Francis12
JF-Expert Member
- Sep 30, 2016
- 7,533
- 22,276
Mange Kimambi: Mwanaharakati mwiba wa serikali ya Magufuli
Ikiwa ni zaidi ya miaka miwili sasa tangu Rais John Magufuli wa Tanzania aingie madarakani, rais huyo ameonesha kutokusita kukabiliana na wapinzani wake, kuanzia wanasiasa na hata viongozi wa dini.
Rais Magufuli amethibiti shughuli za kisiasa za wapinzani. Mikutano ya hadhara na maandamano ya kisiasa vyote vimezuiliwa, huku viongozi wote wa juu wa chama kikuu cha upinzani cha Chadema wakiwa wanakabiliwa na kesi mbalimbali mahakamani ikiwa ni pamoja na makosa ya kusababisha vurugu.
Serikali ya Rais Magufuli, ambaye ni muumini mzuri wa kanisa Katoliki, imetishia kuzifutia usajili asasi zote za kidini ambazo aidha zinajihusisha na siasa au kuzungumzia siasa katika mahubiri ya ibada
Lakini sasa rais huyo anakabiliana na upinzani mkubwa katika utawala wake kutoka kwa mwanaharakati wa kisiasa ambaye ushawishi wake bado unawashangaza wengi.
Mange Kimambi, mwanamitindo aliyebadilika kuwa mwanaharakati wa siasa, ndie muasisi wa maandamano yanayaopangwa nchi nzima kupinga kile anachokiita kuwa ni muendelezo wa ukiukwaji wa haki za binadamu na uminywaji wa haki za kiraia nchini Tanzania.
Mange, akiwa na wafuasi karibu milioni mbili kwenye ukurasa wake wa Instagram, ambaye miaka miwili iliyopita aliutumia ukurasa wake Instagram kumuunga mkono Rais Magufulu wakati wa kampeni za urais, leo hii anautumia ukurasa huo huo kuitisha maandamano makubwa ya kumpinga Magufuli na serikali yake.
Mange ni mama wa watoto watatu anayeishi nao Los Angeles, nchini Marekani. Harakati za mama huyo kumpinga Rais Magufuli zilianza kwenye mitandao ya kijamii takribani miezi sita tu baada ya rais huyo kupinga kuonyeshwa mubashara kwa shughuli za bunge kwasababu za kiuchumi.
Wafuasi wake, wengine wakiwa watumishi wa umma, wamekuwa wakimtumia taarifa mbali mbali zikiwemo zile zinazoaminika kuwa nyaraka nyeti za serikali, kufichua kile wasichokubaliana nacho juu ya mwenendo wa serikali.
Wapo wengi pia ambao wamekuwa wakimtumia picha na taarifa kuonyesha hali duni ya huduma za kijamii katika maeneo yao.
Mange ni mmoja wa watu wa kwanza nchini Tanzania miaka ya mwanzo ya 2000, ambapo alitumia kurasa zake kuzungumzia maisha yake na marafiki zake pamoja na mitindo ya mavazi. Lakini Mange alizungumzia pia habari binafsi mbalimbali za watu maarufu waishio ndani na nje ya Tanzania, wakiwemo walimbwende, wanamuziki na waigizaji filamu.
Wengi wanaamini habari hizi ndizo ziliwavutia watu wengi kuanza kumfuata katika kurasa zake za mitandaoni.
-Wakati ambapo shughuli za kisiasa za vyama vya upinzani zimedhibitiwa na watu kadhaa wamekamatwa na kushtakiwa kwa kuikosoa serikali kwa namna ambayo mamlaka haikupendezwa nayo, ukurasa wa Instagram wa Mange umefanyika sauti kuu kwa wakosoaji wengi wa serikali ya Rais Magufuli
Wakosoaji wa serikali na wanaharakati wa haki za binadamu wameendelea kuonya kwamba haki za kisiasa na uhuru vyombo vya habari na watu kujieleza vimeendelea kuminywa nchini Tanzania. Hata hivyo serikali imekuwa ikitupilia mbali madai haya.
Mara ya mwisho wafuasi wa upinzani walipoandamana mwezi Februari, makabiliano yao na polisi yalisababisha kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwilline ambaye inaelezwa kuwa alipigwa risasi kwa bahati mbaya.
Ikiwa maandamano haya yatafanyika ama la, ni jambo ambalo wengi wanasubiri kuliona. Lakini muitikio wa serikali katika kuapa kudhibiti maandamano haya umetafsiriwa na wengi kuwa ni mafanikio ya ushawishi wa Mange kupitia ukarasa wake wa Instagram tu, jambo ambalo vyama vingi rasmi vya upinzani nchini Tanzania vimeshindwa kulifanya.
