Mapendekezo ya CCM Uchaguzi wa Serikali za mitaa mwakani

Mapendekezo ya CCM Uchaguzi wa Serikali za mitaa mwakani

Hii ndio taabu ya kuwategemea Usalama kuongoza nchi!!
Mikakati ya kijinga sana sana hii, na itazidi kuivuruga nchi!?
 
Akili iliyoganda, mawazo yake yakasinyaa huanza kutafuta hila na huko nako ndiko kuanguka kwake kunapotokea haraka.
 
Ualimu usiwe kigezo cha kupewa nafasi ya kusimamia uchaguzi. Sifa za mwombaji za kusimamia uchaguzi huo ziwe;
a. Mwombaji awe na angalau elimu ya kidato cha nne au cha sita, pamoja na elimu nyingine yeyote ya cheti au zaidi kutoka katika chuo kinachotambuliwa na serikali
b. Mwombaji awe mfanyakazi mwajiriwa wa kudumu wa serikali
c. Mwombaji awe mkazi wa kijiji/mtaa/kitongoji husika kwa mwaka mmoja au zaidi
d. Mwombaji asiwe kiongozi wa nafasi yeyote katika chama chochote cha siasa

2. Kamati ya kupitia maombi na kuteua wasimamizi iundwe na viongozi wa vyama vyote vya siasa vitakavyoshiriki uchaguzi huo, ngazi ya wilaya

3. Kopi za barua za maombi za waombaji ziwasilishwe na waombaji wenyewe kwenye ofisi zote za kila chama kitakachoshiriki uchaguzi huo, ngazi ya wilaya (kama zipo)
 
Maongezi yenu ya matukio ya kufikirika ambayo mmnayafanya kwenye vijiwe na vilabu vya pombe, msiyalete hapa na kutaka kutuaminisha kama ndiyo mkakati kitaifa.

Mkakati wa kuhujumu uko wapi hapo zaidi ya mapendekezo ya CCM yaliyopelekwa kwenye wizara inayohusika na usimamizi wa serikali za mitaa.MiCHADEMA niya ajabu kweli. Badala ya kupeleka mapendekezo yao, badala yake inaanza kulia lia na kulalamika.

Hizi preemptive reasoning zenu za kujiandaa baada ya kunyolewa kwenye sanduku la kura hata hazitosaidia.

Kuwapa watu muda wa 14 days kujiandikisha badala ya 7 days kwenu ni mkakati wa kuhujumu uchaguzi?. My foot.
Kwanza tunashukuru kwa kuwa mwanaCCM wa kwanza kuja mtandaoni na kukiri kuwa ni kweli kuna kitu kama hichi CCM imeanza kukifanya.
Hii inatupa uhalali wa kujadiri hoja hii pasipo wasiwasi wa kuhisi ni uzushi.

*MASWALI YA MSINGI
1/Toka lini CCM imepeleka mapendekezo ya kisiasa serikalini yakakatariwa?

2/Nini hasa lengo la CCM katika kila pendekezo ililoliandika?

3/Hofu na Wasiwasi wa CCM unatoka wapi katika kipindu hiki wakati siku za nyuma Uchaguzi wa vijiji na vitongoji CCM ilikuwa unashinda tu tena sehemu kubwa bila kupingwa?
 

Narudia tena na tena kusema, hujawahi hata siku moja kuleta kitu cha maana humu jamvini, zaidi ya uzushi na maneno yakusadikika kuliko ukweli halisi. Nawasilisha.
Ukweli inauma sana na hapa naona hoja imekugusa ndio maana umeumia sana.

Acha hasira ndugu, jibu hoja na sio kuropokaropoka.
CCM mmekwisha na mipango yenu za wizi wa kura tumeshaishtukia.
 
Kwanza tunashukuru kwa kuwa mwanaCCM wa kwanza kuja mtandaoni na kukiri kuwa ni kweli kuna kitu kama hichi CCM imeanza kukifanya.
Hii inatupa uhalali wa kujadiri hoja hii pasipo wasiwasi wa kuhisi ni uzushi.

