Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,445
- 7,813
Leo waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa anazindua kituo cha Tanzanite Mirerani mkoa wa Manyara, kuwa nami...
=======
Waziri Mkuu: Nimekuja na salam zenu kutoka kwa mheshimiwa Rais, mama Samia Suluhu anawasalimia sana wana Mererani, pia makamu wa Rais. Viongozi wetu wanawatakia mafanikio makubwa kwenye kazi zenu, wale ambao mnafanya kazi za madini mpate mafanikio makubwa, mnaofanya kazi za kilimo, mlime mpate mafanikio makubwa. Mheshimiwa Rais ameniambia niwaambia nitakuja kuwatembelea.
Ndugu wanamirerani, ziara hii pamoja na kuja kuzindua, leo nimepata fursa ya kupita pembeni mwa mgodi wetu mkubwa, nilikuwa sijawahi kupita kuona hali hiyo.
Kwa kweli Kazi kubwa serikali imefanya, kujenga ukuta eneo hili lote na miundombinu yote tunayoiona hapa sio jambo la mzaha na wala msilione kama ni jambo tu la kawaida, limetibitishwa na idadi ya watu niliowakuta hapa, hapa panashika uhai wa watu.. Maisha ya watu yako hapa.
Lazima serikali tuweke utaratibu mzuri tuendelee kuona malengo yenu yanafikiwa. Ujenzi wa ukuta huu ni nia njema ya kuwafikisha huko mnakotarajia.
Tanzanite hii ndio inatusaidia kupata fedha za maeneo mengine.
=======
Waziri Mkuu: Nimekuja na salam zenu kutoka kwa mheshimiwa Rais, mama Samia Suluhu anawasalimia sana wana Mererani, pia makamu wa Rais. Viongozi wetu wanawatakia mafanikio makubwa kwenye kazi zenu, wale ambao mnafanya kazi za madini mpate mafanikio makubwa, mnaofanya kazi za kilimo, mlime mpate mafanikio makubwa. Mheshimiwa Rais ameniambia niwaambia nitakuja kuwatembelea.
Ndugu wanamirerani, ziara hii pamoja na kuja kuzindua, leo nimepata fursa ya kupita pembeni mwa mgodi wetu mkubwa, nilikuwa sijawahi kupita kuona hali hiyo.
Kwa kweli Kazi kubwa serikali imefanya, kujenga ukuta eneo hili lote na miundombinu yote tunayoiona hapa sio jambo la mzaha na wala msilione kama ni jambo tu la kawaida, limetibitishwa na idadi ya watu niliowakuta hapa, hapa panashika uhai wa watu.. Maisha ya watu yako hapa.
Lazima serikali tuweke utaratibu mzuri tuendelee kuona malengo yenu yanafikiwa. Ujenzi wa ukuta huu ni nia njema ya kuwafikisha huko mnakotarajia.
Tanzanite hii ndio inatusaidia kupata fedha za maeneo mengine.