent on her husband, contrary to that we will always have this kind of discussion over and over.. over
Suala la ku start from the bottom ni jema sana lakini kwa kizazi hiki kutokan na mporomoko wa maadili pamoja na matango poli tunayolishana linaonekana limepitwa na wakati, lakini nakuhakikishia kwa watu ambao bado wanalifuata katika kujenga mahusiano yao wanayafurahia maisha.
Unajua hakuna furaha kama kutumia kitu ambacho unafahamu kabisa jinsi kilivyopatikana? yaani ulikwepo kabisa tangu siku ya kwanza kinatafutwa na unakitumia kwa uhuru na kwa kujiamini!
Binafsi sishauri mtu yoyote asomeshe mchumba fanya hivyo akiwa tayari ni mke wako, alkadharika pia kwa mwanamke sishauri aweke uvumilivu kwa mtu ambaye bado hawajawa pamoja kihalali.
Majority of ladies who get married while they’re already financially stable are just in need of upgrading their social status and bearing legitimate babies. They are too far from upholding feminine features in their marriages.
Kama ni tabia ya mtu basi wanawake wengi mnafanana tabia!
Hili sula la women empowerment kwa kweli limekuja kutuvurugia kabisa mfumo mzuri wa maisha ambao umepewa baraka kutoka kwa MUNGU tangu mwanzo wa hii dunia.Ni bahati mbaya sana huu mfumo mpyaa umewalenga zaidi wanawake na kuwasahau wanaume, matokeo yake tumejikuta sisi wanaume tukiishi kwa kufuata misingi ya kale wakati wanawake wao wamebadilika. Unaona sasa hapo panapokuja kuleta mvurugano, ila sema nini huu mfumo wa maisha mpya unaenda kufeli vibaya sana na waathirika wakuu ni wanawake.
feminism/women empowerment imewharibu sana wanawake imewatengeneza kuwa wanaume, ni ngumu mno kumpata mke ambaye tayari akili yake iko crippled na mfumo huu.
Ukiyashirikia hayo mawazo utafeli na ndoa itakushinda hasubui sana, wewe hautakiwi kuwa mtu wa visasi na visasi vyenyewe eti unasubiria wakati wa matatizo kwa mume wako!! Labda nikukumbushe tu wewe mwanamke ndio mlinzi mkuu wa ndoa yako kuliko hata mume wako, sasa tatizo likitokea kwenye ndoa yako na wewe ukakitumia hilo tatizo kwa ajiri ya kujipa ahueni ya mambo yaliyowahi kutokea huko nyuma na hayakukupendeza halo unakuwa umepoteza maana nzima ya kuwa mke