Mapendekezo katiba mpya: Tunahitaji makamu wa rais?

mfano km huyu makamu wa raisi w sasa mimi sioni anafanya nini.....kazi kutembea na wake zake mbugani
 
aliopo sasa sijui hata majukumu yake ni yapi hata raisi akiwa amesafiri sioni kama anatoa maamuzi yeyote, kazi yake kuzunguka kula kodi zetu
 
Unaonaje katika Katiba mpya tuwe na Parliamentary system kwa Zanzibar and Tanganyika governments and Presidential system kwa Union Government? Kwa hiyo Mkuu wa Serikali ya Tanganyika awe Waziri Mkuu na atokane na chama chenye Wajumbe wengi katika Baraza la Wawakilishi Tanganyika, Mkuu wa Serikali ya Zanzibar awe Waziri Mkuu wa Zanzibar na atokane na chama chenye Wawakilishi wengi katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Mkuu wa Nchi awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Bunge la Muungano liwe ni kama upper house ambapo litakuwa na wajumbe sio zaidi ya 100 watakaochaguliwa na kila mkoa (kila mkoa wabunge 2 na idadi inayobakia wanatokana na uwiano wa kura). Mkuu wa shughuli za Serikali ya Muungano katika Bunge la Muungano anakuwa ni Makamu wa Rais wa Muungano.

Nadhani mfumo huu utahakikisha muungano wa Serikali 3 bila kuathiri muungano, utaongeza uwajibikaji kwani Serikali za Tanganyika na Zanzibar zitakuwa na Executive PMs na watawajibika moja kwa moja Bungeni, tutaepuka kuwa na marais 3 (Rais wa muungano, Rais wa Tanganyika na Rais wa Zanzibar). Migogoro yeyote itakayotokea kuhusu muungano itakuwa resolved na Baraza la Muungano ambao litakuwa na wawakilishi wa pande zote mbili. So Presidential system at Union level, Parliamentary system at States levels. Unaonaje pendekezo hilo

Mh. system uliyopendekeza kama inafanania na ile ya India au Singapore ambapo President ni head of the State na Prime Minister head of the executive. Then, kuna lower and upper house (with president belong to the upper house). So, India na Singapore zinafuata Westminster system ambapo executive power is vested in the Prime Minister, while the president, plays a minimal role in affairs of State.

Kwa idea yako, tutaepuka kuwa na Marais watatu lakini hicho cheo kimoja cha urais kitakachobakia kinaweza kuwa ni ceremonial kwa sababu mamlaka mengi yatakuwa chini ya hao Mawaziri Wakuu wawili. Je, ananchi wengi watapenda kumchagua Rais ambaye ni ceremonial tuu? Pia kwa level ya governance tuliyonayo kwa sasa, unaweza kumkuta Rais aki-dictate hao mawaziri wakuu wafanye kazi kuvipi hasa kama wanatokea chama chake.

Lakini kubwa la kiutawala, kwa kuwa na Waziri Wakuu wawili, ina maana watakuwa na mamlaka yanayolingana in their respective areas? Nani atakaye-appoint na ku-dismiss mawaziri? Mawaziri Wakuu or the President? India Prime minister ndiye anaye-appoint na ku-dismiss mawaziri. Pia ni chairman wa cabnet. Kiutawala kama mimi ni chief executive, then sitapenda mtu mwingine anichagulie wasaidizi wangu. Na kama mawaziri watakuwa appointed na Rais, then watakuwa accountable kwa Rais, not the Prime Ministers. Hapa inaweza kuleta tabu.

Ni bora kuwa na a full parliamentary system. Stability ya parliamentary system, though bunge linaweza kuwa na wabunge wengi toka chama kimoja, appears to be best-suited for developing countries kama Tanzania. Kadri nchi inavyobadilika kimaendeleo ndivyo unaweza ku-introduce taratibu a more democratic and plural governance system along the lines of the presidential system.

Kwa kweli suala la muungano is the biggest obstacle kwenye ku-design a good and effective governing system. Kama sio huu muungano wala tusingekuwa na system ya utawala isiyoeleweka. Hata hii ya kusherekea miaka 50 ya uhuru sijui Wazazibari nao watasherekea? Kwa mfano, kama umeona kile kijarida cha kusherekea miaka 50 ya uhuru, kwenye cover kina picha za viongozi sita. Kati hao, wanne wanatokea Zanzibar.

This does not sit well na statement ya Rais wa Tanzania kuutangaza "mwaka 2011 kuwa ni Mwaka wa Maadhimisho ya Miaka Hamsini ya Uhuru wa Tanzania Bara." Kama ni miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara, then kuna umuhimu gani wa kuweka picha za viongozi wasiotoka Tanzania Bara kwenye hicho kijarida? A good and effective governing system lazima itaadhiri muungano tuu. Watanganyika na Wazanzibari have got something to say about this muungano. Kwa nini wasipewe nafasi through referendum to express their views? Hii ingesaidia sana in future to design a good governing system.
 
Mkubwa, na wewe pia unachemka.

Impeachment does not necessarily "imply that a crime has been committed by the President." Angalia articles of impeachment kwenye katiba uone ni vitu gani vitatu vinavyoweza kutumika kuleta mashitaka bungeni.

Ibara ya 46 ambayo ndiyo hasa inaeleza namna ya kuleta mashtaka dhidi ya rais is very theoretical! It is practically impossible kum-impeach rais kwa kufuata vifungu hivyo kwenye hali tunayoishi sasa.Impossible. Nadhani hiki ni kilelezo kingine kwa nini tunahitaji mjadala mpana kwenye hii katiba mpya maana ukisoma hiyo ibara ya 46 haingii akilini wabunge walipitishaje? Labda kwa sababu ilikuwa na enzi za 'zidumu fikra za mwenyekiti' hivyo hakukuwa na mjadala juu ya vipengele vya hii ibara. Mfano 46A (4) (a) kinahusu kuunda kamati maalum ya bunge kuchunguza madai dhidi ya rais. Kifungu kinasema hivi "Judge mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati".

Judge mkuu anateuliwa na rais, kwa mazingira yetu leo hii Judge Othman Chande anaweza kumchunguza Rais Kikwete? Hata kama katiba inasema hivyo lakini kwa mazingira tunayoishi sasa hili linawekezana kweli, na akatoa impartial results? Kwa kifupi katiba tuliyonayo inapwaya sana!
 
Mkubwa, na wewe pia unachemka.

Impeachment does not necessarily "imply that a crime has been committed by the President." Angalia articles of impeachment kwenye katiba uone ni vitu gani vitatu vinavyoweza kutumika kuleta mashitaka bungeni.

Did I say that impeachment "necessarily" imply that a crime has been committed by the President? After all, crime is an act punishable by law as well as an evil act not necessarily punishable by law. Nilivyosema "crime" sikuwa na maana ya "crimes" unazozifikiria. I meant a "crime" for the purpose of the Parliament. That impeachment is a procedure, under which the President is brought up on charges and tried by the Parliament, and, if convicted, the is removed from office. Kwenye mabunge ya nchi nyingine wanasema ame-commit a "crime". Sasa kama wewe umechukulia maana ya neno "crime" kama linavyotumika bungeni kama "crime" ya kawaida, then imekula kwako. LOL.
 
Ibara ya 46 ambayo ndiyo hasa inaeleza namna ya kuleta mashtaka dhidi ya rais is very theoretical! It is practically impossible kum-impeach rais kwa kufuata vifungu hivyo kwenye hali tunayoishi sasa.Impossible. Nadhani hiki ni kilelezo kingine kwa nini tunahitaji mjadala mpana kwenye hii katiba mpya maana ukisoma hiyo ibara ya 46 haingii akilini wabunge walipitishaje? Labda kwa sababu ilikuwa na enzi za 'zidumu fikra za mwenyekiti' hivyo hakukuwa na mjadala juu ya vipengele vya hii ibara. Mfano 46A (4) (a) kinahusu kuunda kamati maalum ya bunge kuchunguza madai dhidi ya rais. Kifungu kinasema hivi "Judge mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati".

Judge mkuu anateuliwa na rais, kwa mazingira yetu leo hii Judge Othman Chande anaweza kumchunguza Rais Kikwete? Hata kama katiba inasema hivyo lakini kwa mazingira tunayoishi sasa hili linawekezana kweli, na akatoa impartial results? Kwa kifupi katiba tuliyonayo inapwaya sana!

Mkuu you're right. Ni vigumu sana Bunge kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais. Ni bora kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais kwa sababu hoja kama hiyo huwa inaletwa na upinzani bungeni. Na kama upinzani una wabunge wengi bungeni, it is likely that they will win the vote. Na kama Rais aki-respond kwa kuitisha vote of confidence motion, itakuwa ngumu kupata hiyo kura kutokana na wingi wa wabunge wa upinzani.

Many parliamentary and presidential political systems include the vote of no confidence in their constitution. Surprisingly, Katiba yetu haina kipengenge cha vote of confidence in relation to the President. But in modern times, votes of no confidence are relatively rare occurrences in democracies. Unless kuwe na wabunge wengi wa upinzani, kutakuwa na relevance yoyote ya kuwa na kifungu cha vote of no confidence kwenye katiba? Mfano ni hii ya juzi iliyofanyika Greece: Greek PM survives confidence vote, signals he may quit | Reuters
 
....Nilivyosema "crime" sikuwa na maana ya "crimes" unazozifikiria. I meant a "crime" for the purpose of ....
Hahahahahahahahhaaaa ha ha hahaaaaaa.....

kaka unatafuta pa kutokea ki utu uzima? Crimes ziko defined kwenye penal code na sheria zinazo define offenses, hakuna crimes za kibunge. Mwanangu umechemka, kubali, kwenye bao ningekwambia swaiba panga tuanze lingine, sio lazima watoto waone unaliwa kete zote!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mfumo aliopendekeza Zitto ni mzuri sana nauunga mkono, nadhani pia tuwe na utaratibu wa rais wa muungano kujibu maswali ya wabunge kwenye bunge la muungano
 
Pasco,

Nimekusoma mara nyingi lakini naomba niseme kitu kimoja. Sometimes, huwa unapotosha sana kwa ku-cite a wrong law. Kama hapa unajaribu kupotosha kuwa kwenye Katiba kuna ibara inayowezesha Bunge kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais. That is not true. Kama hiyo ibara ipo, tuwekee hapa tafadhali. Bunge linaweza kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu lakini sio Rais. Insted, Bunge linaweza kupitisha tuu azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais.

Nafikiri utakuwa ni mmoja wa wale wachache ambao mnashindwa kutofautisha kati ya vote of no confidence na impeachment. The two phrases mean different things. Impeachment implies that a crime has been committed by the President whilst a vote of no confidence does not imply that the person under vote has committed a crime.

Kwa hiyo BAK yuko right kabisa kutaka kuwepo kwa kipengele cha kutokuwa na imani na Rais kwenye Katiba mpya kwa sababu hakuna kipengele kama hicho kwenye Katiba ya sasa.

Ahsante sana Mkuu EMT
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mfumo anaoupendekeza Mh. Zitto, at least at Parliamentary level unafaa, suala kubwa ni namna ya kumuaccomodate President. Siungi mkono hoja ya kuwa na wajumbe 100, ambapo kila mkoa utatoa wajumbe 2. This again is the misuse of our resources, which we can not afford. Mfumo wowote tunaoutaka lazima uzingatie jambo moja muhimu kuwa sisi ni nchi masikini!
 