*MASWALI YA MSINGI
1/Toka lini CCM imepeleka mapendekezo ya kisiasa serikalini yakakatariwa?

2/Nini hasa lengo la CCM katika kila pendekezo ililoliandika?

3/Hofu na Wasiwasi wa CCM unatoka wapi katika kipindu hiki wakati siku za nyuma Uchaguzi wa vijiji na vitongoji CCM ilikuwa unashinda tu tena sehemu kubwa bila kupingwa?
Kama unataka tuanze kujadili mapendekezo ya CCM lazima ulete hapa barua yenyewe na siyo hii "barua(waraka?) inayodaiwa iliyonaswa yenye mapendekezo kwa vile barua ya CCM ni tofauti na kilichoandikwa hapa.

Hutuwezi kuanza kujadili quotation za mleta mada na kuzipachika kama ndiyo barua ya CCM.
 
Nasubiria kwa hamu sana matokeo ya Chaguzi mikoa ya Lindi na Mtwara
 
Kama unataka tuanze kujadili mapendekezo ya CCM lazima ulete hapa barua yenyewe na siyo hii "barua(waraka?) inayodaiwa iliyonaswa yenye mapendekezo kwa vile barua ya CCM ni tofauti na kilichoandikwa hapa.

Hutuwezi kuanza kujadili quotation za mleta mada na kuzipachika kama ndiyo barua ya CCM.

Mkuu kwenye post yako umesema haya ndio mapendekezo ya CCM na hujaona tatizo lolote, vipi tena unabadilika?

Okay hizi nukuu sio za kweli, wewe basi tupe hayo mapendekezo ya kweli ya CCM mliyopeleka TAMISEMI na kwa sababu sio siri tunaweza kuyajadili pia hapa, Kinyume na hivyo tujadili cha mleta mada tu.
 
mwanadiwani kama wanatoa maoni si watoe kwa wazi kwanini watoe kisirisir? ilipaswa vyama vyote vikae na vikubaliane. mambo yenye shaka kwa pande mbili yasiinngizwe. c.c.m italeta vita kwa kulazimisha mambo hata yanayoepukika. wadau wanahitaji tume huru ya uchaguzi yenyewe inataka kuwatumiwa ma dc makada wa c.c.m. tunakoenda kubaya lakini lazimi mshitakiwa kimataifa subiri tu amani ivunjike kama mnavyotaka
 
MAPENDEKEZO YANGU KWA CHADEMA
1/Njama hizi za CCM ziwekwe wazi sasa kwa kila mtanzania ili harakati za kuyapinga zianze sasa tena ngazi ya kijiji kupitia wananchi wenyewe kuliko kusubiri mara yatakapoanza kutekelezwa(CHADEMA itumie bunge, mikutano na vyombo vya habari kufikisha ujumbe wa kuyapinga)

2/CHADEMA sasa itoe mapendekezo yake kuhusu uboreshaji wa chaguzi za vijiji na vitongoji na kuyapeleka TAMISEMI na wakati huo huo utueleze sisi wananchi ili tuanze kushinikiza yafanyiwe kazi na sio kusubiri wakati yameshakataliwa.
 
Mkuu kwenye post yako umesema haya ndio mapendekezo ya CCM na hujaona tatizo lolote, vipi tena unabadilika?

Okay hizi nukuu sio za kweli, wewe basi tupe hayo mapendekezo ya kweli ya CCM mliyopeleka TAMISEMI na kwa sababu sio siri tunaweza kuyajadili pia hapa, Kinume na hivyo tujadili cha mleta mada tu.
Toka lini quotation zikawa ni barua?. Are you ok?.

CCM ina taratibu zake za kiutendaji ambapo hii pia inajumuisha mawasiliano kiofisi.

Barua ya CCM haikuwa press release au haikuhusu umma, bali ilikuwa mahsusi kwa wizara inayoshughurika na serikali za mtaa. Kuileta hapa na kuanza kuijadiri siyo tu ni kinyume cha malengo yake bali pia ni kinyume cha taratibu za kiofisi ambazo CCM inazienzi.

