Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hakuna anayemchukia Ronaldo kama ata act proffessional,na atatanguliza maslahi ya Man utd mbele na kujua kwamba timu ipo kwenye stage ya rebuild.
Unachokiona mkuu ndio tatizo kubwa la Watu wa Tanzania. Mtanzania akiwa shabiki wa kitu au mtu, hata huyo mtu afanye madudu gani huwa hawayaoni na wako tayari kutetea hayo madudu kwasababu ya ushabiki.

wanadhani tunamchukia Ronaldo kwakuwa walitaka tusimame naye hata kwenye jambo lake la kijinga alilofanya dhidi ya kocha na timu nzima.
 

Umenena vyema kabisaa
 
Hakuna anayemchukia Ronaldo kama ata act proffessional,na atatanguliza maslahi ya Man utd mbele na kujua kwamba timu ipo kwenye stage ya rebuild.
Ronaldo ni mkubwa kuliko Ten Hag kimaendeleo, kipesa ,kiuchumi ,kimataji ,yaani everything that's why hata jana kampanga CR7 baada ya ban vs Chelsea hapo Ten Hag anaomba Mungu Ronaldo contract iishe coz atakuwa na 38 na yeye ataridhia kusepa kwenda may be USA or China or Uarabuni kula maisha Ronaldo anamtesa sana Ten Hag I am telling you
 
Niliamini Ten Hag atatubadilisha ila sikufikiria kama ingekuwa faster hivi. Binafsi sina kabisa ile hofu ya kufungwa tukicheza hiki ni kitu ambacho nilikuwa nacho ndani ya United ya 1999 mpaka 2009.

Siku hizi tukiingia uwanjani hata tusipopata matokeo ila unaona kabisa hatukuwa na umakini ktk umaliziaji. Sio kitu cha kawaida hiki kila tukiingia kucheza tunatengeneza zaidi ya nafasi 5 ndani ya mchezo mmoja.

Naamini huyu mshua akileta wachezaji wake anaowahitaji amini amini nawaambia tutafungua sana champagne kila mwisho wa msimu unaomalizika. Tuna mtu mwenye uwezo mkubwa sana kiufundi.
 
Unaongea kiushabiki au kama mwanamichezo? Punguza utoto.
 
Uko sawa lakini Ten hag ndo boss utajiri wako peleka huko, akileta ujinga atakaa benchi hamna namna yani. Hatutaki kulea tena watu wapuuzi na attitude za kijinga kama kina pogba. Zimetucost sana miaka mingi watu wanaamua tu kugoma kocha anacheka cheka.
Yani alichofanyiwa Ronaldo sidhani kama kuna mchezaji mwingine ataleta ujuaji watawaza kama father kala benchi sisi je vitukuu.
 
Nilipenda sana uamuzi wa Ten hag jana kwa Antony jana..

Timu inahaha kutafuta goli watu wanatoka ulimi nje na jasho la kutosha, lenyewe limepokea mpira.. huku kulia Dalot kafungua chumba..Mbele pale Cesa kafungua kwenye box... Linyewe limepokea pasi safi badala ya kupress kwa Dalot au lichokonoe kwa cesa kule kwenye box linazunguka tu na ma spin yake ili kutafuta mkenue kwa mashabiki. Anakuja kutoa pasi too late na cesa kakata tamaa mpira ukaenda nje..

Baada ya kipenga cha break.. likapotelea hukohuko.. hakuna kurudi uwanjani. Wish Ten alimkanya sana.. Wenzako wanamoto sana wewe unaleta utoto..!!
 
[emoji28]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…