Wakati tunajadili kuhusu katiba yetu ya Tanzania; pia kuna umuhimu mkubwa kabisa kutatua matatizo ya Muungano.Ili hii katiba iwe ni ya Serikali ya Tanzania nzima.Mugawanyo wa madaraka uwe wazi; tukiweka kwenye katiba kuwa rais wa Zanzibar ndiye Makamu wa Rais wa Tanzania; je inapotokea Rais wa Tanzania pia anatoka Zanzibar; hapo kutaleta tena utata wa uwakirishi wa juu katika serikali ya Muungano.Inabidi kabla ya kufikia kuliweka hili ndani ya katiba yetu, tuutazame Muungano wetu uwe wa aina gani. Uwe wa Tanganyika na Zanzibar zikiwa na mamlaka yake; lakini zikiwa zimeungana kuunda Serikali ya Muungano. Tanganyika ikiwa na uongozi wake; vivyo hivyo na Zanzibar ikiwa na uongozi wake.Hii itapunguza utata inapotokea Rais wa Muungano anatoka sehemu moja ya Muungano moja kwa moja rais wa upande mwingine ndiye anakuwa Makamu wa kwanza wa Rais na yule wa upande husika anakuwa Naibu makamu wa Rais wa Tanzania. Muundo wa sasa wa Muungano hauekeweki ndiyo maana kero ni nyingi.
 

- Katiba ni ya taifa sio ya CCM, infact kwenye hili la katiba mpya CCM lazima ile bullet kwa the good of the Nation at large!

Umeogea sahihi lakini ndani ya CCM nani mwenye mawazo kama hayo?????????. Mimi nimekuwa mmoja wa kuwashanga watu walikuwa wanamshabula J. Makamba utadhani pale ikulu alikuwa ana akazi muhimu sana. Lakini nilisikita sana kuona mchango na maoni yake juu ya kusafisha chama.(kuvua magamaba)

Kama CCM yenu ndio future yake iko kwenye watu wenye mawazo ya kichama chama zaidi badala ya taifa basi Ni nafuu tuwe na Kiongozi "mchonganishi" kama JK kuliko kuliko so called vijana kama January.

Nilivyosoma magazeti nilishindwa kuelewa nani ni kijana kati ya JK ya January.
 
I'm not politician neither have I got a political Godfather. I'm just a Tanzanian.
We need leaders that can deliver real change and not spend their time in office plotting how they can be re-elected back in office.
We need leaders that have the interest of the nation at heart rather than those with selfish agenda.
We need leaders that know when they are wrong to resign when their intergrity is questionable.
We need leaders that can identify with the numerous ethnic groups in Tanzania.
We need leaders that can steer the country to real change rather than those that are vague, with unachievable promises
We need leaders than serve the nation rather than those that are served by the nation.

A call from all Tanzanians, we real have to wake up and smell the coffee. We are all brothers and should not let these tyrants divide us. Let's educate one another and help steer our country towards democracy. Let's join hands in getting rid of these power hungry individual from power not by stoning, burning, machetteing or bullet but by bail out.

Remember when it was time to debate on their pay, they all agreed. Time for any agenda that benefit the nation then they fight each other.

THINK
 
Tatizo kubwa mawazo, na effotr na akili za watu wengi katika suaa la katiba zimeelekezwa na zimejikitasana kwenye katiba ya "siasa." Tunahitaji watu watambue katiba tunayotaka sio tu ya kisisasa ya kupata wabunge na marais. Tunataka katiba inayotambua wajibu , mipaka, umuhimu , majukumu ya watumishi wa umma nyingine kama Ulinzi, teknlojia, ustawi wa jamii, uchumi, Eimu, etc

Hatutaki katiba ya kulipa bunge nguvu kwa mgongo kuwa ni wawakilishi wa wananchi huku lenyewe na wabunge wake wakijiongezea mishahara bila kuwepo na chomb a huru cha kuhoji au kuhalaisha kwa nini mbunge apokee marupu rupu mengi kulio afisa elimu wa mkoa.

