Hivi mwanamme ana maana gani anaposema 'girlfriend wangu wa kike' au mwanamke anaposema 'boyfriend wangu wa kiume'.Maneno haya nakutana nayo kila mara kwenye mazungumzo na watu na nimechoka kuwasahihisha.
Inategemeana ni nani anayeongea!Kama ni mtu mwelewa, basi ujue ni utani, lakini kama ni huku kwetu uswazi ujue ndo kamaanisha hivyo, na umsahihishe bila kuchoka kwa nia ya kumsaidia!Pole!
Rafiki ukichoka upumzike tu! Waache! Ujue dunia inajaa ujinga na wewe u nani kuokoa dunia??..... Maneno haya nakutana nayo kila mara kwenye mazungumzo na watu na nimechoka kuwasahihisha.
Hapo umenena nilishawahi kumsikia mtangazaji wa Clouds FM akisema barabara ya ocean Road nilicheka sana.hiyo kweli ipo! wabongo inabidi tubadilike! mfano: my wife wangu! hahahahahahaha, your husband wako! kazi ipo!