KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,591
- 4,604
Kwanza, Ninampongeza Waziri mkuu kwa kutatua mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo uliodumu kwa siku 3 mfufulizo. Katikati ya mgomo huo mpaka kutatuliwa kwake tumeona na kusikia mengi hususani madhila waliyokuwa wanakutana nayo wafanyabiashara kutoka kwenye vikosi kazi vya kodi.
Pamoja na mambo mengine, licha ya baadhi ya wafanyabiashara kuonewa lakini kuna wengine ni wakwepaji kodi. Na hapa ndio kwenye msingi wa hoja yangu KUDHIBITI UKWEPAJI KODI.
Kodi ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa lolote duniani hivyo ni jukumu la walipakodi kulipa kodi kulingana na Sheria na taratibu zilizopo. Na hapa ndio panahitajika uwepo wa vidhibiti ili kudhibiti ukwepaji Kodi.
Na haya ndio maoni yangu:
Moja, Kwa kuwa asilimia kubwa ya wafanyabiashara wanaagiza bidhaa zao kutoka nje ya nchi au kutoka viwanda vinavyotengeneza hapa nchini serikali itengeneze " inventory management system" ambayo itafungamanishwa na mfumo wa EFD.
Nikiwa na maana ya kwamba ' importer' wakiagiza bidhaa kutoka nje ya nchi huo mfumo utatumika kufatilia ' inventory' ya huo mzigo kutoka kwa muagizaji mpaka kwa mlaji wa mwisho. Vivyo hivyo kwa bidhaa zinazozalishwa nchini mfumo ufanye udhibiti kutoka kwa mzalishaji mpaka kwa mlaji wa mwisho.
Tukianza kwa 'importer' au muagizaji ,mfumo ufanyaje kazi?
Kwanza, Serikali kwanza idhibiti mianya yote ya kuingizia bidhaa kimagendo kutoka nje na bidhaa zote zinazoingizwa kutoka nje zipitie kwenye mfumo wa forodha iwe bandarini au mipakani. Na hapo kwenye forodha bidhaa zote zisajiliwe na ziingizwe kwenye mfumo wa EFD wa muagizaji. Kwa mfano, vimeagizwa vitenge vitenge 5000 kutoka nje, vitenge hivyo viingizwe wenye mfumo wa EFD wa muagizaji kwamba vitenge hivyo ndio vinakuwa Stock yake mpya. Kama huyo muagizaji akitaka kuuza labda vitenge 200 kwa mteja A ,kupitia kwenye mfumo wa EFD atapunguza vitenge 200 na kubaki 4800 na hivyo 200 atasajili kwenye mfumo wa EFD wa huyo mteja huo.
Mteja A akitaka kuuza vitenge 20 kwenda kwa mteja B atapunguza stock kwa 20 na kubakiwa na 180.
Vivyo, kwa mzalishaji kwenye kila kiwanda kikubwa na vya kati wawepo maafisa wa TRA na hao kazi yao ni kuwasajili wafanyabiashara wanaonunua bidhaa moja kwa moja kwa mzalishaji na hapa tumuite mteja ambaye pia ataingiza kwa mteja B na process itaendelea hivyo mpaka kumfikia mlaji wa mwisho.
Pili, ili hili liwe maana wafanyabiashara wote wawe na mashine za EFD isipokuwa kwa wale tu ambao wanatambuliwa kama machinga na machinga wote wawepo kwenye maeneo waliyopangiwa. Machinga yoyote anayefanya biashara mbele ya duka la mtu aliyesajiliwa kwenye mfumo naye ni lazima atoe risit za EFD kama wenzake.
Tatu, badala ya kuhusisha task force na mengineyo TRA ijikite kwenye kaguzi za kushtukiza kwenye maduka au waajiri kampuni za ukaguzi wa mahesabu kuwasaidia kufanya kazi wanapohisi pana ubadhirifu. Kwa kuwa stock zitakuwa zimesajiliwa kwenye mfumo itakuwa ni rahisi kujua ubadhirifu.
Faida za uwepo wa INVENTORY MANAGEMENT SYSTEM
Kwanza, kutakuwa na udhibiti mzuri wa stock utakaowezesha kufanya makadirio sahihi ya Kodi. Kupitia kwenye mfumo TRA itajua ni mzigo kiasi gani mfanyabiashara alioingiza, kiasi gani alichouza na kwa kiasi gani alichouza na kilichobaki ni kipi kwa hiyo itawezesha kufanya physical stock taking kwa urahisi na kujua udanganyifu.
Pili, Mfumo utarahisha ufanyaji kazi wa TRA na kuweka kwa uwazi mkubwa shughuli za wafanyabiashara na walipakodi
Wanasema namba hazidanganyi, mfumo huu utapunguza udanganyifu kwa kiwango kikubwa na matukio ya kupika stock ili kulipa kodi pungufu yatapungua.
Tatu, mfumo huo utatumika kama mbadala wa usajiri wa stoo kwa sababu imezoeleka wafanyabiashara kutumia stoo Kama kichaka Cha kutoa bidhaa bila risiti hivyo kwa kuwa mfumo huu utasaidia kujua inventory nzima ya mfanyabiashara tafsiri yake tutaijua tu stoo kwa sababu kwenye physical stock taking stoo pia itaoneshwa.