CCM siyo CHADEMA.
 
Maongezi yenu ya matukio ya kufikirika ambayo mmnayafanya kwenye vijiwe na vilabu vya pombe, msiyalete hapa na kutaka kutuaminisha kama ndiyo mkakati kitaifa.

Mkakati wa kuhujumu uko wapi hapo zaidi ya mapendekezo ya CCM yaliyopelekwa kwenye wizara inayohusika na usimamizi wa serikali za mitaa.MiCHADEMA niya ajabu kweli. Badala ya kupeleka mapendekezo yao, badala yake inaanza kulia lia na kulalamika.

Hizi preemptive reasoning zenu za kujiandaa baada ya kunyolewa kwenye sanduku la kura hata hazitosaidia.

Kuwapa watu muda wa 14 days kujiandikisha badala ya 7 days kwenu ni mkakati wa kuhujumu uchaguzi?. My foot.

Yani unabishana na barua ya katibu mkuu wako? Sitashangaa siku chama kingine kikiingia ikulu utaendelea kubisha na kusema si kingine kilichopo ikulu bali ni ccm,lkn ni sawa siku hizi magamba hawana hoja hata wkielezwa ukweli wanabisha km yanayotokea mtwala
 
Binafsi nilipata taarifa kama miezi 6 iliyopita kutoka kwa mmoja wa viongozi wakubwa serikalini, ambaye alidai kwamba kulikuwa mkakati batili wa kuarisha uchaguzi wa serikali za mitaa/vijji mwaka 2014 kwa hoja kuwa serikali haina fedha za kutosha za kuuendesha uchaguzi huo. Lengo likiwa ni kuepusha aibu ya ccm kushindwa vijiji vingi na hivyo, kusababisha athari kubwa na mbaya kwenye uchaguzi wa 2015 kwa upande wa CCM.
kwa mujibu wa mtonyaji wangu,tatizo kubwa la mpango huo ni kama serikali itaeleweka kwa wananchi huku wakitarajia vyama vya upinzani kuupinga mpanga huo kwa kusema kuwa ccm wameogopa uchaguzi, kitu ambacho mtoa taarifa wangu anasema kingewaathiri zaidi badala ya kuwasaidia.

Hata hivyo, taarifa ziliandikwa ktk gazeti maarufu kufichua habari nzito nzito la mawio la Kila wiki (kila alhamisi) inayoonesha kuwa, mkakati wa kuahirisha uchaguzi unawatatiza na badala yake gazeti limefichua mikakati kadhaa batili yenye lengo kuhakikisha ccm inashinda uchaguzi huo kwa gharama yo yote. Gazeti lilimuuliza Tundu Lissu kuhusu Mikakati hiyo, naye akakiri kuifahamu vizuri.

Mikakati hiyo ya ccm ni pamoja viongozi wake kuandika kimya kimya barua (waraka?) yenye kumb No CMM/OND/626/VOL.111/44 kwenda ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI wakipendekeza mambo kadhaa ambayo ni dhahiri yanalenga kuhujumu uchaguzi huo. Mapendekezo hayo batili ni kama yafuatavyo;
A) CCM wamependekeza waalimu wasisimamie uchaguzi wa vitongoji na serikali za mitaa/vjiji kwa madai kwamba walimu wana mgogoro na serikali kuhusu maslahi yao.
B) Wamependekeza wananchi waombe nafasi hiyo ya kusimamia uchaguzi kwa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ( yaani mkuu wa wilaya/mkoa) ambaye pia mjumbe wa kamati ya siasa ya ccm ya wilaya/mkoa?
C) CCM wamependekeza udhamini wa wagombea utolewe na viongozi wa ngazi husika – mgombea kitongoji au mtaa/kijiji adhamiwe na viongozi wa chama chake wa ngazi hiyo.
D) CCM pia wamependekeza wasimamizi hao wa uchaguzi wasiwasaidie watu wasiojua kusoma na kuandika badala yake mawakala wa vyama watumike kuwasaidia.
E) CCM wamependekeza muda wa kujiandikisha uwe siku 14 ( siyo 7) na mpiga kura awe amekaa ktk eneo husika kwa muda usiopungua miezi 3.

