Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Lete link.

Tuone barcelona walipeleka ofa gani ambazo united ikatoa ofa nzuri kuwazidi barcelona.


Na ishu sio ofa tu,ishu ni mchezaji anataka kucheza wapi
 
Upo sahihi juu ya matakwa ya mchezaji.

Ila kipindi cha transfers watu wengi hua tunamfuatilia Fabrizio Romano, Mo, Piers kwakua ni waandishi ambao wana sources za ndani kiasi kwamba wakisema kitu juu ya mtu kuondoka au kuja hua haina kupindua.

Wote hao hakuna hata mmoja aliyewahi ripoti kama united wanakabiliwa na upinzani kutoka kwa timu zingine katika kutaka kuwasajili hao wachezaji ilikua ni united inaenda peke yake inarudi na mtu. Ni kama kwa Maguire.

Am simply saying hakuna credible source ambayo ina hii story ya kufanana na stori ya the times na wote tunajua the times ni gazeti la udaku kwa huko kwao. Ni kama vile uquote gazeti la Ijumaa Wikienda kama reference ya madai yako.
 

Well,skysport hao hapo juu.

Wakati wewe unafuatilia sajili za wakata majani kama Pablo Mari na wengineo mimi nilikuwa nafuatia kwa karibu usajili wa fundi huyu wa kireno na Barca walikuwa wanamtaka without a dought..Kwa VdB sitaki hata kubishana..tuishie hapa.
 
Ila kwa mchezaji kama Lacazete TV yako unaipiga pafyum kila asbuh na jioni, sio?

We kweli mpenda vibovu.
Mpenda vibovu siku zote havijui vikali, kwahiyo sikushangai unavyo mkanyagia Rashfood.

Rashfood hakuna taka taka yeyote ya kuilinganisha nayo pale Arsenal.

Hiyo pesa iliyo wekwa hapo ni gharama halali kwa mujibu wa wataalam wa maswala hayo, sasa wewe mkulima wa mihogo kutoka Tomoni unakuja unapinga.
 
Hahaha unamuita rashfood? Siyo rashford?

Anyway, rashfood ana magoli 9 katika ligi. Lacazette ana magoli 11 katika ligi na lacazette hachezi mechi zote.
 
Kama kuna timu ilimtaka Messi na ikashindwa maana yake hakuna timu ya kucompete na hivi vilabu vitatu sokoni.
Man united.
Barcelona.
Real Madrid.

Kama kuna mchezaji hazikumnunua ujue hazikuweka pesa tu.
Sancho Tu kipengele ...ndo iwe Messi 😂
 
Castr huu mjadala hautaisha kwa kuwa unahamisha magoli kila mara.
Hoja yako ya msingi ilikuwa inabase kwenye financia muscles za man utd dhidi ya timu washindani kwenye sajili za wachezaji. Lakini mkuu Daemusin kakupa vielelezo kuwa sababu ya kushindwa kwa united haikuwa pesa bali sababu tofauti na hapo,ukabadili upepo.
Kwa klabu kama united kuwekewa kipengele cha buy back sio sahihi,haikuwa level yetu kamwe.
 
Ni Arsenal na timu zingine ndogondogo ndiyo zinaweza kubali kuweka buy back Clause na Release clause za kipuuzi kwa wachezaji zinazowanunua.
 
Itakua ajabu mimi nikisema united haikua na pesa za kusajili hao watu. Na hakuna sehemu nimesema united haina pesa ya kusajili, nilisema imetaka watu na kuwakosa na nikasema walipoenda.

Nikaonyesha wachezaji iliowapata na kwamba hao wachezaji hawakushindaniwa na timu nyingine.

Kama kuna sehemu nimesema kwamba united ilikosa hao wachezaji kwakua haina pesa onyesha.
 
Kweli kabisa mdau jamaa anahamisha sana magoli
 
Bwana mdogo mbona nilivyoleta link ya skysport umekula kona hadi ndala umeziacha hapa?
 
Kama Jesse' anarudi basi VdB atafutiwe timu akacheze..He is still young na akienda timu inayom-suit atacheza.

Lakini je atafanya anachofanya Westham kwa sasa?..
Timu yetu inacheza vibaya sana ni kama hawafanyi training siku hizi za pattern ya kucheza tunapata magoli kwa papatu papatu tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…