Hapa sio kwa wafanyakazi wenye direct access ya bima huko anapofanyia kazi?Km nilivyoelewa mtoto unaweza kumsajili km tegemezi naona imekaa vzr maana ilitolewa hii
Kabla ya kuja na ushauri wangekuja kwa wadau, wanachama nini kifanyike. Kwani kinachowasibu wananchi au wateja wenu baada ya kuwazuia huduma toto afya hamkijui? Vaeni viatu vya wengine.
Mnamo Machi 13, 2023 NHIF ilitoa taarifa rasmi kutangaza kusitisha Huduma ya Toto Afya Kadi ili kupisha Maboresho ya huduma hiyo na kuwataka Wazazi kusajili Watoto kama Wategemezi kupitia Vifurushi vingine vya Bima ya Afya au Shule wanazosoma, soma: NHIF yafuta Bima ya Afya kwa watoto "Toto Afya Kadi".
Je, Una maoni gani kwa NHIF na Serikali baada ya tangazo hilo?
Nini maoni yako kuhusu hili?
Ili kupata nafasi ya kupaza sauti yako katika mjadala huu tafadhali jiunge nasi katika Mjadala wa TwitterSpace ya JamiiForums itakaofanyika tarehe 15/03/2023 kuanzia saa 12:00 jioni mpaka saa 02:00 usiku.
Pia, unaweza kuandika maoni yako kwenye uzi huu ambayo yatasomwa siku ya mjadala.
Karibuni.
Ni vitu vilivyowahitaji fikra nyepesi tu. Dunia inakabiliana kupunguza vifo vya watoto wao Wana entertain kuondoa tiba ya mtoto, Tena anayelindwa na sera ya matibabu bure. Hivi waliikaa kikao na kufikiri? Au sababu wao Wana uhakika na matibabu muogopeni Mungu. Mtoto ni malaika, alikuja duniani kwa mapenzi ya watu wazima si kwa yeye kupenda, naungana nawe mtoto apewe haki yake. Kwanza Serikali ilipaswa imtibu huyo mtoto kutoka day 1 Hadi 5 yrs, wananchi wameisaidia kwa kujilipia bimaHuo ni ubinafsi na hatua mbaya kwa wananchi wa hali ya chini, muogopeni Mungu nyie wahusika wa huu mpango.
Sio watu wote wapo na ajira au mifumo ya kuchangia bima iweje leo hii mlete huo mpango?
Lengo ni kupunguza idadi ya wanachama kama mlivyokuwa mkilalamika kuwa mfuko unaelemewa?
mnakera saana nitarudi usiku kuendeleza hoja.
kwa mujibu wa nhif, mtoto wako atakuwa covered mpaka bima yake itapoisha ndiyo ukitaka kumkatia tena utaratibu mpya utatumika.mimi nimo katika wale wanaosubiria siku 90 za kupewa kadi yangu ya TOTO
Kwa ajili ya mwanangu
hivi sasa zimesalia siku 25 tu kupewa.
thankskwa mujibu wa nhif, mtoto wako atakuwa covered mpaka bima yake itapoisha ndiyo ukitaka kumkatia tena utaratibu mpya utatumika.
Ambayo nayo itakuwa failure...Hii ni hatua mojawapo ya kuelekea BIMA YA AFYA KWA WOTE.
Kwa kweli. Kwanza walianza na kuondoa utaratibu va zile fomu za bima za njano za kuchukulia dawa nje ya hospitali kwa zile dawa ambazo hospitali hakuna, utaratibu huo unatutesa hadi sasa maana inabidi utoe pesa cash ukanunue. Wameona haitoshi wamekuja na wanayodai maboresho ya mfuko wa bima, haya siyo maboresho bali ni ukatili kwa mtoto kama ukatili mwingine tu.Wizara imemshinda Ummy aondolewe apishe watu wenye huruma na ubunifu kwa watanzania.
Kuna watoto ambao wazazi wao wapo nje sasa wazazi hao wanakata bima kwao zitawasaidia nini?
Hiyo NHIF iliyofilisika ndio inaenda kufa kibudu. Kibudu cha kifo cha mende miguu juu
Ndio maana Madelu anawaambia wanajuatu mambo ya usangoma
Hawataweza maana ni sehemu ya walamba asali wao wakisimama majukwani kazi ni kutoa viloja vya kipumbavu kama kula ugali ni umasikini.Nawaomba lema na heche wapigie kelele hili jambo.