PostGE2025 Mange Kimambi, "aliye engineer maandamano," akataa maridhiano

PostGE2025 Mange Kimambi, "aliye engineer maandamano," akataa maridhiano

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

barracuda

Member
Joined
Nov 2, 2025
Posts
31
Reaction score
140
Mange Kimambi, ambaye serikali kupitia Mwanasheria Mkuu ilisema ame "engineer" maandamano, amekataa maridhiano kwa kauli kali.

Kwa ushauri wangu, ujumbe wa serikali kuongea na Mange ujumuishe watu wenye heshma na credibility kutoka nje ya serikali. Uwe wa watu wasionuka damu. Hapo panaweza pakawa pa kuanzia.
 
Ni nani kwakwambia shida ya watanzania ni maridhiano? Ama ndo bado mnaendelea kuwaona watanzania ni wajinga?

Mkidhani hivyo mtazidi kupotea, watanzania wanataka haki yao iliyopotea na kupokwa. Wanataka kuheshimiwa tena, wanataka mashtaka kwa wanaostahili mashtaka.

Hawa wanaoleta maridhiano leo ndo walioshauriwa kukaa meza moja na watanzania wakagoma kata kata eti leo baada ya kuwa washapata walichokuwa wanataka sasa wanataka maridhiano ..this is satirical. Ni dharau kubwa sana
 
Mange kimambi ni mfanyabiashara .
Na wateja wake wakubwa ni ambao hata akiwaambia moja jumlisha 3 jibu lake 20 wanamwitikia.
Pakifanyika maridhiano biashara yake inakufa rasmi.
Hawezi kabisa kuridhia maridhiano
Unaridhiana na nani na kwa nini?

Sharti la kwanza la maridhiano ni wote walioua watajwe majina yao na washitakiwe
 
Kwa akili zako una amini mange ndiye aliye engineer maandamano?
Sijayasema mimi hayo.

Serikali ndio imesema "Mange Kimambi ame engineer maandamano." Kupitia Attorney General Hamza Johari.

LAKINI, MANGE KIMAMBI NA MARIA SARUNGI WANAWASHINDAJE SERIKALI USHAWISHI KWA UMAAAAAAA ?????????

Matakwimu yote mnayo nyinyi, ya matundu ya vyoo mliochimba, na ma pedi ya wasichana mangapi, na ma ndoo ya maji mliowatua kina mama vichwani, na mi mbegu ya mihogo isiyoliwa na wadudu.

Na mishule ya kata mlojenga, tumieni hayo matakwimu basiiiiiiii..... aaaah!!

Au hamyaamini hayo ma matakwimu ya huduma mlotoa ? Hapana, itakuwa hamyaamini. Mtoto wa Prof. Mkenda, Waziri wa Elimu, hawezi kusoma sekondari la kata la Yusuf Makamba, Mabibo kwa Mpalange. Ndo maana mnashindwa ushawishi mpaka na kina Recho Dangwa.
 
Endeleeni kuwa bize na Mange, vijana wana jambo lao tena 9D.

Mange alihamasisha maandamano April 26 utawala wa Magufuli, nani aliandamana?

Tofauti ya kipindi kile na sasa, watu wamekata tamaa.

Kaeni hivyo mkiamini vijana wanaandamana kwa kuwa Mange kasema. Mkija kushtuka itakuwa too late.
 
Mange Kimambi, ambaye serikali kupitia Mwanasheria Mkuu ilisema ame "engineer" maandamano, amekataa maridhiano kwa kauli kali.

Kwa ushauri wangu, ujumbe wa serikali kuongea na Mange ujumuishe watu wenye heshma na credibility kutoka nje ya serikali. Uwe wa watu wasionuka damu. Hapo panaweza pakawa pa kuanzia.
MARIDHIANO?
1. Kuridhiana nini?
2. Kuridhiana nani na nami?
3. Kuridhiana kitu gani?
 
Endeleeni kuwa bize na Mange, vijana wana jambo lao tena 9D.

Mange alihamasisha maandamano April 26 utawala wa Magufuli, nani aliandamana?

Tofauti ya kipindi kile na sasa, watu wamekata tamaa.

Kaeni hivyo mkiamini vijana wanaandamana kwa kuwa Mange kasema. Mkija kushtuka itakuwa too late.
Wanajifanya hamnazo,waache waendelee kushupaza shingo!
 
wewe unawashwa makalio, serikali ikae na changudoa wa wazungu kufanya mazungumzo, nyie ndio wale wateja wake nini? Mawazo ya kipumpafu kabisa haya, serikali ikae na mange kufanya mazungumzo kuhusiana na amani ya Tanzania? wewe ni Fala kweli. Nyie fanyeni hayo maanmano bana tusitishane kabisa. Muhimu msiharibu mali zetu tu. December nakaa na mkuki dukani kwangu.
 
Polepole alisema kuna wazee walikuwa tayari wanajipanga kwa ajili ya maridhiano kabla ya kiini macho kilichoitwa uchaguzi
 
Maridhiano yalitakiwa yafanyike kipindi hiki pitia uzi huu
 
Back
Top Bottom