Mangula: Najuta kuishi jimbo la Halima Mdee

Mangula: Najuta kuishi jimbo la Halima Mdee

Mangula na ashukuru kuwa walau amebahatika kupata zile nyumba za wizi, zilizouzwa kwa bei ya kupeana pale Osterbay. Hivyo walau ana pango na hatimaye CCM wamemkubuka tena na kupewa kibarua baada ya kuwa anaadhirika kwa kosa la kuumuzi bwana mkubwa JK.

Mtakumbuka kwenye uchaguzi wa 2005 Mangula alimshikia bango JK na kampeni yake akimtuhumu kufanya matumizi makubwa ya kupindukia wakati wa kampeni yake na hivyo kukiuka miiko ya Chama. Leo yupo pale kwenye wadhifa lakini namwogopa JK kama babake mzazi Mzee anaogopa kunyang'anywa mkate mkononi.
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Philip Mangula, amesema anajuta na anaona aibu kuishi katika Jimbo la Kawe linaloongozwa na Halima Mdee (Chadema), na kuwataka wanachama wa CCM kuhakikisha uchaguzi wa mwaka 2015 jimbo hilo linarudi kwao.
Mangula aliyasema hayo jana alipozungumza na viongozi mbalimbali wa kata na wilaya zote za jijini Dar es Salaam pamoja na viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam wa CCM.
“Ni aibu mimi ni mkazi wa Oysterbay jijini Dar es Salaam, na Mdee ndiye Mbunge wangu sasa siku akisema anataka kuongea na wazee wa jimbo lake mimi ntafanyaje? siwezi kwenda nitasingizia naumwa ili nisiende,” alisema.

Maswali yangu kwake ni haya:
-WanaCCM pekee wa jimbo la Kawe wanatosha kulirudisha jimbo CCM ktk sanduku la kura?
-Kwanini awe mwongo asisngizie kuumwa,kwani hana demokrasia ya kukataa kwenda kwenye kikao?

-Kinachomsababisha ajute ni kipi?

Makamu mwenyekiti ana akili mgando.
 
Back
Top Bottom