Tetesi: Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ( SABASABA ) kudorora tena kwa mara nyingine

Nilikuwa na moto wa kwenda Sabasaba baada ya kuondoka nchini kwa miaka mingi.

Nilivyorudi nilikuwa disappointed.

Nilikuta Sabasaba pameachwa bila matengenezo miaka mingi, vyoo vinanuka kiasi cha kuweza kusababisha magonjwa, kilichonisikitisha zaidi, mabanda mengi yakikuea yanafungwa saa 12. Nikauliza kwa nini? Wakasema wanaogopa wizi usiku.

Nikaona kuna sababu nyingi uchumi wetu unakuwa na matatizo mengi.
 
Ni kweli mkuu, huwa wanakuja kuuza bidhaa zao sio maonyesho, mwaka huu itakuwa maonyesho ya kweli na kutoa bidhaa za bure za promosheni
Hao wa kimataifa watakuja kumuonyesha nani bidhaa zao wakati wanajua wafanyabiashara wa ndani wanaogopa kufanya uwekezaji kwa hofu ya kukamatwa
 
M

Maonesho kama neno linavyomaanisha ni watu waingie kuona, watapata taarifa za bidhaa... ubora, bei, matumizi, faida nk... biashara itaanza pale na hasa baadae... pale ni matangazo ya bidhaa... hali itakapokuwa nzuri bidhaa zitauzika tuu... sio lazima pale.... Sabasaba sio mtaa wa Kongo au Karume...
Mbona pale mlimani city na rock city mail huwa tunaingia bureee na kuna hadhi kuliko huko sabasaba, tena na uchumi wenyewe huu siji kabisa
 
Nayataman sana tena siku ya kwanza tu naenda na suzuk carry kusomba vya bure bure halaf nakuja kuwaumiza mtaan
 
Nilikuwa na moto wa kwenda Sabasaba baada ya kuondoka nchini kwa miaka mingi.

Nilivyorudi nilikuwa disappointed.

Nilikuta Sabasaba pameachwa bila matengenezo miaka mingi, vyoo vinanuka kiasi cha kuweza kusababisha magonjwa, kilichonisikitisha zaidi, mabanda mengi yakikuea yanafungwa saa 12. Nikauliza kwa nini? Wakasema wanaogopa wizi usiku.

Nikaona kuna sababu nyingi uchumi wetu unakuwa na matatizo mengi.
Vibaka wote wanahamia hapo , polisi baada ya kujinyakulia rushwa mlangoni wakati wa mchana , huelekea banda la Kizota kula Kitimoto .
 
Kwa kuzingatia uzoefu maonesho ya aina ile na maudhui Yake ni kuwa ilipaswa Watu wawe wanaingia bure ili mradi kunakuwa na umakini mkubwa ktk kuzingatia ulinzi na usalama Kwa ujumla wake ndivyo nchi nyingine kufanya, sasa haya ya hapa kwetu sijui Kwa nini wanataka Watu waingie Kwa kulipia ? Yani kwenda kuona bidhaa au huduma zinazozalishwa au kuuzwa na Watu au makampuni Mimi mwananchi nilipie? yani ni Kwa mfano Mtu anataka kuingia Kwenye Mall au supermarket halafu Kabla ya kuingia aambiwe lipa kwanza kiingilio kwa pesa ndo ukafanye window shopping au ukanunue unachotaka, je hiyo inaingia akilini? Binafsi naona siyo Sawa hata kidogo! Mwenye hoja tofauti aseme!
Uko sahihi mkuu.
 
Vibaka wote wanahamia hapo , polisi baada ya kujinyakulia rushwa mlangoni wakati wa mchana , huelekea banda la Kizota kula Kitimoto .
Kuna kipindi miaka ya tisini nilikuwa naingia Sabasaba baada ya kutoka kazini. Nimeulamba, simu kwenye mkanda.

Kibaka mmoja akanitime akachukua simu.

Hakujua kwamba ni kama nimesomea Israeli na sijawahi kuibiwa.

Nikamshtukia palepale, bado kidogo nimuitie mwizi watu wamchome moto.

Akanirudishia simu yangu.

Kwa hiyo naelewa vibaka wanahamia, lakini polisi kama unavyosema, wanacheza.
 
Hapana, hii ni namna ya kuchuja vibaka, wavuta bangi, wakabaji na watu wengine wa aina hiyo.

Hiyo haipaswi kuwa njia pekee ya kuchuja vibala, wezi na wavuta bangi, njia nzuri Ni kuimarisha ulinzi Na usalama tu that is the best practice na kuwapa wananchi mzigo wa kulipa viingilio ! Mbona Kariakoo Watu huenda bila viingilio? Mbona Kwenye ma malls Na super market Watu huingia bila viingilio? Kwa hiyo hoja yako haina mashiko!
 
Yanaitwa Maonesho ya biashara , lakini ukweli ni kwamba pamoja na bidhaa kadhaa kuonyeshwa , Wafanyabiashara tumetumia nafasi hiyo kuuza , tena kwa mauzo ambayo huvunja rekodi .

Sasa kutokana na kwamba almost 85% ya wateja wetu ni hawa wananchi wa kawaida ambao wamepigika vibaya sana kiasi cha kushindwa hata kumudu milo mitatu , basi tutegemee maumivu.

Sababu za kupigika kwa wananchi wa Tanzania zinafahamika .

Nachukua nafasi hii kuwatahadharisha wafanyabiashara wenzangu kwamba MAONESHO YA MWAKA HUU NI MAONESHO KWELI , NA WALA SI MAUZO TENA KAMA MLIVYOZOEA
Hv hua ni Maonesho au Maonyesho pls leo niwekeni sawa.
 
Hiyo haipaswi kuwa njia pekee ya kuchuja vibala, wezi na wavuta bangi, njia nzuri Ni kuimarisha ulinzi Na usalama tu that is the best practice na kuwapa wananchi mzigo wa kulipa viingilio ! Mbona Kariakoo Watu huenda bila viingilio? Mbona Kwenye ma malls Na super market Watu huingia bila viingilio? Kwa hiyo hoja yako haina mashiko!
Napendekeza pawe na kiingilio cha kuingia kko
 
Japo ni mapema lakini kuna kila dalili ya andiko hili kutimia .
 
Back
Top Bottom