Maneno ya Mwalimu Nyerere juu ya Udikteta

Maneno ya Mwalimu Nyerere juu ya Udikteta

Void ab initio

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2015
Posts
5,731
Reaction score
5,672
"Kuogopwa ni sifa na ada ya madikteta, viongozi halisi hawapendi kuishiriki sifa hii. Kujenga mazoea ya kutii viongozi hata katika mambo haramu ni dalili ya woga, ni kukaribisha udikteta." - Mwalimu Nyerere

C7lUlC7VUAATGGC.jpg


 
Sawa kabisa Mwalimu. Ndiyo maana tuliwafurahia hawa waalimu. Lakini sasa tuna mashaka.
 
Likiongozi linataka kuogopwa tu!! Mara ooh ningewapoteza. ..ntawafanyia ukatili!!
 
"Kuogopwa ni sifa na ada ya madikteta, viongozi halisi hawapendi kuishiriki sifa hii. Kujenga mazoea ya kutii viongozi hata katika mambo haramu ni dalili ya woga, ni kukaribisha udikteta." - Mwalimu Nyerere
Acha kuwa na kchw kama chá kuk ,lissu alimuelezeaje nyerere kuhusu huo idikiteta?.

Usiwe unakurupuka
 
Kuna Mwenyekiti wa kudumu wa Chama fulani ...haya maneno yatamuhusu.

Yaani hata akija na tamko la ajabu kiasi gani wafuasi hawahoji wao ni kufuata tu.
 
Walioishi kipindi cha utawala wa Mwl. Nyerere wanafahamu maana ya maneno hayo.

Balozi tu wa nyumba kumi alikuwa anaogopwa sana achilia mbali Rais Nyerere.

Wakati wa Mwl. Nyerere, katiba haikuwa hata na Tamko la Haki za binadamu.

Zidumu fikra za Mwenyekiti ulikuwa ni wimbo ambao lazima uimbe kila siku.
 
" kiongozi wa Tanzania lazima afate katiba kwani alichaguliwa kupitia kstiba,akaapa kuilinda, kiongozi asiefata katiba hatufai, hatutaki kiongozi anaeongoza kwa akili zake au kwa ushauri wa mkewe manake hatujui kesho mkewe atamwambia nn" mwalimu nyerere.

U- Umoja

K- Kupinga

U- Udikteta

T- Tanzania

"Hakuna kufanya siasa mpaka 2020" magufuli

"sijaribiwi hakuna kufanya mikutano wala maandamano"

Katiba. "vyama vya siasa vina haki ya kufanya siasa"

Katiba" kuna haki ya kukutana"


je Nyerere angekuepo Leo asingeshiriki operation UKUTA.
 
" kiongozi wa Tanzania lazima afate katiba kwani alichaguliwa kupitia kstiba,akaapa kuilinda, kiongozi asiefata katiba hatufai, hatutaki kiongozi anaeongoza kwa akili zake au kwa ushauri wa mkewe manake hatujui kesho mkewe atamwambia nn" mwalimu nyerere.

U- Umoja

K- Kupinga

U- Udikteta

T- Tanzania

"Hakuna kufanya siasa mpaka 2020" magufuli

"sijaribiwi hakuna kufanya mikutano wala maandamano"

Katiba. "vyama vya siasa vina haki ya kufanya siasa"

Katiba" kuna haki ya kukutana"


je Nyerere angekuepo Leo asingeshiriki operation UKUTA.
It is very true.

Kwa hotuba aliyotoa Mwalimu Nyerere mwaka 1995, ingetokea leo angekuwa hai, angesupport harakati za Ukuta kwa asilimia 100.

Kwa kuwa katika hotuba hiyo ya mwaka 1995, Mwalimu Nyerere alieleza wazi kuwa tunachagua Rais ili aweze kuitii na kuilinda Katiba kama alivyoapa wakati anakabidhiwa madaraka hayo kuwa ataitii Katiba na kuiheshimu.

Mwalimu aliendelea kueleza kuwa iwapo watanzania watachagua Rais ambaye hataitii na kuilinda Katiba aliongea bila kumung'unya maneno kuwa Rais wa aina hiyo HATUFAI........

Kitendo cha Mkuu wa nchi kupiga marufuku shughuli zozote za kisiasa hadi mwaka 2020 na wakati huo huo kuruhusu chama chake cha CCM kufanya shughuli za kisiasa bila 'kuguswa' na Polisi, ni dhahiri ni kuisigina Katiba ya nchi.