Tunawashukru CDM kwa kukomalia hii issue lakini tunawaomba pia wasijisahu wakadai katiba na mabailiko ya kisiasa tu.
 
Unaonaje katika Katiba mpya tuwe na Parliamentary system kwa Zanzibar and Tanganyika governments and Presidential system kwa Union Government? Kwa hiyo Mkuu wa Serikali ya Tanganyika awe Waziri Mkuu na atokane na chama chenye Wajumbe wengi katika Baraza la Wawakilishi Tanganyika, Mkuu wa Serikali ya Zanzibar awe Waziri Mkuu wa Zanzibar na atokane na chama chenye Wawakilishi wengi katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
Mkuu wa Nchi awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Bunge la Muungano liwe ni kama upper house ambapo litakuwa na wajumbe sio zaidi ya 100 watakaochaguliwa na kila mkoa (kila mkoa wabunge 2 na idadi inayobakia wanatokana na uwiano wa kura). Mkuu wa shughuli za Serikali ya Muungano katika Bunge la Muungano anakuwa ni Makamu wa Rais wa Muungano.

Nadhani mfumo huu utahakikisha muungano wa Serikali 3 bila kuathiri muungano, utaongeza uwajibikaji kwani Serikali za Tanganyika na Zanzibar zitakuwa na Executive PMs na watawajibika moja kwa moja Bungeni, tutaepuka kuwa na marais 3 (Rais wa muungano, Rais wa Tanganyika na Rais wa Zanzibar). Migogoro yeyote itakayotokea kuhusu muungano itakuwa resolved na Baraza la Muungano ambao litakuwa na wawakilishi wa pande zote mbili.
So Presidential system at Union level, Parliamentary system at States levels. Unaonaje pendekezo hilo


Mh Zitto ..mfumo uliopendekeza ni mzuri...lakini muhimu hapo ni tujuwe atakayekuwa na mamlaka juu ya vyombo vyote vya dola.....kwa kifupi amiri jeshi mkuu awe ni rais wa muungano...
Pia hapa Zanzibar itabidi wabadili tena katiba Yao iendane na katiba ya muungano.....of which naona Kama Zanzibar factor ni ngumu ...kwa kifupi wao ndio Wenye veto kwenye huu mchakato....na sidhani kama tunawatendea haki watanganyika kwenye hili....

Umeongelea kuwa waziri mkuu atokane na chama cheenye wabunge wengi kwenye lower house....?.....Kuna uwezekano hapa wa waziri mkuu na rais kuwa vyama tofauti ....na rais atakuwa na dola....hapa panaweza kuwa na tatizo...wakitofautiana.....

Jambo lingine la jumla ambalo ningependa tujadili ....mnaonaje tuwe na serikali za majimbo au mikoa zenye nguvu zaidi na kuwajibika kwa wananchi .......kuleta maendeleo badala ya mfumo wa sasa wa wakuu wa mikoa au wilaya ambao ni Kama viranja tu wa kisiasa na wengi wao hasa wa mikoa ya pembezoni wanashinda Dar kila siku.....hawana uchungu kabisa na wananchi.....
Tukiimarisha local gorverment inaweza beba jukumu hili......yaani chama chenye wabunge wengi wilayani ...Kitatoa meya ambao yeye na wao ndio watakaoendesha serikali ya wilaya kwa ujumla....watendaji wataendelea kutoka serikali kuu kwa dhana ya umoja wa kitaifa.....
Nafasi ya meya (wamkoa) au Gavana Itatokana na chama chenye overal majority ya madiwani kwenye mkoa .....

