Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Udhaifu.

Miaka 16.

Hakyamungu sijakuelewa.
 
Hakika Arsenal hawako kwenye mpito tena wako kwenye mporomoko tayari.
 
1. Jones: 9 seasons completed, 224 games played (in all competitions), average of 25 games per season with his average dropping to 19 games per season in the last 5 years.
2. Bailly: 4 seasons completed, 83 games played (in all competitions), average of 20 games per season
3. Rojo: 5.5 seasons completed, 122 games played (in all competitions), average of 22 games per season

mpaka muda huu harry maguire ameshacheza mechi takribani 50


kama hizi takwimu zina ukweli basi hawa jamaa ni watumishi hewa
 
Mkuu pia kuna ile "kitu kikiwa sio chako kuna namna una kizingatia"..maybe hiyo ndo sababu,don't forget about that

ila perfomance zao sidhani kama ni za kutisha au ni perfomance ambazo hawakuwahi kizitengeneza wakiwa na sisi
 
Ukweli ni kwamba Phil Jones toka asajiliwe United amekuwa fringe player tu kila msimu.

Misimu mitano iliyopita huenda Phil Jones vitanda vya wagonjwa vya pale Carrington vitakuwa vinamtambua kwa sura na jina kiasi cha kumkumbuka asipovilalia.

Marco's Rojo na Bailly hizi nazo ni failed project na hazitatusaidia tena kwa hali ilivyo tuna kila sababu ya kuachana na Bailly tusajili beki mwingine wa maana badala ya kuwa na beki ambaye muda mwingi yuko kuuguza majeraha.
 
Bailly nahisi kalogwa kijijini kwao
Jamaa ana gundu hatari.....
 
Bailly nahisi kalogwa kijijini kwao
Jamaa ana gundu hatari.....
Uchezaji wa Bailly na Phil Jones hautofautiani sana wanatumia nguvu nyingi sana uwanjani hivyo kuumia ni jambo lisiloepukika.

Kama uliangalia mechi ya Man united na Shelfield ya 3 -3 Phil Jones alianguka mara nyingi sana nilitegemea akitoka uwanjani lazima awe hospitalized ni kweli toka mechi hiyo hajawahi kuonekana uwanjani tena.
 
Adidas waache ujinga

Mbona wanawafyatulia Arsenal kits kali?..iweje sisi tuletewe home kit ya 2020/2021 ambayo ni mfanano wa 2017/2018 away kit?
nilichojifunza:
man utd tumekuwa na desturi ya kujitofautisha na team nyenginezo kwenye ishu ya designing ya jersey.....

angalia jersey za real madrid na AC milan (miaka yote zinakuwa na mfanano fulani) na wote wapo chini ya adidas kama sisi.
lakini ukija kwetu ni uhuni mtupu, material yanayotumika yanaweza kuwa ni ya kisasa lakini muonekano wa jezi mbele ya hadhira ukawa unatia shaka.

designer wa jezi ni kampuni au timu husika?
 
Si ndio ile mechi tulicheza mabek wa kati i wa3 nyuma ?
Nakumbuka alikuwa anaanguka km vile hana kichwa !!!!
 
Si ndio ile mechi tulicheza mabek wa kati i wa3 nyuma ?
Nakumbuka alikuwa anaanguka km vile hana kichwa !!!!
Hiyo mechi hajawahi kuonekana popote hata kwenye benchi sijui alipata injury kubwa kiasi gani
 
Nilifuatili nikaona sehemu kuwa Adidas ndo wanaosimamia kila kitu kuanzia kudesign..lakini Puma wanaodesign ni designers wa timu wakishirikiana na wa kampuni..but i'm not 100pc sure about that
 
Adidas waache ujinga

Mbona wanawafyatulia Arsenal kits kali?..iweje sisi tuletewe home kit ya 2020/2021 ambayo ni mfanano wa 2017/2018 away kit?

Rubbish
Ninachoona jezi ya Arsenal ni kali kutokana na rangi zake, nyekundu na nyeupe ni combo moja ya hatari sana. Hii jezi yetu full red na vi-stripe vyeupe vya adidas havina mvuto.

Hiyo jezi hapo chini ni kali kutokana na mchanganyo wake wa rangi. Designer wa adidas anapofeli ni kukosea hadi away na 3rd kits.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…