Ikiwa ni zaidi ya miaka miwili sasa tangu Rais John Magufuli wa Tanzania aingie madarakani, rais huyo ameonesha kutokusita kukabiliana na wapinzani wake, kuanzia wanasiasa na hata viongozi wa dini.
Rais Magufuli amethibiti shughuli za kisiasa za wapinzani. Mikutano ya hadhara na maandamano ya kisiasa vyote vimezuiliwa, huku viongozi wote wa juu wa chama kikuu cha upinzani cha Chadema wakiwa wanakabiliwa na kesi mbalimbali mahakamani ikiwa ni pamoja na makosa ya kusababisha vurugu.
Serikali ya Rais Magufuli, ambaye ni muumini mzuri wa kanisa Katoliki, imetishia kuzifutia usajili asasi zote za kidini ambazo aidha zinajihusisha na siasa au kuzungumzia siasa katika mahubiri ya ibada
Lakini sasa rais huyo anakabiliana na upinzani mkubwa katika utawala wake kutoka kwa mwanaharakati wa kisiasa ambaye ushawishi wake bado unawashangaza wengi.
Mange Kimambi, mwanamitindo aliyebadilika kuwa mwanaharakati wa siasa, ndie muasisi wa maandamano yanayaopangwa nchi nzima kupinga kile anachokiita kuwa ni muendelezo wa ukiukwaji wa haki za binadamu na uminywaji wa haki za kiraia nchini Tanzania.
Mange, akiwa na wafuasi karibu milioni mbili kwenye ukurasa wake wa Instagram, ambaye miaka miwili iliyopita aliutumia ukurasa wake Instagram kumuunga mkono Rais Magufulu wakati wa kampeni za urais, leo hii anautumia ukurasa huo huo kuitisha maandamano makubwa ya kumpinga Magufuli na serikali yake.
Mange ni mama wa watoto watatu anayeishi nao Los Angeles, nchini Marekani. Harakati za mama huyo kumpinga Rais Magufuli zilianza kwenye mitandao ya kijamii takribani miezi sita tu baada ya rais huyo kupinga kuonyeshwa mubashara kwa shughuli za bunge kwasababu za kiuchumi.
Wafuasi wake, wengine wakiwa watumishi wa umma, wamekuwa wakimtumia taarifa mbali mbali zikiwemo zile zinazoaminika kuwa nyaraka nyeti za serikali, kufichua kile wasichokubaliana nacho juu ya mwenendo wa serikali.
Wapo wengi pia ambao wamekuwa wakimtumia picha na taarifa kuonyesha hali duni ya huduma za kijamii katika maeneo yao.
Mange ni mmoja wa watu wa kwanza nchini Tanzania miaka ya mwanzo ya 2000, ambapo alitumia kurasa zake kuzungumzia maisha yake na marafiki zake pamoja na mitindo ya mavazi. Lakini Mange alizungumzia pia habari binafsi mbalimbali za watu maarufu waishio ndani na nje ya Tanzania, wakiwemo walimbwende, wanamuziki na waigizaji filamu.
Wengi wanaamini habari hizi ndizo ziliwavutia watu wengi kuanza kumfuata katika kurasa zake za mitandaoni.
-Wakati ambapo shughuli za kisiasa za vyama vya upinzani zimedhibitiwa na watu kadhaa wamekamatwa na kushtakiwa kwa kuikosoa serikali kwa namna ambayo mamlaka haikupendezwa nayo, ukurasa wa Instagram wa Mange umefanyika sauti kuu kwa wakosoaji wengi wa serikali ya Rais Magufuli
Wakosoaji wa serikali na wanaharakati wa haki za binadamu wameendelea kuonya kwamba haki za kisiasa na uhuru vyombo vya habari na watu kujieleza vimeendelea kuminywa nchini Tanzania. Hata hivyo serikali imekuwa ikitupilia mbali madai haya.
Mara ya mwisho wafuasi wa upinzani walipoandamana mwezi Februari, makabiliano yao na polisi yalisababisha kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwilline ambaye inaelezwa kuwa alipigwa risasi kwa bahati mbaya.
Ikiwa maandamano haya yatafanyika ama la, ni jambo ambalo wengi wanasubiri kuliona. Lakini muitikio wa serikali katika kuapa kudhibiti maandamano haya umetafsiriwa na wengi kuwa ni mafanikio ya ushawishi wa Mange kupitia ukarasa wake wa Instagram tu, jambo ambalo vyama vingi rasmi vya upinzani nchini Tanzania vimeshindwa kulifanya.