Manchester United (Red Devils) | Special Thread

  1. Newcastle united - tulikosa umakini
  2. Chelsea - tulikosa umakini
  3. Tottenham - waliomba mpira umalize
  4. Masharifu- hawajapiga shuti golini
Naendelea kusimama na kauli yangu:

Sikhofii kufungwa kwa manchester united ila nakhofia kutokufunga magoli kwa manchester united.

Karibuni jikoni west ham united,
Ukimuondoa manchester city, hakuna timu nyengine kwa premier league inayonipa khofu kwa sasa.

Nafahamu mpira una matokeo matatu ila hakuna timu inayoingia uwanjani wakiwa na malengo ya kupoteza mchezo au kutoa suluhu.
 
Gernacho kanifurahisha sana huyu dogo ana mguu mmoja safi sana apate mechi nyingi kama kina sancho hawataki kucheza wakae benchi.
Sema mlaini sasa akiguswa kidogo chali uyu afundishwe ROHO ngumu kama Gavi ni mdogo lakini kakichezewa kiatu kanaendelea tu labda aumie sana ndo atasimama...Foul kama 7+ zote kachezewa gnacho tu..BtW ni kafundi sana shida ndo iyo
 
Hakuna anayemchukia Ronaldo kama ata act proffessional,na atatanguliza maslahi ya Man utd mbele na kujua kwamba timu ipo kwenye stage ya rebuild.
Unachokiona mkuu ndio tatizo kubwa la Watu wa Tanzania. Mtanzania akiwa shabiki wa kitu au mtu, hata huyo mtu afanye madudu gani huwa hawayaoni na wako tayari kutetea hayo madudu kwasababu ya ushabiki.

wanadhani tunamchukia Ronaldo kwakuwa walitaka tusimame naye hata kwenye jambo lake la kijinga alilofanya dhidi ya kocha na timu nzima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…