Sioni tija peyote sasa ambako kuna watendaji wa halmashauri na wilayani ....it is dupilication of posts.....serikali inaweza kupunguza nusu ya watendaji wake kwa mfumo huuu na kazi zitaenda haraka zaidi....watakaopunguzwa watasaidia kusukuma sekta binafsi...sio lazima kila mtu aajiriwe na serikali.......tunahitaji waondoke ,ili tupate nafasi za Kuajiri walimu zaidi....,polisi etc...
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mkuu Philemon, hoja ya Majimbo inajadilika sana na ni muhimu sana kwenye Katiba mpya, ninaitafutia hoja kabla sijaifungulia thread: MUCH RESPECT!
 
Mfumo anaoupendekeza Mh. Zitto, at least at Parliamentary level unafaa, suala kubwa ni namna ya kumuaccomodate President. Siungi mkono hoja ya kuwa na wajumbe 100, ambapo kila mkoa utatoa wajumbe 2. This again is the misuse of our resources, which we can not afford. Mfumo wowote tunaoutaka lazima uzingatie jambo moja muhimu kuwa sisi ni nchi masikini!

Tuandike katiba kwa kuzingatia kuwa sisi ni nchi masikini? Unaamini tutaendelea kuwa masikini daima dumu? Nadhani tuandike katiba kwa kuzingatia kwamba mifumo ya UWAJIBIKAJI inakuwa imara. Uwajibikaji utasaidia sana kuhakikisha rasilimali za nchi zinatumika kwa maendeleo ya wananchi. Attitude ya umasikini tuiondoe katika akili zetu. Tanzania ni nchi tajiri yenye watu masikini....
 
Mh Zitto ..mfumo uliopendekeza ni mzuri...lakini muhimu hapo ni tujuwe atakayekuwa na mamlaka juu ya vyombo vyote vya dola.....kwa kifupi amiri jeshi mkuu awe ni rais wa muungano...
Pia hapa Zanzibar itabidi wabadili tena katiba Yao iendane na katiba ya muungano.....of which naona Kama Zanzibar factor ni ngumu ...kwa kifupi wao ndio Wenye veto kwenye huu mchakato....na sidhani kama tunawatendea haki watanganyika kwenye hili....

Umeongelea kuwa waziri mkuu atokane na chama cheenye wabunge wengi kwenye lower house....?.....Kuna uwezekano hapa wa waziri mkuu na rais kuwa vyama tofauti ....na rais atakuwa na dola....hapa panaweza kuwa na tatizo...wakitofautiana.....

Jambo lingine la jumla ambalo ningependa tujadili ....mnaonaje tuwe na serikali za majimbo au mikoa zenye nguvu zaidi na kuwajibika kwa wananchi .......kuleta maendeleo badala ya mfumo wa sasa wa wakuu wa mikoa au wilaya ambao ni Kama viranja tu wa kisiasa na wengi wao hasa wa mikoa ya pembezoni wanashinda Dar kila siku.....hawana uchungu kabisa na wananchi.....
Tukiimarisha local gorverment inaweza beba jukumu hili......yaani chama chenye wabunge wengi wilayani ...Kitatoa meya ambao yeye na wao ndio watakaoendesha serikali ya wilaya kwa ujumla....watendaji wataendelea kutoka serikali kuu kwa dhana ya umoja wa kitaifa.....
Nafasi ya meya (wamkoa) au Gavana Itatokana na chama chenye overal majority ya madiwani kwenye mkoa .....

Sioni tija peyote sasa ambako kuna watendaji wa halmashauri na wilayani ....it is dupilication of posts.....serikali inaweza kupunguza nusu ya watendaji wake kwa mfumo huuu na kazi zitaenda haraka zaidi....watakaopunguzwa watasaidia kusukuma sekta binafsi...sio lazima kila mtu aajiriwe na serikali.......tunahitaji waondoke ,ili tupate nafasi za Kuajiri walimu zaidi....,polisi etc...

Rais wa Jamhuri ya Muungano ndiye anakuwa Amiri jeshi Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, mkuu wa nchi. Kila Waziri Mkuu atateua Baraza lake la Mawaziri bila kuingiliwa na Rais. Rais wa muungano atateua Mawaziri kwa Wizara za Muungano tu - Nje, Ulinzi, Ndani, Union Treasury.