Ni hayo tu kwa leo
Pamoja na mambo mengine, licha ya baadhi ya wafanyabiashara kuonewa lakini kuna wengine ni wakwepaji kodi. Na hapa ndio kwenye msingi wa hoja yangu KUDHIBITI UKWEPAJI KODI.
Kodi ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa lolote duniani hivyo ni jukumu la walipakodi kulipa kodi kulingana na Sheria na taratibu zilizopo. Na hapa ndio panahitajika uwepo wa vidhibiti ili kudhibiti ukwepaji Kodi.
Na haya ndio maoni yangu:
Moja, Kwa kuwa asilimia kubwa ya wafanyabiashara wanaagiza bidhaa zao kutoka nje ya nchi au kutoka viwanda vinavyotengeneza hapa nchini serikali itengeneze " inventory management system" ambayo itafungamanishwa na mfumo wa EFD.
Nikiwa na maana ya kwamba ' importer' wakiagiza bidhaa kutoka nje ya nchi huo mfumo utatumika kufatilia ' inventory' ya huo mzigo kutoka kwa muagizaji mpaka kwa mlaji wa mwisho. Vivyo hivyo kwa bidhaa zinazozalishwa nchini mfumo ufanye udhibiti kutoka kwa mzalishaji mpaka kwa mlaji wa mwisho.
Tukianza kwa 'importer' au muagizaji ,mfumo ufanyaje kazi?
Kwanza, Serikali kwanza idhibiti mianya yote ya kuingizia bidhaa kimagendo kutoka nje na bidhaa zote zinazoingizwa kutoka nje zipitie kwenye mfumo wa forodha iwe bandarini au mipakani. Na hapo kwenye forodha bidhaa zote zisajiliwe na ziingizwe kwenye mfumo wa EFD wa muagizaji. Kwa mfano, vimeagizwa vitenge vitenge 5000 kutoka nje, vitenge hivyo viingizwe wenye mfumo wa EFD wa muagizaji kwamba vitenge hivyo ndio vinakuwa Stock yake mpya. Kama huyo muagizaji akitaka kuuza labda vitenge 200 kwa mteja A ,kupitia kwenye mfumo wa EFD atapunguza vitenge 200 na kubaki 4800 na hivyo 200 atasajili kwenye mfumo wa EFD wa huyo mteja huo.
Mteja A akitaka kuuza vitenge 20 kwenda kwa mteja B atapunguza stock kwa 20 na kubakiwa na 180.
Vivyo, kwa mzalishaji kwenye kila kiwanda kikubwa na vya kati wawepo maafisa wa TRA na hao kazi yao ni kuwasajili wafanyabiashara wanaonunua bidhaa moja kwa moja kwa mzalishaji na hapa tumuite mteja ambaye pia ataingiza kwa mteja B na process itaendelea hivyo mpaka kumfikia mlaji wa mwisho.
Pili, ili hili liwe maana wafanyabiashara wote wawe na mashine za EFD isipokuwa kwa wale tu ambao wanatambuliwa kama machinga na machinga wote wawepo kwenye maeneo waliyopangiwa. Machinga yoyote anayefanya biashara mbele ya duka la mtu aliyesajiliwa kwenye mfumo naye ni lazima atoe risit za EFD kama wenzake.
Tatu, badala ya kuhusisha task force na mengineyo TRA ijikite kwenye kaguzi za kushtukiza kwenye maduka au waajiri kampuni za ukaguzi wa mahesabu kuwasaidia kufanya kazi wanapohisi pana ubadhirifu. Kwa kuwa stock zitakuwa zimesajiliwa kwenye mfumo itakuwa ni rahisi kujua ubadhirifu.
Faida za uwepo wa INVENTORY MANAGEMENT SYSTEM
Kwanza, kutakuwa na udhibiti mzuri wa stock utakaowezesha kufanya makadirio sahihi ya Kodi. Kupitia kwenye mfumo TRA itajua ni mzigo kiasi gani mfanyabiashara alioingiza, kiasi gani alichouza na kwa kiasi gani alichouza na kilichobaki ni kipi kwa hiyo itawezesha kufanya physical stock taking kwa urahisi na kujua udanganyifu.
Pili, Mfumo utarahisha ufanyaji kazi wa TRA na kuweka kwa uwazi mkubwa shughuli za wafanyabiashara na walipakodi
Wanasema namba hazidanganyi, mfumo huu utapunguza udanganyifu kwa kiwango kikubwa na matukio ya kupika stock ili kulipa kodi pungufu yatapungua.
Tatu, mfumo huo utatumika kama mbadala wa usajiri wa stoo kwa sababu imezoeleka wafanyabiashara kutumia stoo Kama kichaka Cha kutoa bidhaa bila risiti hivyo kwa kuwa mfumo huu utasaidia kujua inventory nzima ya mfanyabiashara tafsiri yake tutaijua tu stoo kwa sababu kwenye physical stock taking stoo pia itaoneshwa.
Ni hayo tu kwa leo