Inashangaza mno kwa wanaccm ambao siku zote husimama kwenye majukwaa ya kisiasa na kujinadi kuwa watamuenzi Mwalimu kwa vitendo, lakini kwa wosia huo muhimu sana kwa Taifa letu, wameamua kuupiga teke!
 
It is very true.

Kwa hotuba aliyotoa Mwalimu Nyerere mwaka 1995, ingetokea leo angekuwa hai, angesupport harakati za Ukuta kwa asilimia 100.

Kwa kuwa katika hotuba hiyo ya mwaka 1995, Mwalimu Nyerere alieleza wazi kuwa tunachagua Rais ili aweze kuitii na kuilinda Katiba kama alivyoapa wakati anakabidhiwa madaraka hayo kuwa ataitii Katiba na kuiheshimu.

Mwalimu aliendelea kueleza kuwa iwapo watanzania watachagua Rais ambaye hataitii na kuilinda Katiba aliongea bila kumung'unya maneno kuwa Rais wa aina hiyo HATUFAI........

Kitendo cha Mkuu wa nchi kupiga marufuku shughuli zozote za kisiasa hadi mwaka 2020 na wakati huo huo kuruhusu chama chake cha CCM kufanya shughuli za kisiasa bila 'kuguswa' na Polisi, ni dhahiri ni kuisigina Katiba ya nchi.

Inashangaza mno kwa wanaccm ambao siku zote husimama kwenye majukwaa ya kisiasa na kujinadi kuwa watamuenzi Mwalimu kwa vitendo, lakini kwa wosia huo muhimu sana kwa Taifa letu, wameamua kuupiga teke!
good justification nyerere ahusishwe katika operation ukuta
 
tunapinga dikteta uchwara in lissu's voice
Na kwa kweli katika kipindi hiki cha majaribu makubwa kwa Taifa letu, kazi ya Upolisi ndiyo itakayokuwa na changamoto kuliko kazi yoyote ile...

Kwa kuwa kwa ethics za Upolisi ni lazima utekeleze amri yoyote unayopewa na Mkuu wa kazi bila kutafakari kama amri hiyo ni halali au laa.......

Ni dhahiri kuwa amri watakayopewa Polisi na mabosi wao ya kuasambaratisha maandamano na mikutano ya Ukawa itakuwa siyo halali, lakini kutokana na ethics za kazi yao hawatakuwa na option nyingine zaidi ya kutekeleza amri watakayopewa ya kuwashughulikia wale raia wanaoitwa waleta fyoko fyoko.....

Hata hivyo Polisi nao wanapaswa kuzingatia ule msemo unaosema Cha kuambiwa changanya na akili zako.....

Bila shaka hawajasahau tukio la hivi karibuni kule Iringa ambako Askari wa cheo cha chini alihukumiwa kwenda jela miaka 15 kwa kosa la mauaji ya mwandishi wa Habari Daudi Mwangosi huku Kamu... handa aliyemuamuru Askari huyo kumlipua Mwangosi akiendelea kula kuku uraiani....

Ni dhahiri kuwa katika utekelezaji wa kuzima mikutano ya Ukuta, iwapo kutatokea maafa ni maaskari wa vyeo vya chini pekee watakaopandishwa kizimbani wakati mabosi wao waliowatuma kutekeleza jukumu hilo wakiwaacha uraiani wakila kuku........
 
Alitamka kuwa KATIBA hii ni ya kidikiteita na kuwa ikiipata dikiteita atawaumiza Watanzania. Kwa manufaa yake hakuirekebisha. Alikuwa nabii wa kuona mbali , aliona akaiacha hivyo. KWA NINI ALIFANYA HIVYO?
 
ndio maana hakuwahi kuvaa manguo ya kijani, ye muda wote kapiga gwanda
Kweli mkuu, tukichunguza sana wale wanaojisifu kuwa wao ni ccm , hakuna hata mmoja aliyebakia ambae ana mitazamo ile mizuri aliyokuwa nayo mwalimu, hawa ni watu tofauti kabisa, wanajinufaisha chini ya brand na legacy ya mtu mwingine tu, ingekuwa ni wao ndio waanzishe chama tungekuwa kama taifa lolote lile lenye migogoro, na ni vizuri tujiulize je wanakaribia kulimaliza salio la mwalimu, la umoja, ujamaa ,undugu na uzalendo, ,,, sijui likiisha hilo salio ni matukio gani yataanza hapa Tanzania, maana wanahasira na hilo salio, usiku na mchana wanasaka namna ya kulimaliza, undugu wetu , umoja na uzalendo unaisha sasa kwa kasi ya ajabu!
 
Back
Top Bottom