Ni kweli Rais na Mawaziri wakuu wataweza kutoka vyama tofauti. Huu ndio mfumo uliopo hata sasa kwamba WM anatoka chama chenye wabunge wengi na sio lazima kiwe chama anachotoka Rais.
 
- Wakati umefika wa kupunguza msururu wa Viongozi wa juu, na hasa gharama za kuwatunza waki-retire, I mean people naomba kuuliza hivi kweli tunawahitaji Waziri Mkuu na Makamu wa Rais katika Serikali yetu? kwa maoni yangu one has to go kwenye katiba mpya na hasa Makamu wa Rais, kama ni muhimu kuwa naye basi Waziri Mkuu ashike hiyo nafasi kama zamani.

- The idea kwamba hata Visiwani kunakuwa na Makamu wa Rais, tena wawili it does not make a sense at all, wanafanya nini? Hivi vinakuwa ni vyeo vya huruma tu, under whose expense? kodi yetu wananchi wakati ni sasa kwenye katiba mpya kuondokana na na huu msururu wa Viongozi wa juu, tuwe na huruma kwa Walalahoi kidogo jamani!

MUCH RESPECT PEOPLEs!

William @..NYC, USA: Mutuz Le Baharia!

Mawazo ni mazuri sana, kama wanataka kuwa na makamu wa rais na kama bado tupo kwenye muungano, basi kama rais atatoka Tanzania bara, waziri mkuu atoke Tanzania visiwani na kinyume chake... Lah basi cheo cha rais kiondolewe kibakie cha waziri mkuu, au cheo cha uwaziri mkuu kiondolewe na rais ndio hawe waziri mkuu.

Mimi si Mwanasiasa, na si mtu wa kupigia debe haya mambo ya siasa za Kiafrika... Lakini kuna mambo ambayo uwa nayaona kama si lazima sana yawepo na haswa kwenye safu ya uongozi wa nchi.

Haya mambo ya kuwa na Wabunge wa viti maalum , Wabunge kuwa Mawaziri, Wakuu wa mikoa kuchaguliwa n a Rais... Mikoa kuwa na Meya hapo hapo kuna Mkuu wa Mkoa... Yote haya ni maswala ambayo yanapaswa kuangaliwa upya.

Kwa sababu mtu akigombea ubunge kisha anachaguliwa tena kuwa Waziri, kunapunguza uwakilishi wake Bungeni. Na kama wabunge kubaki kuwa wabunge kutaondoa tamaa ya Wabunge kujipendekeza kwa serikali ili wachaguliwe kuwa mawaziri....

Kuhusiana na muda au vipindi vingapi kwa maoni yangu mimi as long as wananchi wanakupenda na uwezo wa kuwakilisha na kutatua matatizo ya wananchi unayo basi endelea kugombea... Hii ni kwa ngazi ya ubunge... Na wanapaswa kuwa na ofisi kwenye majimbo yao au hata ofisi ndogo uko vijijini, na iwe lazima mbunge kutembelea jimbo lake na vitongoji mwake kila mwaka, na hakishindwa basi hawajibishwe na atumie pesa au posho anazolipwa uko bungeni (yaani kusiwe na pesa za ziada kutoka serikalini wala asiombe kwa wananchi, labda wananchi wapende wenyewe kumchangia au chama chake kifanye utaratibu wa kumpatia)

