Mimi nashangazwa na Manispaa ya Tabora Kupitia kwa Mkurugenzi na Afisa elimu idara ya sekondari, kwa kuamua kwa makusudi kabisa kutotenga fungu la kusomesha walimu kwenye budget, eti kwamba manispaa ya Tabora haina mpango huo. Cha kushangaza manispaa ya Tabora hata walimu walioko masomoni hawasaidiwi chochote, iwe nauli, ghalama za masomo na vingine, hata mbunge wetu kalinyamazia tu hilo halioni, AFisa elimu sekondari hana msaada kabisa kwa walimu, kila siku kugombana na walimu, Mkurugenzi kashindwa lao moja na afisa elimu sekondari. Wanajamii tusaidieni walimu Manispaa ya Tabora idara ya secondari kuna mdudu atatumaliza au wote tunaweza kukimbia kabisa. Tunahitaji michango yenu ya mawazo angalau Mbunge hatusaidii amekalia simba tu, Mkurugenzi hamna kitu, karibuni kwa mawazo.:tonguez: