Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 10,509
- 16,734
Tangu taifa la Russia lilipoanza kufanya huruma na kupeleka chakula Ulaya inaonekana nguvu za jeshi la Ukraine zimeongezeka kiasi kwamba sasa kuna taarifa katika baadhi ya maeneo yaliyoshikiliwa na Urusi tangu wiki hii kuanza huko mashariki ya Ukraine yamekombolewa na wanajeshi wa Ukraine.
Raisi Erdogan wa Uturuki hapo juzi alizitahadharisha nchi za Ulaya na Marekani kuwa wasiichukulie Urusi kama taifa poa na kwamba vita hivyo havitoisha kwa kushindwa kwake.
Erdogan ambaye anazijua vizuri hali za jirani zake na yeye mwenyewe akiwa mvumilivu sana katikati ya hali ngumu na ni hodari wa kujibadili rangi zake, amekuwa akiiuzia Ukraine droni zake zinazoipiga Urusi na wakati huo huo akichukua nafaka za Ukraine kupitia mkono wa Urusi kwa bei poa.
Raisi Erdogan wa Uturuki hapo juzi alizitahadharisha nchi za Ulaya na Marekani kuwa wasiichukulie Urusi kama taifa poa na kwamba vita hivyo havitoisha kwa kushindwa kwake.
Erdogan ambaye anazijua vizuri hali za jirani zake na yeye mwenyewe akiwa mvumilivu sana katikati ya hali ngumu na ni hodari wa kujibadili rangi zake, amekuwa akiiuzia Ukraine droni zake zinazoipiga Urusi na wakati huo huo akichukua nafaka za Ukraine kupitia mkono wa Urusi kwa bei poa.