KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,213
- 56,850
Zama za leo wanaume tumekuwa tukilalamika kukosekana kwa mapenzi halisi toka kwa wanawake! Ni dhahiri zama zimebadilika,ule upendo halisi umefifia Ila haujapotea!. Kilichopotea ni kile ambacho hakipo kabisa! na kilichofifia ni kile kipo Ila kwa uchache.
Hatuwezi kuzungumzia mapenzi bila kuiweka pesa! Ndio mapenzi bila pesa hayaendi kwani tafsiri ya pesa imebeba mahitaji yetu. Yenyewe ndio kinunuzi cha mahitaji yetu na huduma tuzitakazo. Mapenzi bila mahitaji ni sawa na mshumaa uulazimishe uwake pasipo na oksijeni!!.
Pesa imekuja kufubaza mapenzi halisi toka kwa viumbe hawa watamu.. kupenda imekuwa ni kwa kufuata mahitaji kuliko mapenzi, ndio wanahitaji kusurvive ndio maana wanafuata wanapoweza kusurvive!.
Mapenzi halisi ni kupenda sifa za mtu husika ama kimuonekano, kiutendaji n.k. Unaweza kuwa na kanuni zako za kutaka mtu kwa sifa uzitakazo lakini hisia zikaanguka kwa mtu mwenye sifa mbili tu kati ya kumi uzitakazo!.
Kupenda hakupangiwi, kupenda hakutajiwi.. kupenda kupo tu natural.
Kwa wepesi mada yangu inazungumzia kauli hii "Sometimes don't chase a woman they'll chase you"
Kuna vitu tunahitaji kuvifahamu kutoka kwa wanawake ili twende sambamba.. kwanza usije kujidanganya kuwa hakuna upendo halisi!.. kila binadamu anao upendo ila ni vile tu upendo huo unahitaji nini ili ukurupuke huko ulipojificha!..
Upendo halisi kwa hawa viumbe wanawake hauji tu bure!.. vipo vitu unavyotakiwa kuwanavyo ili uweze kulindimisha mawimbi ya upendo ndani ya viumbe hawa tuwapendao.
Ipo hivi wanawake hupenda mtu ambae anajali.. kiumbe hichi ni Kama mtoto,ujali huwa na maana kubwa ndani yao!.. wanaume tusikariri kuwa kutongoza ni lazima tutumie maneno au pesa.
Kutongoza na kupata upendo halisi kunatoka kwenye muonekano,matendo,ujali,uanamme wetu n.k
Viumbe vya kike hupenda kuwa comfortable hasa wakiwa na wawapendao hivyo ni juhudi yako kukifanya kiumbe hicho kuwa comfortable kwako.
Wanawake hupenda mtu mcheshi na serious.. mcheshi kwa maana ya kuwa na furaha awapo nawe na serious kwa maana ya mtu unae focus kwenye malengo na kuyatekeleza.
Mwanamke ni kiumbe kinachohitaji usiri wako na sio mpayukaji mtu usie na koromeo.
Ni dhahiri mwanamke anahitaji kiumbe kitanashati.. ipo hivi wanaume wengi tumekuwa hatujijali kimuonekano hii ni Kama asili yetu..😅
Ni vyema kujali muonekano Kama unahitaji hivi viumbe vikufuate!.. only smartness sio inatosha.
Wanawake wanapenda mtu simple na muelewa. Hizo ni sababu chache tu zinazoweza kuwafanya hao viumbe wapende kiuhalisia.. kwa tafsiri nyengine naweza sema ili we need to be gentleman ili tuweze kuibua mapenzi halisi toka kwa hao viumbe.
Guys let's be a gentleman na sio kila siku kuwa watu wa kulalama.