Vilevile kwenye Ukuu wa Mikoa ingependeza zaidi kama hawa wakuu wa mikoa nao wakagombea au kupigiwa kura kama wanavyo pigiwa kura wabunge.... Hii kutawalazimisha kuwajibika kwa raiya zao... Au hao wabunge wa Mkoa au jimbo ndio wanapaswa kugombea nafasi ya Ukuu wa mkoa, hapa ina maanisha kuwa Wabunge wakishirikiana na mkuu wao wa mkoa (ambaye naye ni mbunge) wanakaa katika baraza ambalo wao pamoja na viongozi wachache wa kiraiya, wakiwemo wakuu wa wilaya na raiya waliochaguliwa kuingia kwenye kamati ya kujadiri matatizo ya wananchi, ndio wataamua nini kipelekwe uko bungeni na ikiwezekana miswaada ya bunge inapitia ngazi hii kwanza na kupata maamuzi wa kila mkoa na kisha ndio uko bungeni kunapelekwa mapendekezo au maamuzi ya kimkoa, kwa sababu wananchi washa shirikishwa na uwamuzi ushatolewa.

Kama haiwezekani basi iwepo serikali ya majimbo, ambayo itakuwa na uwajibikaji mkubwa wa majimbo...

Mfano:
Dar Es Salaam, Pwani na Morogoro, linaweza kuwa ni jimbo Moja.
Kagera, Kigoma, na Mara,
Singida, Dodoma na Iringa
Rukwa, Mbeya
Ruvuma, Mtwara na Lindi
Kilimanjaro, Manyara na Tanga
Zanzibar
Pemba
Au ikachaguliwa mikoa yenye kupakana na yenye ukaribu zaidi.
 
Unaonaje katika Katiba mpya tuwe na Parliamentary system kwa Zanzibar and Tanganyika governments and Presidential system kwa Union Government? Kwa hiyo Mkuu wa Serikali ya Tanganyika awe Waziri Mkuu na atokane na chama chenye Wajumbe wengi katika Baraza la Wawakilishi Tanganyika, Mkuu wa Serikali ya Zanzibar awe Waziri Mkuu wa Zanzibar na atokane na chama chenye Wawakilishi wengi katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
Mkuu wa Nchi awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Bunge la Muungano liwe ni kama upper house ambapo litakuwa na wajumbe sio zaidi ya 100 watakaochaguliwa na kila mkoa (kila mkoa wabunge 2 na idadi inayobakia wanatokana na uwiano wa kura). Mkuu wa shughuli za Serikali ya Muungano katika Bunge la Muungano anakuwa ni Makamu wa Rais wa Muungano.

Nadhani mfumo huu utahakikisha muungano wa Serikali 3 bila kuathiri muungano, utaongeza uwajibikaji kwani Serikali za Tanganyika na Zanzibar zitakuwa na Executive PMs na watawajibika moja kwa moja Bungeni, tutaepuka kuwa na marais 3 (Rais wa muungano, Rais wa Tanganyika na Rais wa Zanzibar). Migogoro yeyote itakayotokea kuhusu muungano itakuwa resolved na Baraza la Muungano ambao litakuwa na wawakilishi wa pande zote mbili.
So Presidential system at Union level, Parliamentary system at States levels. Unaonaje pendekezo hilo
Mawazo mazuri sana mkuu wangu isipokuwa tu ktk mfumo huo rais atachaguliwa vipi? kutokana na 1. Popular vote; 2.Mwenye wajumbe wengi ktk Bunge la Muungano (Upper house) au 3.Matokeo ya chaguzi za majimbo ktk states mbili (Tanganyika/ Zanzibar) .

- Yapi majukumu ya rais tukisha kuwa na mfumo kama huu. Maadam kila state itakuwa na waziri mkuu wake, hawa watakuwa na madaraka juu ya uthibiti, usimamiaji na utekelezaji wa kila siku kazi na shughuli za states hizo ni nani atachukua nafasi ya waziri mkuu ktk serikali ya Muungano.

Samahani nimefanya editing baada ya kuona umependekeza makamu wa rais kuchukua nafasi ya waziri mkuu bunge la Muungano..

Mkuu huoni kaa huyu rais atakuwa - ceremonial President maanake sioni kazi ilobakia ikiwa kila state itajitawala na bunge la muungano kuna makamu wa rais, yeye rais atakuwa na madaraka gani haswa?
 
Back
Top Bottom