Gazeti gazeti lilitaka maoni ya CHADEMA kwa Tundu Lissu ambaye alimshauri mwandishi kumtafuta katibu mkuu Dr Slaa kujua msimamo wa CHADEMA. Hata hivyo, Tundu Lissu alipoulizwa kama anajua waraka huo alijibu, tulipokamata nyaraka za akina Asha Rose Migiro, Nape Nnauye, Mwigulu za kuchakachua mchakato wa katiba mpya, vile vile tulikamata mkakati wao wa kuchakachua uchaguzi wa 2014. Tundu Lissu aliendelea kusema, tunajua mipango ya CCM kuhakikisha inashinda uchaguzi wa 2014 hata ikibidi kuchakachua kura. Akaendelea, CHADEMA ni chama kikubwa kaka, tunajua wanchokifanya hatua kwa hatua, wenzetu wamejiandaa kuvuruga uchaguzi wa vitongoji na vijijj.
Kwa mujibu wa gazeti hilo,Tayari katibu mkuu wa TAMISEMI ameshawaandikia barua makatibu wakuu wa vyama vyote akitaka watoe maoni ya kuboresha uchaguzi wa 2014. Hata hivyo, kuombwa kwa maoni hayo, ni mkakati wa maandalizi ya kuchomeka mapendekezo hayo ya ccm kwenye mchakato wa uchaguzi ujao wa serikali vitongoji na mitaa/vijiji.


Maswali ninayojiuliza;
Kitendo cha kutaka wasimamizi wa uchaguzi wa serikali wateuliwe na kada wa ccm kwa jina la mkuu wa wilaya siyo juhudi za wazi wazi za kuhujumu uchaguzi huo? Je, mjumbe wa kamati ya siasa ya ccm wilaya yenye jukumu la kuhakikisha usalama wa ccm kisiasa ataacha kupendelea ccm kwa vile ni mkuu wailaya?

Pili, Kitendo cha ccm kutaka wagombea wadhaminiwe na ngazi husika, siyo kwamba ccm wanatarajia kuwa vyama vya upinzani havina uongozi ktk ngazi ya vijiji na vitongoji? Je huu siyo mkakati wa ccm kutaka kupita bila kupingwa kwa wagombea wa vyama vingine kukosa udhamini? Nadhani wamesahau kuwa CHADEMA iko mpaka ngazi ya vitongoji.

Tatu, Kwa nini ccm wanawakimbia walimu? Je, siyo kwamba CCM inataka uchaguzi huo usimamiwe na wananchi wa kawaida wakati lengo lao ni kuchomeka wanaccm kusimamia uchaguzi huo kupitia kwa kada wa ccm au mkuu wa wilaya ili waipendelee CCM?
Je CHADEMA tunapaswa kufanya nini kama jambo hili litatokea?


Nawasilisha.



Mwisho wa ubaya ni aibu watajaribu kufanya kila aina ya uovu ili mradi washinde lakini hawatafanikiwa kwa kuwa siku zote mpendwa na wengi ni chaguo la mungu na ukimwamini mungu shetani hana nafasi,hawa CCM ni wafuasi wa shetani na hawafanikiwa hata wafanyaje.
 
machozi ya watanzania yanaanza kulenga kwa macho tunapoelekea siasa hizi zitatufanya wengine tufe maskin kwan viongozi midomo imewekwa kwenye maneno na maneno hayajawekwa kwenye vitendo.... Mungu sidia Tz
 
Ccm inataka kuwatumia wajumbe wa kamati za siasa za wilaya na mikoa ili kuwateulia wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani 2014, ili kuilinda ccm! Kinana nimemdharau kwa ufinyu wa mawazo'
 
Back
Top Bottom